Habari za Punde

Dk Shein afutarisha Ikulu

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                  27.6.2015
---
RAIS  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein jana alishiriki futari ya pamoja na Wafanyakazi wa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma pamoja na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ.

Futari hiyo ya pamoja ilifanyika katika viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar ambapo pia, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad, Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Pandu Ameir Kificho, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa BLW Dk. Abdulhamid Yahaya Mzee na viongozi wengine wa Serikali.

Akitoa neno la shukurani kwa niaba ya Mhe. Rais mara baada ya futari hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Mhe. Dk. Mwinyihaji Makame alisema kuwa lengo la futari hiyo ni kupongezana kwa wafanyakazi na viongozi wa Wizara hizo baada ya kupitishwa Bajeti za Wizara hizo katika Baraza la Nane la Wawakilishi lililofikia kikomo chake hapo jana ambalo lilivunjwa rasmin na Rais Dk. Shein.

Dk. Mwinyi alitoa pongezi hizo kwa niaba ya Rais kwa wafanyakazi na viongozi wa Wizara hizo kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kuhakikisha Wizara zao zinatekeleza majukumu yaliokusudiwa kwa lengo la kupata maendeleo na mafanikio makubwa zaidi katika Wizara hizo na Serikali nzima kwa juma.

Pia Dk. Mwinyi, alitumia fursa hiyo kuwashukuru viongozi,wafanyakazi hao pamoja na waalikwa wote kwa kuhudhuria futari hiyo maalum ya pamoja.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.