Na Haji Nassor, Pemba
…HUU ni zaidi ya unyama...
Ahaa…kumbe
hawakukosea wahenga waliosema kuni inayoteketea jikoni, huchekwa na ilio
kando…….
Naamini
walikua na maana pana, kwamba ile kuni ilio kando haijui kuwa ikimaliza
iliojokoni ni zamu yake.
Kwenye
jamii, watoto ndio kuni zilizojikoni, na kuni za kando ni wazeeo, wengi husema watoto
ni taifa la kesho.
Wengine
husema ni taifa la leo, kauli zote hizo zinaingia akili, maana, wapo watoto
wameshatoa mchango mkubwa taifa kama vile michezo ya riadha, usanii na hata
kuhifadhi kura-an au bibilia.
Sasa
kama hayo yote yanaaingia akili, iweje jamii ya leo na wanaoitwa watu wazima wa
taifa hili, kuwafanyia unyama watoto wetu ambao tunakubaliana ndio taifa la leo.
Kwani
hawapo watu wanaoonekana na heshima zao na akili zao wanawanyanyapaa watoto
wanaoishi na VVU au hata wazazi wao waliokufa kwa sababu hizo.
Kisiwa
cha Pemba kama kilivyo cha Unguja, nacho kimejipatia umaarufa mkubwa ukanda wa
Afrika Mashariki na kati, kutokana na wakaazi wake kuwa ni wakarimu na wapenda
watu.
Wageni
wangi walivutika sana kufikia Kisiwani Pemba, ili kujionea ukarimu wa watu wake
uliojaa neema na uaminifu hali iliopelekea kisiwa hicho kujipatia majina
kadhaa.
Wengine
hukitaja kisiwa cha Pemba kama cha marashi ya karafuu, jazzira, makka ndogo
majina yote hayo pamoja na mengine yalikinyanyua juu kisiwa hicho.
Leo
tukiwa ndani ya miaka 25 tokea wagonjwa wa mwanzo kutambulika kuwa na VVU
kwenye hospitali ya Mnazi mmoja Unguja, mwaka 1886, na hatimae kisiwa cha
Pemba.
Yote
kwa yote, inaingia akili kwamba eti kuja kwa VVU ndio iwe sababu wa wakaazi wa
Kisiwa hicho, waachane na mila na desturi zao nzuri wa ukarimu na ubianaadamu
na kufikia pahala kuwa wakuu wa unyanyapaa?
Mbona
zipo tafiti zilizofanya na Tume ya Ukimwi Zanzibar, zimekuwa zikionyesha kuwa
kisiwa hicho miaka 1990, wakaazi wake walikuwa wanaongoza kwa kuwanyanyapaa
watu wanaoishi na VVU.
Wengine
waliona hilo ni ahuweni, maana unyanyapaa huo ulikuwa kwa watu wenye umri
mkubwa na wakati mwengine anaenyanyapaa anaweza kujitetea.
Sasa
hili lililopo ni zaidi ya unyama maana wananchi hawa wa kisiwa cha Pemba,
wamekuwa midomoni mwa watu wanaoishi na VUU na Ukimwi kwamba sasa unyanyapaa
umehamia kwa watoto.
Wapo
wazazi na walezi ambao wanaishi na VVU na Ukimwi kisiwani Pemba, wamekuwa
wakilalamikia hilo kwamba, sasa jamii ya kisiwani humo imewaacha wao na wa
kuwafanyia unyama watoto wao.
“Unyanyapaa
anaofanyiwa mwanangu ni jirani zetu na hata wapiti njia hupewa majina mabaya
kama vile, msambaazaji umeme, mwenye wali wetu, na hata kumuita muuwaji’’,sasa
hii ndio hali ya Pemba alisema Mzazi.
Mzazi
huyo ambae alisema alikaa na kuishi na VVU kwa miaka minne bila ya
kujitangaaza, alihofia sana unyanyapaa ndani ya jamii ya kijiji cha Wawi
anapoishi, ingawa baadae aliamua.
“Mimi
nilijitangaaza mara baada ya kufariki mumewangu mwaka 2011, lakini adha na
kebehi ya wapemba ilinifika, maana nilisusiwa kila kitu’’,alinikumbusha.
Moza
Haji Kombo (49) wa Chake Chake, yeye anasema hakukaa muda mrefu alijitangaaza,
ingawa unyanyapaa hasa ulimkumba mwanawe hadi sasa.
Mwanangu
hana hamu ya kutoka nje, maana hapa mtaani anacheza na watoto hawazidi wanne,
waliobakia anasema anawaogopa, maana wamekuwa wakimuita majina mabaya.
