Habari za Punde

ZSSF Yatoa Elimu ya Mafao ya Uzazi na Kujichangia kwa Hiari


Afisa Mipango , Utekelezaji na Ufuatiliaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) , Khalifa Muumin Hilal,akielezea jinsi mfuko wa ZSSF unavyotowa huduma za Mafao kwa Wanachama wake  
Maofisa Utumishi na Mipango wa Ofisi za Serikali na Binafsi wakimsikiliza Ofisa wa ZSSF wakati wa mkutano wa kutowa Elimu ya Mafao ya Uzazi kwa Wanachama wake.

Afisa Mipango , Utekelezaji na Ufuatiliaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) , Khalifa Muumin Hilali, amewahakikishia Wananchi na Watoto kwa ujumla kuwa Watafaidika na matumizi ya Kiwanja cha Kufurahishia Watoto kilichoko Tibirinzi Kisiwani Pemba, katika Sikukuu ya IdilFitri inayokuja kwa vile Ujenzi wake umeshafikia asilimia 98%.

Akizungumza na mwandishi wa Habari hizi huko Kiwanjani Tibirinzi nje kidogo ya Mji wa Chake Chake Kisiwani humo, alisema ujenzi huo unatarajiwa kukamilika muda mfupi ujao kwa vile Pembea zote Tano zimeshafungwa na Umeme mkubwa ambao ulikuwa ni kikwazo cha kuzifanyia majaribio 

Mashine zilizopo Kiwanjani hapo tayari mafundi wako hatuwa za mwisho kumaliza kuunga.
Hilali, alieleza kuwa kazi kubwa iliobakia kwa sasa ni usafishaji wa kiwanja ambao unaendelea na umaliziaji wa Ujenzi wa Barabara ya Ndani ya Kiwanja ambayo imefikia hatuwa ya umaliziaji ambapo Mafundi walihakikisha kuwa kabla ya kumi la kwanza kumalizika watakuwa wameshamaliza kazi hiyo na tayari kwa matumizi.

“Tatizo letu kubwa tulilokuwa nalo ni Umeme wa Uhakika ( mkubwa ) na tayari mafundi wapo na wameshafunga Transfoma na mashine nyengine na Waya umeshafika Kiwanjani kutokea Wesha ni kiasi cha kuunganisha tu kwa majaribio na Pembea iliobakia mafundi wa Kichina wanasubiri kukamilika kwa uunganishaji wa Umeme wamalize kufunga na kufanya majaribio,” alisema .


Kwa Upande wa Meneja wa Mfuko huo Pemba, Rashid Abdalla Moh’d, alisema kuwa kazi iliobakia ni ndogo nan i ukweli Kiwanja hicho kitatumika kwa Sikukuu ya IdilFitri inayokuja , baada ya watoto kukikosa kwa muda mkubwa sasa kwa vile ujenzi umefikia hatuwa za mwisho.

Akizungumzia suala la bei ya Kiwanja kwa mtu atakae ingia , alieleza kuwa ni Tshs 1,000/= kwa Mtu mzima na 500/= kwa mtoto na hiyo haina utafauti baina ya Unguja na Pemba.

“ Tatizo letu lilikuwa ni Umeme mkubwa kwa vile hivi Vifaa haviwezi kwenda kwa Umeme mdogo uliokuwepo na tayari mafundi kutoka Kampuni ya Molel Electrical Contractors Ltd ya Dar-es-Salaam wanamalizia kuunganisha kutoka Waya unaotoka Wesha hadi humu ndani,” alieleza.

Nae Fundi Umeme kutoka Kampuni hiyo kutoka Kampuni hiyo, Engineer , Rwegoshora Clavers, aleleza kuwa kazi ya kuingiza Umeme ndani ya Kiwanja tayari imefikia hatuwa mzuri na tayari wameshafunga Transfomer kubwa Kiwanjani hapo na tayari wamesha unganisha na Mashine nyengine za kuendeshea Mashine za Kiwanjani hapo.

“ Wananchi wasiwe na Wasi wasi Shughuli ya Umeme imekamilika na tunawaahidi Kiwanja watakitumia bila ya Wasiwasi wowote,” alieleza Engineer huyo.


Watoto wa Kisiwa cha Pemba , wamekosa kufurahia Sikukuu katika Kiwanja hicho kwa muda mkubwa tokea pale Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF , kuamuwa kukifanyia matengenezo makubwa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.