Habari za Punde

Siku ya msaada wa kisheria ilivyoadhimishwa kisiwani Pemba

 AFISA Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba Hassan Ali, akizungumza mbele ya waalimu wa somo la uraia kisiwani humo, kwenye mkutano wa kukusanya maoni juu ya kuliimarisha somo hilo, mkutano uliofanyika Kituoni hapo mjini Chake chake, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 AFISA Mdhamini wizara ya Elimu Pemba Kitwana Salim Sururu akifungua mkutano wa siku moja, wa kutoa ushauri wa kuliimarisha somo la uraia, mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, kulia ni Mkaguzi wa elimu Amour Rashid na kushoto ni Afisa Mipango wa ZLSC Mohamed Hassan Ali, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WAALIMU wa somo la uraia Kisiwani Pemba, wakifanya kazi za makundi, kutoa changamoto na njia za ufumbuzi ili kuliimarisha somo hilo, kwenye mkutano uliofanyika Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba mjini Chakechake, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 BAADHI ya watendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba na wanasheria wengine, wakielekea kisiwa cha Fundo wilaya ya Wete, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya msaada wa kisheria duniani, kwa kuwapa msaada wa kisheria wananchi wa shehia hiyo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).


 : WATENDAJI wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, wanasheria wa serikali na waandishi wa habari wakiwa kwenye fukwe ya kisiwa cha Fundo wilaya ya Wete, kwenda kuwapa wananchi msaada wa kisheria bila ya malipo, ikiwa ni maadhimisha ya siku ya msaada wa kisheria duniani, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MAOFISA wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, wakitoa msaada wa kisheria kwa wananchi wa shehia ya Fundo wilaya ya Wete, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya msaada wa kisheria duniani, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 MWANDISHI wa habari kituo cha radio cha ZENJ FM Pemba Berema Suleiman Nassor, akizungumza na mwananchi wa shehia ya Fundo wilaya ya Wete, Omar Khamis Hamad (70) mara baada ya kupewa msaada wa kisheria, uliotolewa na wanasheria walioungana na Kituo cha Huduma za Sheria Pemba, kwenye maadhimisho ya siku ya msaada wa kisheria, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WATENDAJI wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC pamoja na wanasheria wakirudi kisiwa cha Fundo wilaya ya Wete, kwenye maadhimisho ya siku ya msaada wa kisheria, ambapo wananchi kadhaa walipewa msaada huo bila ya malipo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MWANDISHI wa habari kituo cha radio cha ZENJ FM Pemba Berema Suleiman Nassor, akizungumza na Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba Fatma Khamis Hemed mara baada ya kuadhimisha siku ya msaada wa kisheria, maadhimisho hayo yalifanyika Kisiwa cha Fundo wilaya ya Wete Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.