Habari za Punde

Wadau wataka serikali zisimamie ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa SDGs


  Afisa Mkuu wa uwakilishi wa Kudumu wa  Tanzania  katika Umoja wa Mataifa, Bw. Songelael Shilla,  akizungumza wakati wa Mkutano wa pembezoni ( Side-Event) ulioandaliwa  kwa ushirikiano  kati  ya Uwakilishi na Asasi za Kimataifa,   kwaajili ya kubadilishana mawazo kuhusu nafasi za  Ki Kanda  na  Kitaifa katika  mfumo wa ufuatiliaji na  udhibiti,  fursa na  changamoto za  Malengo  ya Maendeleo  Endelevu baada ya 2015 kwa upande wa Afrika.
 Sehemu ya  Washiriki wa mkutano huo wa pembezoni ambapo washiriki  pamoja na mambo mengine walisisitiza haja na umuhimu wa wananchi kushirikishwa kikamilifu  katika eneo hilo la ufanyaji wa tathmini na  ufuatiliaji kwa kile walichosema malengo hayo ya  maendeleo endelevu yanawahusu wananchi  hiyo ushiriki wako ni muhimu
 Sehemu ya Sehemu wa Washiriki wa mkutano huo wa pembezoni ambapo washiriki  pamoja na mambo mengine walisisitiza haja na umuhimu wa wananchi kushirikishwa kikamilifu  katika eneo hilo la ufanyaji wa tathmini na  ufuatiliaji kwa kile walichosema malengo hayo ya  maendeleo endelevu yanawahusu wananchi  hiyo ushiriki wako ni muhimu


Na Mwandishi Maalum, New York

Mchakato  wa  ukamilishaji wa   Malengo Mapya ya Maendeleo endelevu  baada ya  2015 ( SDGs)  umeingia katika hatua nyingine muhimu ambapo,  nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanakutana    hapa makao makuu ya UM   wakijadiliana kuhusu mfumo wa ufuatiliaji  na   tathmini ya  malengo  hayo.
Mkutano huo   unaojadili aina ya mfumo wa ufuatiliaji na tathmini, utafanyika kwa siku  nne na umeanza siku ya jumatatu  kwa wajumbe kutoa  mchango wa maoni  na  mawazo yao kwa kuzingatia rasimu  iliyowasilishwa na wenyeviti- wenza wa mchakato wa majadiliano  juu ya ajenda na malengo ya maendeleoe endelevu baada ya  2015.
 Karibu wajumbe wote waliozungumza katika siku ya kwanza   ya majadiliano haya, wametoa mapendekezo yao yanayotaka  mfumo  huo wa ufuatiliaji na tathmini uwe wa nama gani.

