Habari za Punde

Spika Maulid Awaweka Mguu Sawa Wajumbe. Aunda Kamati 7 za Kisekta


·       Zachagua Wenyeviti  na wasaidizo wao
·       Machano, Dkt Mwinyihaji Kuongoza Kamati

Na, Himid Choko, BLW.

SPIKA  wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zubeir Ali Maulid ameunda Kamati saba (7) za Kudumu za kisekta za Baraza la wawakilishi , ili kuhakikisha kwamba  Baraza hilo linatekeleza kwa ufanisi  mkubwa zaidi Kazi ya kuisimiamia serikali.

Katibu wa Baraza la Wawakilishi Dkt Yahaya Khamis Hamad amesema Spika Maulid ameunda Kamati hizo kwa mujibu wa  Kanuni ya 107 (1) (a) ya Baraza la Wawakilishi Toleo la 2012.

Amesema kwa mujibu wa Kanuni hiyo  mjumbe yeyote wa Baraza asiyekuwa Makamu wa Pili wa Rais, Waziri, Naibu Waziri au Mwanasheria Mkuu anaweza kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumu yeyote inayohusika na Kanuni za Baraza.

Dkt Yahya  amezitaja  Kamati hizo kua  ni ile ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa, ambayo itahusika na Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais. Wajumbe wa Kamati hii wamemchagua Omar Seif Abeid ( Konde) kuwa Mwenyekiti na  Panya Ali Abdullah (Viti Maalum) kuwa Makamo Mwenyekiti.

Wajumbe wengine wa Kamati hii ni  Amina Idd Mabrouk (Viti Maalum), Mtumwa Suleiman Makame (Viti Maalum) , Simai Mohammed Said (Tunguu) , Mohammed Said Dimwa (Mpendae),  Hussein Ibrahim Makungu (Mtoni) na  Mussa Ali Mussa (Ole) . Awali katika Baraza lililopita Kamati hii ilikua ikiongozwa na Hamza Hassan Juma akiwakilisha Jimbo la Kwamtipura.

Kamati nyengine ni ya Sheria na Utawala, ambayo inahusika na  Ofisi ya Rais, Katiba, Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Wizara ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ambapo wajumbe wa Kamati hiyo wamemchagua aliyewahi kuwa Waziri na Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi katika awamu zilizopita    Machano Othman Said (Mfenesini) kuwa Mwenyekiti wake na  Mwantatu Mbarak Khamis (Viti Maalum),  kuwa Makamo Mwenyekiti.

Wajumbe wengine wa Kamati ya Katiba Sheria na Utawala ni pamoja na Saada Ramadhan Mwenda ( Viti Maalum), Wanu Hafidh Ameir (viti Maalum), Mihayo Juma N,hunga (Mwera), Shamata Shaame Khamis ( Micheweni), Nadir Abdullatif Yussuf (Chaani) na Ali Khamis Bakari(Tumbe).

Dkt. Yahya  amesema aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa katika Awamu iliyopita , Hamza Hassan Juma (Shauri Moyo) ameendelea kutumikia wadhifa huo katika   Kamati ya Mawasiliano na Ujenzi   ambayo itahusika na Wizara ya Ardhi , Maji, Nishati na Mazingira pamoja na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji .


Amesema Kamati hiyo ya Mawasiliano na ujenzi pia imemchagua Suleiman Sarhan Said (Chakechake) kuwa Makamo mwenyekiti wake . Wajumbe wengine wanaounda Kamati hiyo ni pamoja na  Mohammedraza Hassanali Mohammedali (Uzini), Abdullah Ali Kombo (Mwanakwerekwe), Mwanaidi Kassim Mussa (viti maalum), Khadija Omar Kibano (Mtambwe), Bahati Khamis Kombo (Chambani), Nassor Salim  Ali (Kikwajuni), na  Said Omar Said (Wingwi),

Kamati nyengine ni Kamati ya Maendeleo ya wanawake na Ustawi wa Jamii  ambayo imemchagua aliyekuwa Waziri katika Awamu zilizopita Dr. Mwinyihaji Makame (Dimani)  kuwa  Mwenyekiti na Tatu Mohammed Ussi  kuwa Makamo Mwenyekiti wa kamati hiyo.

Wajumbe wengine wa Kamati hii  ambayo itahusika na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali pamoja na Wizara ya Afya ni Viwe Khamis Abdullah( Viti Maalum), Hidaya Ali Makame ( Viti Maalum), Mwanaasha Khamis Juma ( Chukwani) , Masoud Abrahman Masoud ( Bububu) , Ame Haji Ali ( Nungwi) na Makame Said Juma  (Kojani).

Kwa upande wa Kamati ya  Kuchunguza na Kudhibiti Hesabu za Serikali na Mashirika (PAC) inaongozwa na Miraji Khamis Mussa (Chunbuni)  na Makamo Mwenyikiti wake ni Shaib Said Shaib (Chonga) , Wajumbe wengine ni  Mtumwa Peya Yussf (Bumbwini), Zainab Abdullah Salum (Viti Maalum), Dr. Makame Ali Ussi( Mto pepo),  Abdullah Maulid Diwani Jang”ombe), Zulfa Mmaka Omar (Viti Maalum).

Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayohusika na Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya biashara, Viwanda na Masoko pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi inaongozwa na  Yussuf Hassan Idd ( Fuoni ) na Makamo mwenyekiti wake ni Hamida Abdullah Issa ( Viti Maalum). Wajumbe wengine wa Kamati hii ni Ussi Yahya  Haji (Mkwajuni), Bihindi Khamis Hamad (Viti Maalum), Shadya Mohammed Suleiman ( Viti Maalum) , Ali Salum Haji (Kwahani), Hamad Abdullah Rashi(Wawi), na Mohammed Mgaza Jecha( Mtambile).

Dkt Yahaya ameitaja Kamati ya mwisho kuwa ni ile ya Mifugo, Utalii, Uwezeshaji na Habari  itakayohusika na Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo pamoja na Wizara ya Kazi, Uwezeshaji , Wazee , Vijana , Wanawake na Watoto. Amesema kamati hiyo itaongozwa na Ali Suleiman Ali( Kijitoupele) na Makamo Mwenyekiti wake ni Salha Mohammed Mwinjuma (Viti Maalum).

Wajumbe wengine ni  Zainab Abdullah Salum ( Viti Maalum), Asha Abdullah Mussa (Kiwengwa), Jaku Hashim Ayoub( Paje), Suleiman Makame Ali (Ziwani), Mussa Foum Mussa( Kiwani), Hassan Khamis Hafidh ( Welezo) na Maryam  Thani Juma (Gando).


Mwisho

Imetolewa na Divisheni ya Itifaki na  Uhusiano, BLW
O777436016.

Sunday, 17 April 2016

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.