Mama
huyu anasikitishwa sana na majirani zake, amabo ni wenye umri mkubwa, kwa
kubuni majina mabaya na kumuita mwanawe ambapo anasema hilo humkosesha furaha
na amani kucheza.
“Watu
wazima ambao kukicha wanaingia masikitini na kanisa, wanamuita mwanagu mwenye
sumu, anaesubiri kufa, sio mwenzetu au hata kumuita mtu wa Tume’’,alisema kwa
kusikitika.
Kaimu
Mratibu wa Tume wa Ukimwi Zanzibar ZAC kisiwani Pemba, Ali Mbaroku Omar, yeye
anasema linalofanyika nchi nzima la kuwanyanyapaa watoto ni zaidi ya unyama.
Yeye
anashangaa kuona watu wenye akili zao timamu, kubuni majina ya mabaya na
kuwaita watoto ambao pengine wazazi wao walishakufa kwa Ukimwi au wenyewe
wanaishi na VVU.
“Mwenye
Ukimwi au Virusi ameshajielewa na ndio maana akapewa majina mabaya, sasa huyu
anaemnyanyapaa mwenzake anaahadi gani na Muumba, kwamba atakua salaama
daiama’’, alihoji.
Na
ndio maana Kaimu Mratibu huyo, anasema wamekuwa wakipokea malalamiko hayo kila
muda, kwa watoto kunyanyapaliwa kwa kupewa majina ya kishenzi.
Lakini
akasema kila mmoja akilia anashika kichwa chwake, na ndio maana yeye anaona
unyanyapaa mkubw ani ule wa kukoseshwa haki zao za msingi.
Makame
Juma Hamad wa kijiji cha Msuka wilaya ya Micheweni Pemba, yeye anasema kama
sheria ya masuala ya Ukimwi haijaanza kazi vyema, basi kila mtu atakua na
nafasi pana ya kuwafanyia unyanyapaa watoto.
“Imekua
ni jambo la lazima kwa watoto hata wanaoishi tu nyumba ya mtu mwenye VVU, basi
unyanyapaa pia humfika na mtoto ambae hajui lolote”,alifafanua.
Ama
kweli mtoto wa mwenzio sasa sio wako, yawaje jirani ambae alitajwa na maandiko
matakatifu kuwa ndio ndugu, lakini aanze kwa ubaya.
Maryam
Said Abdalla, ambae ameolewa na mwanamme asie na Virusi, anasema hata huyo
mtoto wao amekuwa akiipata pata kwa majirani.
Anakiri
kuwa hali ya nyanyapaa kwao wenye umri mkubwa sasa
umepungua, lakikini
mashambulizi yamelekezwa kwa watoto wao kwa nguvu.
‘Mimi
sasa sinyanyapaliwi tena, maana wameshaniona kama nimekomaa, lakini adhabu wa
watoto wetu, ndio kwenye kazi huko’’,alifafanua.
Aliyataja
majina ambayo husikia watoto wenye VUU au wazazi wao waliokufa kwa tatizo hilo
kama vile, majeneza, mava, wauwaji jambo ambalo huwasononesha sana.
Mtoto
(11) ambae pia anaishi na VVU kwa muda huo, mkaazi wa Mtambile wilaya ya
Mkoani, ingawa hajapenda kujitangaaza rasmi, anasema aliishi na tatizo kwa muda
wa miaka saba bila ya yeye kuelezwa.
“Sasa
niko shuleni na nimeleewa kwamba nna tatizo hilo mwaka 2012, ingawa
nilishituka, lakini nilikuwa nanyanyapaliwa ikawa sijui nini tatizo’’,alisema.
Yeye
anasema na hata baada ya wazazi wake kumuleza, na kuwaeleza marafiki zake, wapo
walioachana na yeye hadi leo, na wengine hata kumuita jeneza kutokana na kuwa
VVU.
Sheikh
Said Ahmad wa Chake Chake, yeye anasema suala la istizai ‘unyanyapaa’
halikubaliki maana humpa mzingira magumu mwenye uongojwa wa aina yoyote.
Yeye
anasema muislamu wa kweli aliepata mafunzo ya dini na kuyafuata kwa vitendo,
haweza kuwafanyia unyanyapaa watoto na hasa kwa kuwabandika majina mabaya.
“Uislamu
haukatazi mtu kuwa na jina la umaarufu, lakini liwe zuri mfano ‘amini’ hafidhi
na sio kumuita mtu sumu, au kaburi haya ni makosa’’,alisema.
Yohona
Kalagwa ambae ni mchungaji katika kanisa la usharika lililopo Chake Chake,
anasema hakuna mtu alieruhisiwa kumuita mwenzake jina analokasirika nalo.
