Habari za Punde

Wagombea Uwakilishi Pemba katika Semina ya maadili ya Uchaguzi

DSC02941Mkurugenzi wa Uchaguzi Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Ndg.Salum Kassim Ali akitoa neno la utanguzlizi kuhusu wajibu wa wagombea wa Uchaguzi katika warsha ya siku moja kwa wagombea wa Uwakilishi yenye lengo la kuongeza ufahamu juu ya maadili ya Uchaguzi na kuibua hatua madhubuti katika kuimarisha Amani ndani ya kipindi hiki cha Uchaguzi, warsha hiyo ilifanyika tarehe 09/09/2015  Ukumbi wa Hoteli ya Hifadhi Zanzibar.
DSC02943Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mh. Ayoub Bakar Hamadi  akifungua warsha ya Wagombea wa Uchaguzi iliyofanyika tarehe 09/09/2015 Ukumbi wa  hoteli ya Hifadhi Chake Chake Pemba, warsha hiyo ilikuwa na lengo la kuongeza ufahamu wa maadili ya Uchaguzi na kuibua masuala ambayo yanaweza kuzuia kuwepo kwa Uchaguzi wa Amani
DSC02978Mgombea wa Uwakilishi kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi (CUF) Jimbo la Micheweni Mh. Subeit Khamis Faki akichangia Mada juu ya masuala ya rushwa katika warsha ya siku moja ya Wagombea wa Uchaguzi iliyofanyika Hoteli ya Hifadhi Pemba tarehe 09/09/2015.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.