Habari za Punde

Hali ya Uzinduzi wa Kampeni ya Urais ya CCM Kibanda Maiti leo jioni Zenj.


Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Mgombea wa Rais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho tawala  Dkt. Ali Mohamed Shein wakionesha ilanui ya Uchaguzi ya CCM leo wakati wa uzinduzi wa kampeni za Urais mbele ya umati mkubwa sana katika uwanja wa Kibandamaiti mjini Unguja.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Mgombea wa Rais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho tawala  Dkt. Ali Mohamed Shein wakionesha ilanui ya Uchaguzi ya CCM leo wakati wa uzinduzi wa kampeni za Urais mbele ya umati mkubwa sana katika uwanja wa Kibandamaiti mjini Unguja.


Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia  leo wakati wa uzinduzi wa kampeni za Urais katika uwanja wa Kibandamaiti mjini Unguja.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiongea na umati mkubwa sana wa wananchi  leo wakati wa uzinduzi wa kampeni za Urais katika uwanja wa Kibandamaiti mjini Unguja.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mjini Unguja Mhe Borafya Silima akiwahutubia Wana CCM wakati wa uzinduzi wa Kampeni za Chama cha Mapinduzi iliofanyika katika viwanja vya Demokrasia kibanda maiti Zanzibar.



Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakiwa katika kiwanja cha Demokrasia wakimsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwahutubia na kutoa Ilani ya CCM.

 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe Jakaya Mrisho Kkwete akiteta jambo na Rais Mstaaf wa Zanzibar Dk Amani Abeid Karume baada ya kumalizika kwa mkutano wa uzinduzi wa Kampeni ya CCM iliofanyika katika viwanja vya ibanda maiti Zanzibar jioni hii.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na wananchiu wenye furaha baada ya uzinduzi wa kampeni za Urais katika uwanja wa Kibandamaiti mjini Unguja.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe Benjamin William Mkapa akiagana na viongozi wa CCM Zanzibar baada ya kuhudhuria na pia kuhutubia katika uzinduzi wa kampeni za Urais katika uwanja wa Kibandamaiti mjini Unguja.

PICHA NA IKULU
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe Benjamin William Mkapa akiagana na viongozi wa CCM Zanzibar baada ya kuhudhuria na pia kuhutubia katika uzinduzi wa kampeni za Urais katika uwanja wa Kibandamaiti mjini Unguja.
(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.