Na Zuhura Juma, PEMBA
“GEWE imetuwezesha kuibua matendo ya
udhalilishaji yaliyokuwa yamejificha katika jamii”
“Ama kweli! kikulacho, kinguoni mwako”, wahenga
hawakukosea walipoutoa msemo huu, kwani wakati wote huo tumekuwa tukiliwa na
matendo ya udhalilishaji bila kujijua wenyewe.
“Tulikuwa
kimyaa… mda wote huo kama tuliozindikwa, jinsi matendo ya udhalilishaji yalivyokuwa
yakitokea bila wenyewe kushughulika na kuliona ni jambo la kawaida"
…
hivyo ndivyo yalivyokuwa yakiwatoka maneno waratibu wa shehia, jinsi
walivyoweza kuyaibua matendo yaliyokuwa yakitendeka katika jamii…
Kwa
kweli ni jinamizi kubwa lililokuwa likiinamia jamii siku za nyuma, ingawa bado
lipo lakini limebakia ncha tu liweze kuondoka.
Na
hili linawezekana kuliondosha kabisa, kwani tumeweza kula samaki mzima… hivi
tushindwe na mkia?
“Mhuuu…
lililopo lipoo, maana tumejua mengi zaidi na zaidi katika jamii yaliyokuwa
yamefunikwa nyungu na baadhi ya wanajamii”, waliongeza kusema.
Kwa
kweli jamii ilidhalilika kwa watoto kubakwa, kulawitiwa na hata kutelekezwa na
wazazi wao.
Jambo
ambalo lilipelekea watoto wengi kukosa haki zao za msingi ikiwa ni pamoja na
kukosa elimu.
Vitendo
hivyo vilionekana kushamiri siku hadi siku katikia jamii, lakini mradi wa kukuza
usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake ‘GEWE’, uliweza kuvipunguza kwa kiasi
kikubwa.
Hii
ni katika jitihada yake ya kutoa elimu katika nyanja tofauti, ilimuradi yaweze
kupotea kabisa katika jamii.
Na
hili limefanikiwa ingawa havijaondoka vyote lakini vimepungua.
Mradi
huo ulitoa fursa ya kuibua maovu yaliyojificha, kutoa elimu kwa jamii ambapo
iliweza kuelimika, kuibua kesi za udhalilishaji.
Pia
kutatua kero ikiwa ni pamoja mabomba ya maji machafu ambayo yanaweza
kusababisha maradhi.
Tokea
kutolewa elimu kwa waratibu wa shehia zilizopitiwa na mradi huo, imesaidia sana
kuibua matatizo yaliyojificha katika siku za nyuma kwenye jamii.
Labda
niseme GEWE inahitaji pongezi kubwa kwa jitihada zake zilizotumika katika
kuvipiga vita vitendo vya udhalilishaji katika jamii.
Elimu
ya taarifa na maarifa ni miongoni mwa elimu waliyoipata waratibu hao, ambayo
walitakiwa kuweka kituo kitakachoweza kuleta mabadiliko zaidi.
Kituo
cha taarifa na maarifa ni kituo cha wanaharakati ngazi ya jamii ambayo
itasaidia jamii kupata uelewa na uchambuzi na kuona wanajenga nguvu za pamoja,
ili kuleta mabadiliko.
Kituo
hicho kinatakiwa kianze ngazi ya shehia, ili kuzikusanya kesi na kuzipeleka
katika kituo na kuweza kuzifuatilia kwa pamoja.
Kufanya
hivyo kutapelekea kujenga nguvu za pamoja katika kuzishughulikia kesi kwa
pamoja na kwa kina, ili kuweza kuzipatia ufumbuzi unaofaa.
Mafunzo
hayo, ymewafanya waratibu hao kuungana kwa pamoja na kushirikiana katika
kuyafichua matatizo yaliyojificha na kuweza kuyakusanya pamoja na kuyafuatilia.
Kituo
cha taarifa na maarifa kimesaidia kwa kiasi kikubwa katika kuyakusanya matukio
ya udhalilishaji yanayotokea katika kila
shehia.
Siti
Khatib Ali mratibu wa shehia ya Mchangamdogo akisifu kituo cha taarifa na
maarifa kimeweza kuwasaidia kujenga nguvu za pamoja katika kuleta mabadiliko.
“Kituo
kimetusaidia sana, kwani tumeweza kukutana na kubadilishana mawazo na kutafuta njia
ya ziada ya kuweza kuvitokomeza vitendo hivi”, alizidi kusifu.
Kama
wahenga walivyosema ‘Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu’, hivyo msemo huu
umewasaidia sana waratibu pale ambapo wameweka kituo kwa ajili ya kukutana na
kupanga mikakati yao.
Mratibu
wa shehia ya Mjiniole, Khadija Henoik Maziku anafahamisha tokea kuweka kituo
hicho wameweza kuzikusanya kesi katika kila shehia na kuzikusanya pamoja katika
kituo.
