Kwa Habari, Picha na Matukio Tembelea ZanziNews
Tangaza nasi kwa bei nafuu (advertise with us ). Tupigie 0777 424152 au tuandikie (email) othmanmaulid@gmail.com
Mkurugenzi wa Uchaguzi Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Ndg.Salum Kassim Ali akitoa neno la utanguzlizi kuhusu wajibu wa wagombea wa Uchaguzi katika warsha ya siku moja kwa wagombea wa Uwakilishi yenye lengo la kuongeza ufahamu juu ya maadili ya Uchaguzi na kuibua hatua madhubuti katika kuimarisha Amani ndani ya kipindi hiki cha Uchaguzi, warsha hiyo ilifanyika tarehe 09/09/2015 Ukumbi wa Hoteli ya Hifadhi Zanzibar.
Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mh. Ayoub Bakar Hamadi akifungua warsha ya Wagombea wa Uchaguzi iliyofanyika tarehe 09/09/2015 Ukumbi wa hoteli ya Hifadhi Chake Chake Pemba, warsha hiyo ilikuwa na lengo la kuongeza ufahamu wa maadili ya Uchaguzi na kuibua masuala ambayo yanaweza kuzuia kuwepo kwa Uchaguzi wa Amani
Mgombea wa Uwakilishi kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi (CUF) Jimbo la Micheweni Mh. Subeit Khamis Faki akichangia Mada juu ya masuala ya rushwa katika warsha ya siku moja ya Wagombea wa Uchaguzi iliyofanyika Hoteli ya Hifadhi Pemba tarehe 09/09/2015.
No comments:
Post a Comment