Habari za Punde

Wizara ya Afya Zanzibar yaadhimisha siku ya afya Duniani kwa kutoa elimu ya maradhi yasiyoambukiza kwa skuli mbali mbali

Mkuu wa Kitengo cha maradhi yasiyoambukiza (NCD) Omar Mwalimu Omar akitoa elimu  kwa wanafunzi wa Skuli ya Sekondari ya Kiembesamaki juu ya njia bora za kujikinga na  maradhi yasiyoambukiza ikiwa ni maadhimisho ya siku ya afya Duniani. 

 Muuguzi kutoka kliniki  ya wagonjwa wa kisukari Hospitali ya Mnazimmoja Bi. Mwanaharusi Shaaban akitoa elimu ya ugonjwa wa kisukari kwa wanafunzi wa Skuli ya Mwanakwerekwe C katika sherehe za kuadhimisha siku ya Afya Duniani zinazoadhimishwa kila ifikapo tarehe 7 April.  Zanzibar imeadhimisha siku hiyo April 13 kwa kutoa elimu skuli za serikali na binafsi.

 Baadhi ya wanafunzi wa Skuli ya Mwanakwerekwe C wakimskiliza kwa makini mtoa elimu ya maradhi yasiyo ambukiza Bi. Mwanaharusi Shaaban (hayupo pichani) wakati wa sherehe za siku ya Afya Duniani zinazoadhimishwa kila ikifika tarehe 7 kila mwaka.

 Mwanafunzi Shadia Issa Juma akiuliza swali kwa Muuguzi kitengo cha wagonjwa wa kisukari Bi. Mwanaharusi Shaaban.

 Mkufunzi kutoka kitengo cha maradhi yasiyoambukiza (NCD) cha Wizara ya Afya Rabia Ali Makame akifundisha wanafunzi wa Skuli ya SOS kuhusiana na visababishi vinavyopelekea maradhi yasiyo ya kuambukiza katika sherehe za kuadhimisha siku ya Afya Duniani.

 Baadhi ya wanafunzi wa Skuli ya SOS wakimskiliza kwa makini Mkufunzi kutoka kitengo cha maradhi yasiyoambukiza (NCD) cha Wizara ya Afya Rabia Ali Makame (hayupo pichani) wakati wa sherehe za siku ya Afya Duniani zinazoadhimishwa kila ikifika tarehe 7 kila mwaka.

Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.