Jambo
ambalo limewarahisishia katika shughuli zao za ufuatiliaji, kwani wengi sio
mmoja hivyo hushirikiana katika kulitatua tatizo.
“Kituo
chetu cha taarifa na maarifa kimetujengea ushirikiano mkubwa na tumepata ule
mwamko wa kuzikusanya kesi katika shehia zetu na kuzifikisha katika kituo kwa
ajili ya kuzifuatilia”, alisema huku uso wake ukionesha furaha.
Ni
kesi 47 zilizoripotiwa katika kituo cha taarifa na maarifa, ambazo zimetoka
katika shehia zilizopitiwa na mradi wa GEWE.
Kesi
hizo zipo katika mchakato wa kuzifuatilia, ambapo hushirikiana kwa pamoja jambo
ambalo limekuwa ni faraja kwao kwa kuwepo kwa kituo hicho.
Salma
Abdallah Hamad mratibu kutoka shehia ya Shengejuu hakukaa kimya jinsi
alivyofaidika na elimu hiyo ya kuweka kituo cha maarifa na taarifa kwa kupiga
hatua kubwa ya kupambana na kesi za udhalilishaji.
“Tumeweza
kuzikusanya kesi kwa pamoja katika kituo chetu cha taarifa na maarifa, ambapo
kesi za utelekezwaji zimepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na nyuma”,
alieleza.
“Kwa
sasa kesi za utelekezwaji kwa wanawake na watoto zimeonesha sura nzuri, kwani
akina baba walio wengi wamekuwa karibu na familia zao.
Jamii
imebadilika kutoka hali moja kwenda nyengine, ambapo kesi zimepungua kwa kiasi
kikubwa.
Kupungua
kwa kesi hizo, ni faraja kubwa kwa waratibu hao, jambo ambalo ndio lengo kubwa
la mradi wa GEWE katika kuvitokomeza vitendo vya udhalilishaji.
Waratibu
hao pia waliweza kupatiwa elimu ya urakidishi, ambayo imewawezesha kupita
katika jamii na kujua changamoto zinazowakabili wananchi.
Walitakiwa
kusikiliza changamoto zinazowakabili wananchi ambazo ni huduma za jamii na
kuziwasilisha katika vyombo vya habari, ili kuweza kupata ufumbuzi.
Tokea
kuweka kituo hicho tayari wamefanya mambo mbali mbali kutokana na ushirikiano
mkubwa waliouonesha waratibu hao.
Mratibu
kutoka katika mradi wa GEWE Asha Abdi Makame, anaeleza waratibu hao walitakiwa
waanzishe kituo cha taarifa na maarifa ili wakusanye matukio yote ya Wilaya na
wapate kuzitoa katika vyombo vya habari.
“Muvitumie
vyombo vya habari, ili kuona matendo haya yanaondoka kabisa na sasa tunataka
tutanue wigo, tuzishirikishe na shehia nyengine na tayari tumepata mwakilishi
kutoka Mkoani”, alisema Mratibu.
Mratibu
aliwahamasisha kuyafanyiakazi mafunzo na kuweza kukidumisha kituo cha taarifa
na maarifa, kwani kinajenga ushirikiano mkubwa.
Na
walitakiwa elimu hizo kuwafikishia shehia nyengine ambazo hazikuingia katika
mradi, ili kuweza kuvitokomeza vitendo.
…..
Grace kutoka GEWE hakukaa kimya na kusema ili kuweza kuvitokomeza vitendo vya
ukatili wa kijinsia, hawana budi kuzidisha ushirikianobega katika kituo chao
cha taarifa na maarifa.
“Ili
vitendo hivi viweze kuondoka kabisa, munatakiwa mufuatilie kwa kina na
mufanyekazi kwa pamoja”, alishauru.
Afisa
Ustawi wa Jamii Wilaya ya Wete Pemba, alisema ili kuweza kupata taifa bora la
baadae hapana budi kushirikiana katika kuviondosha vitendo vya ukatili wa
kijinsia katika jamii.
“Mradi
wa GEWE umewezesha kuvipunguza vitendo vya udhalilishaji, hivyo tusichoke
kufuatilia kwa umakini na kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya vitendo hivi”,
alifahamisha.
Afisa
huyo aliwataka waratibu hao kukitunza na kukiimarisha kituo cha taarifa na
maarifa na kuwaarifu wao wakati wakiweka mikutano yao, ili kuweza kushirikiana
katika kuzitatua changamoto hizo.
Kuwepo
kwa kituo cha taarifa na maarifa ni muhimu kwa waratibu wa shehia, ambazo
zinaweza kujenga nguvu ya pamoja katika kukusanya matukio na kuyafuatilia.
Mradi
wa kukuza Usawa wa Kijinsia na Kuwawezesha Wanawake GEWE, uliweza kupiga vita
vitendo hivyo kwa kutoa elimu katika jamii, ulioanza mwaka 2012 hadi kumalizika
mwaka 2014, ambapo umeengezewa muda wa mwaka mmoja ulioanza Disemba 2015 hadi
Disemba mwaka huu.
No comments:
Post a Comment