Habari za Punde

TRA Zanzibar yawakumbusha wafanyabiashara kulipa kodi


TANGAZO KWA WAFANYABIASHARA WOTE

 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwatangazia wafanyabiashara wote kuwa:-

 1. Kwa wafanyabiashara ambao wanadaiwa kodi mbalimbali wanakumbushwa kulipa haraka kwani kukaa na fedha ya serikali ni kukosesha maendeleo ya Taifa letu na ni kitendo cha aibu. Tunawapongeza walipakodi wote ambao wanalipa kodi kwa wakati.

 2. Ni wajibu wa kila mfanyabishara kutoa risiti kwa mauzo yote unayoyafanya. Pia wateja wote mnawajibu wa kudai risiti kwa manunuzi yote mnayoyafanya ili kuchangia katika mapato ya serikali

 3. Wafanyabiasha ambao wanafanya biashara bila ya kuwa na Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN)) wafike katika ofisi za TRA ili wapatiwe TIN. Kumbuka utaratibu wa kupatiwa TIN umeboreshwa na hutolewa BURE. 

4. Kwa wale wenye magari ya biashara (biashara za usafirishaji) wanasisitizwa kuja kulipia kodi yao ya mapato (TRA) kwa mwaka 2016 kabla ya mwezi wa Machi 2016 kumalizika. 

5. Mwisho, Maofisa wa TRA watapita sehemu za biashara kwa lengo la kuelimisha na kufuatilia wale wote wanakiuka sheria na taratibu za kodi. 

Hivyo TRA inaomba ushiriano wenu ili kufanikisha zoezi hili. “Pamoja Tunajenga Taifa Letu” 

Imetolewa na, Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.