Akizungumza kwa niaba ya  Kundi la Nchi 77 na China ( G77&China)  Mwakilishi wa Afrika ya Kusini amesema    nchi zinazounda kundi hilo  wangependa kuona kwamba mambo yafuatayo pamoja na  mengine mengi  yanazingatiwa katika eneo hilo  la  ufuatiliaji na  tathmini.
Baadhi ya  mapendekezo ya  G77na China  ni   mfumo wa ufuatiliani na  tathimin uwe na  upeo mpana   na umilikiwe na nchi husika kwa  kuzingatia mazingira yake, mahitaji yake na vipaumbele vyake.
Kundi hilo limetaka pia  ufuatiliaji na tathmini,  eneo ambalo ni muhimu katika utekelezaji wa  SDGs lazima uongozwe na kusimamiwa na serikali na uwe wa hiari  uzishikisha  Wizara   mbalimbali  na  wadau wengine ambao wataonekana kuwa ni muhimu.
Vile vile kundi  la  G77 na China limesisitiza haja na umuhimu wa  kuhakikisha kuwa  mfumo wa  ufuatiliaji na tathmini unapaswa uwe  ujumuishi na wenye uwiano   ukizingatia pia ajenda namba 17 na malengo yote 169.
Kundi hilo la  77  na China pia  limeleza kwamba ni kwa  kupitia mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ndipo  ambapo Umoja wa Mataifa utakuwa katika nafasi   nzuri kutathmini utekelezaji wa  ajenda za maendeleo baada  ya 2015   ili kuhakikisha kwamba lengo kuu la   malengo hayo  ambalo ni  kuondoka umaskini linafikiwa.
Wachangiaji wengine wamesisitiza  umuhimu wa uwazi, ushirikishwaji na uwajibikaji wa makundi yote zikiwamo  Taasisi  na mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Baadhi ya wazugumzaji  wameeleza   umuhimu wa matumizi sahihi ya takwimu,  uwezeshwaji katika ukusanyaji wa takwimu hizo ikiwa ni pamoja na  umuhimu wa   ushiriki wa Asasi zisizo za kiserikali katika  mchakato huo wa ufuatiliaji  na tathmini.
Wachangiaji wengine wamekwenda mbali zaidi kwa kutaka ushiriki na ujumuishi wa wananchi katika  eneo hilo kwa kile wanachosema  ili utekelezaji wa  malengo hayo  uwe wenye tija wananchi wanapashwa kuwa sehemu ya    kufanya  tathmini na kufuatilia kwa kuwa  eneo kubwa la SDGs   linahusu wananchi.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inashiriki kikamilifu katika  majadiliano yote  muhimu ya mchakato mzima   maandalizi ya  SDGs ambapo wawakilishi wa  kutoka Wizara ya  Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Kimataifa,   Tume ya Mipango Tanzania Bara na  Visiwani na  Wawakilishi  kutoka Asasi zisizo za  Kiserikali wamekuwa wakihudhuria mijadala hiyo ikiwa ni pamoja na kusimamia maslahi ya  Tanzania na  Bara la  Afrika  katika ujumla wake.
Aidha  Tanzania  Kupitia Mwakilishi wake wa Kudumu  katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi ni  kiongozi wa majadiliano   ( lead negotiator) kuhusu SDGs kwa  Kundi la Afrika.
Pamoja na   majadiliano ya jumla kuhusu mfumo wa  tathmini  na  ufuatiliaji,  palikuwapo  na mijadala ya pembezoni ( side events)  iliyoandaliwa na wadau mbalimbali,   moja ya mijadala hiyo ya pembezoni  ni  ule  uliojadili nafasi za  Ki Kanda  na  Kitaifa katika  mfumo wa ufuatiliaji na  udhibiti,  fursa na  changamoto za  Malengo  ya Maendeleo  Endelevu baada ya 2015 kwa upande wa Afrika.
Mjadala huo  na ambao uliwashirikisha wadau mbalimbali kutoka nchi wanachama na Asasi zisizo za Kiserikali  uliandaliwa kwa ushirikiano kati  ya Uwakilishi wa Kudumu wa  Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Asasi   za Africa CSOs Working  Group on Post  2015, Beyond 2015, Africa Development Interchange Network na Africa   Monitor.
Akichangia uzoefu wa Tanzania katika eneo la  tathmini na Ufuatiliani,  Afisa  Mkuu wa Uwakilishi wa Kudumu,  Bw.  Songelael Shilla,   amewaeleza washiriki wa mjadala huo kwamba,  baadhi ya mambo ambayo yalichangia kwa kiasi   Fulani udhaifu katika utekelezaji wa   Malengo ya Maendeleo ya  Millenia ni pamoja na  ushirikishwaji  hafifu wa jamii kuanzia ngazi ya wilaya,  kata na .
Vile  Matatizo  katika eneo la Takwimu eneo ambalo pia lilisababia migongano miongoni wa  makundi mbalimbali  ya watendaji. Eneo  jingine ambalo alilitaja kuwa  limechangia  utekelezaji hafifu katika baadhi ya MDGs  ni ile la kutilia makazo   raslimali fedha kama ndio msingi mkuu wa  mafanikio  ya  MDGs.
Kwa sababu hiyo  Afisa  huyo ambaye alizungumza kwa Niaba ya  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  alisema Tanzania  inaamini na baada ya kujifunza  na uzoefu uliotokana na utekelezaji wa MDGs, kwamba mipango madhubuti, jumuishi  na iliyowazi katika mfumo wa ufuatiliaji na   tathimini ya utekelezaji  malengo  ya maendeleo endelevu baada ya  2015 utawezesha utekelezaji  wenye tija wa  SDGs.

Baadhi ya wazungumzaji katika  mjadala huo walisisitiza pia kwamba  kama  kweli Afrika inataka kupata mafanikio katika utekelezaji wa SDGs basi  haina budi kuwekeza kwa   wananchi wake ambao  ndio wadau  na walengwa wakubwa wa SDGs hizo, wakasitiza pia umiliki  wa mfumo huo na uwajibikaji wa wadau mbalimbali kuanzia serikali , jumuiya ya kimataifa,  asasi zisizo za kiserikali na wananchi  kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.