“Mimi
sijaona katika bibilia kwamba, eti mtoto aitwe jina tu lolote, basi lazima
apewe jina lenye maana na tija na sio la kupotosha au kubeza’’,alisema.
Mratibu
wa Jumuia ya watu wanaoishi na VVU Pemba ZAPHA+ Mmanga Seif Massoud, anasema
idadi ya watoto 62 walionao kwenye jumuia kwa Pemba ni ndogo na shaka yake ni
unyanyapaa.
“Ingawa
juhudi tumeshazifanya sisi kwa kushirikiana na Tume ya Ukimwi, lakini wapo
wachache hawataki kubadili tabia na huwanyanyapaa watoto’’,alifafanua.
Mmanga,
yeye anaona sasa suala la watoto wenye VVU kupewa majina ya ajabu limepungua,
maana kabla ya kutoa elimu walikuwa wanapokea kesi moja kila mwezi, lakini sasa
ni miezi mitatu hawajapokea.
Aliyataja
majina ambayo huitwa watoto hao kama vile’maukimwi, wasambaazaji, wenye sumu,
lakini akasema kwa sasa hali inaridhisa kidogo.
Kwa
upande wa Zanzibar tayari ipo sheria ya masuala la Ukimwi na ikikataza suala la
kumnyanyapaa mtu kwenye Ukiwmi au Virusi kwa njia yoyote, ile na wakati wowote
itaanza kufanya kazi.
Ingawa
kwa Tanzania bara yenyewe ipo, na ndio maana kifungu cha 32 cha Sheria ya
Kudhibiti Ukimwi namba 28/2008 kupiga marufuku unyanyapaa, watu wanaoishi na
Virusi vya Ukimwi (VVU).
Kutokana na hali hiyo, jamii ya wenye VVU imedai imekuwa ikilazimika
kukubaliana na unyanyapaa unaofanywa na baadhi ya watu, ili kulinda CD4
zisipunguwe mwilini.
Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Waviu Washauri kutoka wilaya sita za Mkoa
wa Simiyu, waliotembelea Kituo cha Matunzo na Tiba (CTC) cha Hospitali ya Rufaa
ya Bugando iliyopo jijini Mwanza.
Shija
Mashimba, Mviu Mshauri wa hospitali hiyo, anadai kuwa tatizo la unyanyapaa kwa
watu wenye VVU ni kubwa, na njia pekee ya kukomesha hali hiyo ni kukubaliana na
matakwa ya jamii ili kutunza kinga za mwili (CD4).
Happiness
Malamala, mkazi wa Bariadi mjini ambaye anaishi na VVU na Mviu Mshauri, alidai
Halmashauri ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu inavyo vituo vitatu vinavyotoa
huduma ya tiba na matunzo kwa wenye VVU, ambako hadi kufikia Julai 2014 idadi
ya wateja waliopotea walikuwa 875.
Anafafanua
kuwa kati ya hao 769 walikwishaanzishiwa dawa za ARV huku 106 wakiwa
hawajaanzishiwa dawa hizo, ambapo katika kipindi cha Julai 2014 hadi Machi 2015
idadi ya wateja waliofuatiliwa ni 319 ambapo kati yao 272 wanatumia dawa za ARV
huku 47 wakiwa hawajaanza kutumia dawa hizo.
Mtandao wa Kanda ya Afrika Mashariki ya Mashirika yanayotoa Huduma za Ukimwi,
umekiri kuwa kundi kubwa la watoto
wanakabiliwa na unyanyapaa na ubaguzi na hakuna sheria wala sera za kuwalinda
katika kanda.
Mtando huo ulisema kuna ripoti za
walimu wakuu wanaokataa wanafunzi ambao wana VVU huku wakikabiliwa na
unyanyapaa, na kukataa shule.
Nchi za EAC zimetia saini mikataba kadhaa ya kimataifa kuhusu ubaguzi wa
VVU/UKIMWI ikiwa ni pamoja na Azimio la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na
Mkataba wa Haki za Watoto, katika ngazi ya kanda, nchi pia zina vifungu kuhusu
haki za watoto.
Hata hivyo, mapengo ya haki za binadamu kuhusiana na watoto na VVU bado yapo,
ikiwa ni pamoja na haki ya kulindwa kutokana na ubaguzi.
Suala la unyanyapaa limekuwa likitajwa na wanaharakati wa masuala ya
kupambana na Ukimwi, kwamba yanaweza kuwa kizingiti cha kupunguza maambukizi
mapya ya VUU.
No comments:
Post a Comment