Ndugu Zangu
Napenda kuchukua nafasi hii adhimu mbele yenu kuandika mada yangu tukufu kama ilivyotanjwa hapo juu.
Kwa niaba yangu binafsi, Wazanzibari na Watanzania wote kwa ujumla waliopo hapa Washington State na Nchini Marekani napenda kutumia nafasi ya kutoa maelezo ya vifaa vilivyopo hivi sasa katika Storage zetu kwa hatua kuvisafirisha kutoka Bandari ya Seattle hadi Zanzibar.
Vifaa hivi vimekusanywa na mimi kwa mashirikiano wafadhili mbali mbali waliojitolea kwa ajili ya kusaidia juhudi za maendeleo huko Zanzibar Tanzania ikiwemo Sefrioui Bassidy Foundation vifaa hivyo ni meza (tables) , computers , vigari vya kubebea wagonjwa wasiojiweza (wheel chairs) , vitabu (books) , na kadhalika.
Madhumuni makubwa ya kukusanya vifaa vyote ni mchango kusaidia juhudi za kuondoa kero mbali mbali zinazowakabili jamii yetu huko nchini kwetu katika huduma za afya na elimu kama ukosefu wa vitabu katika maktaba zenu, huduma za computer bado ni ngumu kupatikana ipasavyo katika shule mbali mbali pamoja na Hospitali nyingi kukosa huduma za vifaa kama wheels chairs na Walemavu kwa ujumla.
Napenda kutumia fura hii kama changamoto kuwaomba ndugu zangu Raia wema kutoka Nchini Marekani , Tanzania na Zanzibar kwa ujumla hususan waliopo nje kwa nia njema kuchangia hali na mali misaada ya kifedha kwa ajili ya Usafirishaji wa vifaa vyote viliopo sasa kutoka Seattle hadi Zanzibar mwezi July 2015.
Gharama za container lenye futi 40 ni dollars 6,500 bei hii imetokana na utafiti tuliofanya kupitia shirika la meli la Delma shipping line, Michango yote inakaribishwa kwa wote kwa kiwango cha aina yoyote na kutumwa katika account zifuatavyo
Jina : AMIN IBRAHIM ALLY
BANK OF CHASE WA ACCOUNT NO 622920028
Mchango unakaribishwa pia kwa njia cheque kwa jina hapo juu katika anuwani ifuatayo
1616 156th AVE NE APT 230 BELLEVUE WA 98007
na sisi wa UK mbona mumetusahau? tutachangia vipi?
ReplyDeleteNyie wa uk tumeni pesa kwa benki....mdau ushapewa acc.no ndo tuseme hujui ama ? Kama hujui basi Nenda aifanye Transfer......
ReplyDelete