Habari za Punde

Maalim Seif alipohudhuria mkutano mkuu wa Chadema uliompitisha Lowassa kuwa mgombea Urais na Duni kuwa mgombea mwenza

 Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akihutubia kwenye mkutano Mkuu wa Chadema uliofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chadema wakimsikiliza Maalim Seif wakati akihutubia kwenye mkutano huo. Kulia ni Mke wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chadema, Mama Regina Lowassa.
 Mwenyekiti wa Chadema Freema Mbowe (wa pili kushoto) akiwatambulisha mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema Mhe. Edward Lowassa, mgombea mwenza wake Mhe. Juma Duni Haji na Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad.


   Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema Mhe. Edward Lowassa,  akiwa na mgombea mwenza wake Mhe. Juma Duni Haji.
 Wagombea urais wanaowakilisha UKAWA wakibadilishana mawazo baada ya mkutano mkuu wa Chadema. Kushoto ni Mwenyekiti wa Chadema Mhe. Freeman Mbowe.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema Mhe. Edward Lowassa akisalimiana na Mwenyekiti Mwenza wa UKAWA Bw. James Mbatia.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema Mhe. Edward Lowassa, akisalimiana na mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad. (Picha na Salmin Said, OMKR)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.