Habari za Punde

Bidhaa zilizomalizika muda wake zateketezwa kisiwani Pemba

 WAFANYAKAZI wa Wizara ya Biashara na Viwanda na Masoko Pemba, wakizichana pakiti 204 za sukari iliyopitiwa na muda wakati wa uteketezaji wa sukari hiyo huko katika mashimo ya makaani Vitongozi, sukari iliyokuwa ikimilikiwa na Mfaranya biashara maarufu chake chake Mohamed Ali Aboud,(Munauwari)(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 BAADHI ya wafanya biashara kisiwani Pemba, wamebuni ujanja wa kuzibadilisha tarehe za kuharibika bidhaa zao, kama zinavyoonekana katika picha Mfuko wa Super Special kahawa ikiwa imebadilishwa muda wake halisi wa mwisho wa matumizi.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 KATIBU tawala Wilaya ya Chake Chake Rashid Abdalla Rashid, akiwa ameshikilia baadhi ya soda soda zilizopitiwa na Muda, wakati wa kuvibagua biadhaa hizo kabla ya kuchomwa moto huko Makaani Vitongoji Wilaya ya Chake Chake. (Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 GARI aina ya Buldoza la Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Pemba, kikichanganya sukari iliyoharibika na mchanga, ili kuzuwia wananchi wasiweze kuichukuwa ikiwa imeshapitiwa na muda, kazi hiyo iliyofanyika huko Makaani Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 GARI aina ya Buldoza la Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Pemba, kikichanganya sukari iliyoharibika na mchanga, ili kuzuwia wananchi wasiweze kuichukuwa ikiwa imeshapitiwa na muda, kazi hiyo iliyofanyika huko Makaani Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 BAADHI ya wafanyakazi wa Wizara ya Biashara Viawanda na Masoko Kisiwani Pemba, wakiimimina karafuu mbovu ambayo imeshapitiwa na muda, wakati wa uteketezaji wa vyakula vibovu huko makaani Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Pemba. (Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
BAADHI ya bidhaa za majimaji kama vile Juisi, arki, marashi na bidhaa za vitafunio vikiwa vimeshapitiwa na muda wake wa matumizi vikisubiri kuteketezwa kwa moto huko Makaani Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Pemba. (Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

1 comment:

  1. Hakuna njia ya mbadala ya kuziteketeza hizo bidhaa.
    Uchomaji hauathiri avya ya binadmu kutokana kemikali zilizotengezea vifungio kama hiyo mifuko na kadhalika

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.