JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
|
TAARIFA KWA UMMA
UWEKAJI WAZI WA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA KATIKA
MIKOA YOTE YA UNGUJA NA PEMBA.
Tume
ya Taifa ya Uchaguzi inatarajia kuweka Wazi Daftari la Awali la Wapiga Kura katika
Mikoa yote ya Unguja na Pemba kuanzia tarehe 03/09/2015 hadi tarehe 07/09/2015
ili Umma uweze kupata nafasi ya kulikagua Daftari la Awali na kutoa taarifa za
kufanyiwa marekebisho pale inapostahili.
Tume
ya Taifa ya Uchaguzi, inaomba wananchi wote wajitokeze kukagua Daftari hilo litakalowekwa
wazi katika Ofisi za Shehia, na ili kurekebisha taarifa za Wapiga Kura BVR Kit
zitawekwa katika ofisi za Wilaya. Wakati wa uhakiki Mpiga kura anaweza kuhakiki
taarifa zake kutumia simu ya mkononi kwa
kuingiza *152*00# au tovuti ya Tume www.nec.go.tz kisha
wafuate maelekezo, ili kama kuna mapungufu yaweze kufanyiwa kazi kabla ya
kuchapisha Daftari la mwisho litakalotumika siku ya Uchaguzi.
Imetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi
No comments:
Post a Comment