Na Mwandishi Wetu.
Kampuni ya simu ya Zantel leo imetoa shilingi milioni 10 kwa Maktaba
Kuu ya Zanzibar kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa vitabu na kusaidia maktaba
katika uendeshaji wa shughuli zake pamoja na kurahisisha upatikanaji wa maarifa
mtandaoni kwa wakazi wa Zanzibar.
Akizungumza wakati wa
hafla ya makabidhiano hayo,Afsa
Mtendaji Mkuu wa Zantel, Benoit Janin
alisema msaada huo kwa maktaba ya
Zanzibar unalenga katika kusadia kurahisisha upatikanaji wa maarifa miongoni
mwa jamii ya Wazanzibar.
‘Maktaba ni njia
pekee na rahisi ya kusaidia upatikanaji wa maarifa miongoni mwa wanajamii bila
kujali tofauti zao za kiuchumi’ alisema Benoit.
Maktaba ya Zanzibar, kama sehemu ya majukumu yake, inayo wajibu wa
kuhakikisha inatoa huduma bora na zenye ufanisi zinazokidhi mahitaji ya wakazi
wanaoishi mijini na vijijini katika kuhakikisha upatikanaji wa taarifa za elimu,
habari, utamaduni na burudani.
‘Upatikanaji wa maarifa kwa wanajamii ni jambo la muhimu na
suluhisho la changamoto hii ni kuhakikisha tunatoa fursa sawa kwa kuwezesha
upatikanaji wa maarifa katika maktaba za jamii’ alisema Benoit.
Kwa upande mwingine, Benoit
alibainisha kuwa kama kampuni ya simu inayoongoza Zanzibar, Zantel
inaona fahari kushiriki katika kuchangia ukuaji na ustawi wa jamii.
‘Tunamini kwamba kujifunza ni muhimu kwa maendeleo
na ndio sababu kampuni ya Zantel inashiriki katika kusaidia
kukuza maendeleo ya elimu kama moja ya maeneo ya shughuli zake za kusaidia jamii’ alisema Benoit.
Naye mgeni rasmi wakati wa
makabidhiano hayo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Ufundi, Mheshimiwa Abdalla
Mzee, aliipongeza kampuni ya Zantel kwa mchango wao katika kukuza maendeleo ya
elimu Zanzibar.
‘Tunatoa pongezi na shukurani za dhati kwa kampuni ya simu ya
Zantel kwa ajili ya mchango wao katika kukuza maendeleo ya elimu ya Zanzibar,
na msaada huu uliotolewa leo kwa maktaba ya Zanzibar utasaidia katika
kurahisisha upatakanaji wa vitabu na hivyo kuimarisha mazingira ya utoaji
maarifa miongoni mwa wazanzibar’ alisema Mzee.
Mheshimiwa Mzee pia amesema msaada uliotolewa na Zantel utasaidia
katika uboreshaji wa maktaba katika
Visiwa vya Zanzibar hasa ununuzi wa
vitabu pamoja na utafutaji wa maarifa kutoka mtandaoni.
‘Kazi kubwa ya maktaba Zanizibar ni kuhakikisha inatoa huduma kwa
lengo la kuongeza ujuzi na maarifa miongoni mwa wazanzibar, na hivyo basi
msaada huu kutoka Zantel utaleta msukumo wa utekelezaji wa azma yetu hiyo' alimaliza
Mheshimiwa Mzee.
No comments:
Post a Comment