VIONGOZI wa CCM Zanzibar wamewataka wananchi na wanaCCM kuwachagua viongozi
wa chama hicho ili waendelee kuwaletea maendeleo endelevu yaliotokana na
Mapinduzi ya Januari 12, 1964.
Hayo waliyaeleza leo huko katika mkutano
wa Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliofanyika Jimbo la Bumbwini, Mkoa wa Kaskazini
Unguja uliohudhuriwa na maelfu ya wanaCCM na wananchi ambapo mgeni rasmi
alikuwa mgombea nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed
Shein.
Viongozi hao wa CCM walipata fursa ya
kusalimiana na wananchi pamoja na WanaCCM waliohudhuria katika mkutano huo waliwataka
wanachi na wanaCCM kutambua historia yao na kutambua maendeleo yaliopatikana
baada ya Mapinduzi.
Bi Fatma Karume nae alipata fursa ya
kusa,limiana na wananchi na wanaCCM katika mkutano huo na kueleza kuwa Bumbwini
mpaka Makoba pamoja na Kiongwe kumshukuru MwenyeziMungu kwa kuwapa neema.
Alisema kuwa ASP iliundwa kwa lengo la
kuwatetea wanyonge na kuwasifu watu wa Bumbwini kwa kuiunga mkono CCM na
kueleza kuwa Mapinduzi ndio yalioleta na kama si Mapinduzi maendeleo Bumbwini
yasingepatikana.
Bi Fatma alisema kuwa watu wa Bumbwini
lazima wawe macho na wawakatae wapinga maendeleo na badala yake kinachotakiwa
hivi sasa ni maendeleo yanayoletwa na CCM na kuwaombea kura viongozi wa CCM.
Nae Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa
ambaye pia, ni Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za
SMZ Haji Omar Kheir alisema kuwa kabla ya Mapinduzi kulikuwa na skuli mbili
katika Mkoa huo ya Mkwajuni na skuli ya Donge lakini katika maeneo yote ya Mkoa
huo na baada ya hapo ndipo ikajengwa skuli ya Bumbwini na Kinyasini.
Alisema kuwa watu wa maeneo mengine
yaliobakia katika Mkoa huo hawakupata fursa ya kusoma na mara baada ya
Mapinduzi ndipo walipopata fursa na skuli nyengine zilipoanza kuenea pamoja na
kuwa na kituo kimoja tu cha afya cha Mkokotoni kabla ya Mapinduzi ambapo
wanaume waligeuzwa kuwa magoigoi katika majahazi.
Alisema kuwa kwa hivi sasa elimu, afya na
sekta nyengine nyinzi zimeimarika na hivi sasa maendeleo makubwa yapo katika
mkoa huo ambayo yamekuja baada ya Mapinduzi chini ya ASP na hatimae CCM.
Waziri Kheir alishangwa za na wale
wanaodai mamlaka kamili wakati tayari Zanzibar ina mamlaka yake kamili na
kusema kuwa anaamini kuwa CCM itarejeshwa madarakani kutokana na utekelezaji
mzuri wa Ilani na Sera zake.
Alisema kuwa wafuasi wa vyama vya
upinzani wamekuwa wakileta usumbufu mkubwa barabarani na kwa lengo la kutafuta
sababu za kuleta vurugu na kusema kuwa mwaka huu Zanzibar vurugu hazipo na
kuwataka wanaCCM kuvihifadhi vizuri vitambulisho vyao vya kupigia kura.
Nae Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd alisema kuwa ushindi wa CCM
hauna shaka wala hakuna wa kuuzuia na kusisitiza kuwa mwaka huu ndio mwisho wa
chama cha CUF.
Balozi Seif aliwataka wananchi wa
Kaskazini B kuanza kupamba maskani zao kwani ushindi wa CCM unakuja na kusema
kuwa upinza hivi sasa hauna hoja na hoja yao ni kumsema yeye katika mikutano
yao ya hadhara.
Katika maelezo yake alishangazwa na kauli
zinazotolewa na viongozi wa CUF kuwa yeye pamoja na Haji Omar Kheir na Hamza
Hassan watampelekwa The Hague, na kueleza kuwa viongozi wa kulepekwa huko ni wa
CUF kutokana na matukio mengi waliyoyafanya yakiwemo kusababisha maafa kwa
wananchi katika matukio kadhaa waliyoyatengeza kwa makusudi.
Balozi Seif alieleza kuwa CUF inaandaa
vurugu katika uchaguzi ujao kwa kutaka kujipanga huko Bwawani kwa lengo la
kusubiri matokea na yakiwa hayajawaridhisha wanakusudia waanze vurugu kuanzia
eneo hilo na kusisitiza wasijaribu kufanya hivyo kwani wenye kazi zao wapo.
Alisema kuwa chama hicho cha upinzani
hivi sasa kina mpango wa kutafuta fulana za CCM ili wafuasi wao wavae siku ya
uchaguzi kwa lengo la kufanya fujo, na kusisitiza kuwa CCM itahakikisha
inasimamia amani na utulivu na kusisitiza kuwa vyombo vya Dola vitasimia na
kuwadhibiti wale wote watakaofanya vurugu.
Aliwataka wapinzani kuacha kumsingizia
mambo ambayo hajayafanya kwani hizo sio siasa wala demokrasia ya vyama vingi,
ambapo pia alitumia fursa hiyo kuwaombea kura viongozi wa CCM akiwemo Dk.
Shein, John Magufuli na Mama Samia na kusema kuwa viongozi hao wakishirikiana
pamoja maendeleo makubwa yataendelea kupatikana nchini.
Naibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai
alitumia fursa hiyo kueleza mambo kadhaa ambayo ndiyo yanayokifanya chama cha
CUF kumchukia Balozi Seif Idd huku akieleza utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya
CCM nalo pia limekuwa ni mwiba kwa CUF.
Alisema kuwa watu wanaoweza kuwaunganisha
na kuwaongoza watanzania na wazanzibari ni Dk. Shein na Dk. Magufuli na Samia,
Wabunge, Wawakilishi na Madiwani wa CCM.
Balozi Amina Salum Ali kwa upande wake, alipongeza
maendeleo yaliopatikana katika Jimbo hilo pamoja na Mkoa mzima wa Kaskazini
ikiwa ni pamoja na uimarishwaji wa miundombinu ya barabara, huduma za afya,
umeme, maji safi na salama.
Alisema kuwa Dk. Shein ana mapenzi
makubwa na wananchi wakiwemo akina mama ambapo hali hiyo imekuwa ikionekana
kutokana na juhudi kubwa alizozichukuwa za
kuimarisha sekta za maendeleo zikiwemo huduma za afya hasa katika Jimbo
hilo.
No comments:
Post a Comment