Habari za Punde

Soko la kisasa linahitajika Tumbe

Na Miza Othman / Rahma Khamis- Maelezo

Serikali imetakiwa na Wananchi wa Kijij cha Tumbe  kujenga  soko la kisasa ili kuweza kuendeleza kufanya biashara zao kwa ufanisi na kuepukana usumbufu usio wa lazima.

Hayo yamesemwa  na Waziri wa Mifugo na Uvuvi  Abdilah Jihad Hassni leo huko Baraza la wawakilishi Chukwani nje kidogo ya Mjiwa Zanzibar   wakati akijibu sualila la Mwakilishi wa Jmbo la Wawi Saleh Nassor Juma

 Kutaka kujuwa Sababu zilizopelekea kulazimishwa wavuvi warejee kuuza samaki wao katika soko la Tumbe  wameshaachana nalo kwa muda mrefu.

Amesema Serikali inawajibu wa kuwataka Wavuvi hao waondoe tofauti zao na kurudi kutumia miundombinu iliyogharimu Miliono mia saba za mkopo wa uhisani wa Benki ya dunia kutumika ipasavyo.

Waziri Abdilah Jihad amesema Wizara yake kupitia mradi huo ulifanikisha kuanza ujenzi wa soko  ndani ya mwaka 2011 na kumalizika mwaka 2014 itapelekea kutofahamiana baina ya wenyeji wa Tumbe na maeneo mengine wanaoleta samaki hao.


Aidha ameeleza kuwa kutokana na hali hiyo wavuvi wamaeneo mengine wanaoleta samaki wao katika diko hilo wametakiwa wasivue samaki kwa mfumo wa kuzamia chini ya Bahari katika mwezi wa Ramadhani kwani uzamiaji huo hupelekea wavuvi hao kutokuwa na funga ,wanapouza samaki wao madhambi yao yanakwenda kwa wananchi wa kijiji hicho.

Hata hivyo wananchi wametakiwa kuondowa tofauti zao na kulitumia soko hilo vizuri ili kuljitea maendelo ndani ya biashara zao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.