Habari za Punde

Tamasha la Halotel ‘Back to University’ lakonga Nyoyo za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu


Wanafunzi wakichuana katika mchezo wa netball wakati wa bonanza la Halotel lililofanyika katika viwanja vya Mabibo Hostel


Wanafunzi wa Chuo kikuu Dar es Salaam wakipambana na wanafunzi wa chuo cha ualimu (DUCE) wakati wa bonanza la Halotel lililofanyika Mabibo Hostel.


Msanii Msami akitoa burudani wakati wa tamasha la Halotel lililofanyika Mabibo.


Mkurugenzi wa Halotel tawi la Dar, Bwana Alex Thiem akizungumza na wanafunzi wakati wa Bonanza la Halotel lilifanyika viwanja vya Mabibo Hostel

Msanii Ruby akiburudisha wakati wa tamasha la Halotel lililofanyika Mabibo Hostel.

Stamina akiburudisha wanafunzi wakati wa tamasha la Halotel lililofanyika Mabibo Hostel.

Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria tamasha la Halotel katika viwanja vya Mabibo Hostel.

Na Mwandishi Wetu.
Kampuni ya simu Halotel juzi ilizikonga nyoyo za wanafunzi wa vyuo vikuu kupitia tamasha lake la ‘Back to University’ lililofanyika katika Viwanja vya Hostel ya Mabibo jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na maelfu ya wanafunzi.

Tamasha hilo lilipambwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya, Msami, Ruby na Stamina pia lilitawaliwa na michezo ya aina mbalimbali kama vile Netiboli, soka na mingineo.

Akizungumzia kuhusiana na tamasha hilo Mkurugenzi wa Halotel tawi la Dar es Salaam, Bwana Alex Thiem alisema tamasha hilo lina lengo la kuimarisha uhusiano baina ya Halotel na wanafunzi wa vyuo vikuu.

‘Toka mtandao wetu umeanza hapa nchini tumejikita katika kuhakikisha tunaboresha huduma za simu nchini, lakini kwa upekee kabisa tumekuwa tunawapa wanafunzi huduma bora na nafuu zaidi’ alisema bwana Thiem

Kwa upande wa burudani Msami alipopanda jukwaani alitumia takribani dakika 45 kuzikonga nyoyo za mashabiki wake hao ambapo aliimba nao na kucheza pia hasa akionesha umahiri wake wa kucheza dansi.

Naye msanii Ruby anayetamba na kibao chake kipya cha Forever, alitoa burudani kali kwa maelfu ya wanafunzi waliojitokeza katika hosteli hizo.

Ilipofika majira ya saa 12 jioni akapanda jukwaani msanii Stamina ambae ameandika historia ya kipekee kwa wanafunzi hasa kwa aina yake ya uimbaji wa mashairi yaliyokuwa yakishangiliwa mara kwa mara.

Tamasha hilo lilianza majira ya saa nne asubuhi kwa michezo ya aina mbalimbali kama vile Netiboli pamoja na soka ambapo katika mchezo wa Netiboli timu ya wanafunzi wanaume iliibuka na ushindi wa mabao 11 - 10 dhidi ya timu ya wanawake.

Kwa upande wa mchezo wa soka zilicheza timu mbili ambapo ilianza timu ya Baraza la Mawaziri la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam iliyoibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya timu ya Idara ya Mazoezi ya Viungo.

Katika mechi nyingine, timu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ikaifunga timu ya Chuo Kikuu cha Ualimu (DUCE) 1-0.

Michezo hiyo kwa ujumla ilizokonga nyoyo za wanafunzi wengi ambapo pia walipata wasaa wa kujiunga na huduma za mtandao huo wa simu kama vile kununua laini, kujiunga vifurushi na mengineo.

Kwa upande wake waziri wa michezo wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, bwana Jackson Mayunga aliishukuru kampuni ya Halotel kwa kufanikisha tamasha hilo.


‘Tunawashukuru sana Halotel kwa kufanikisha tamasha hili, na kama unavyoona wanafunzi wamepata nafasi ya kuburudika lakini pia kubadilishana mawazo’ alisema Mayunga.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.