Habari za Punde

Vurugu mechi ya magari ya Abiria Chakechake baada ya Madereva kudai kutii agizo la serikali

 GARI za abiria zikiwa zimesongamano katikati ya mji wa Chakechake, baada ya wamiliki wa gari hizo kudai, kutekeleza agizo la serikali ya mkoa wa kusini Pemba, la kuzitaka gari hizo, zishushe na kupakia abiria kwenye egesho kuu ‘stand’ badala ya kutumia zile za zamani zilizopo pembezoni mwa mji huo (Picha na Habiba Zarali, Pemba).
 MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe: Mwanajuma Majid Abdalla na kushotoni kwake Katibu tawala wa mkoa huo, Ahmed Khalid na Kamanda wa Polisi wa mkoani humo Shehan Mohamed Shehan wakienda kwenye egesho kuu la gari za abiria, ili kutoa ufafanuzi baada ya kutokezea vurumai kwa gari za abiria kuweka msururu mrefu ndani ya mji wa Chakechake, (Picha na Habiba Zarali, Pemba).
MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe: Mwanajuma Majid Abdalla, akizungumza na vyombo vya habari, mara baada ya madereva kudai kutii agizo la serikali ya mkoa, kuziingiza gari zote kwenye egesho kuu jambo lilizoua vurumai jana majira ya asubuhi, (Picha na Habiba Zazrali, Pemba).  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.