Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Mama Mwanamwema Shein mke wa Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mheshimiwa
Waziri ya Afya
Mhe.
Naibu Waziri wa Afya
Mheshimiwa
Katibu mkuu Wizara ya Afya
Mhe.Naibu
Katibu Mkuu
Waheshimiwa
viongozi mbali mbali wa Wizara ya afya
Wageni waalikwa,
Ndugu Wauguzi wezangu,
Mabibi na Mabwana,
Itifaki imezingatiwa
Assalaam
Alaykum,
Awali ya yote hatuna budi kumshukuru
M/Mungu kwa kutujaalia kukutana leo hii tukiwa na furaha na afya njema.
Pia kwa niaba ya Wauguzi wenzangu,
napenda kuchukua fursa hii kukushukuru wewe Mgeni Rasmi kwa kuvunja majukumu
yako muhimu na kukubali ombi letu la kujumika na sisi katika hafla hii.
Mhe.
Mgeni Rasmi,
Madhumuni makubwa ya kukutana kwetu ni
kuadhimisha Siku ya Wauguzi Duniani, Siku ambayo amezaliwa muanzilishi wa
huduma za Uuguzi duniani Bibi Florence Nightingale
ambae alizaliwa kwenye mji wa Florence kule Italy 1820. Mama huyu raia ya Uingereza alileta
mageuzi makubwa kwenye kada ya Uuguzi, alitumia muda wake mwingi kuhudumia
wagonjwa kwa moyo wa huruma, upendo, imani na ushirikiani mkubwa sana.
Mheshimiwa Mgeni rasmi
Siku
hii huadhimishwa kwa kufanya shughuli mbali mbali ili kuimarisha afya ya jamii.
Wadau mbali mbali dunia nzima na wanachama wa Baraza la Kimataifa la Wauguzi
husherehekea siku hii kwa kufanya shughuli katika jamii kwa kipindi cha wiki
nzima. Maudhui
ya mwaka huu ni “MUUGUZI NI CHACHU YA
MABADILIKO: UIMARISHAJI WA UTHABITI WA MIFUMO WA AFYA”
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Katika
kuadhimisha siku hii hapa Zanzibar, Wauguzi wamefanya shughuli mbali mbali katika
jamii kwa kutoa huduma za uchunguzi macho, ugonjwa wa kisukari na sindikizo la
damu, kufanya usafi wa mazingira na utoaji wa zawadi katika kituo cha Wazee
Sebleni na kituo cha kulelea watoto yatima Mazizini.
Mheshimiwa Mgeni rasmi
Ili kuleta mabadiliko chanya katika afya ya jamii, Siku ya Wauguzi
duniani imeanzishwa kuongeza uelewa wa wajibu na majukumu ya Wauguzi pamoja na
kuona umuhimu wa kutimiza mahitaji ya Wauguzi duniani kote. Wauguzi duniani
kote wametoa mchango mkubwa katika kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto
wachanga, kupunguza malaria, kifua kikuu, polio, na kupunguza maambukizo mapya
ya VVU. Hivyo wauguzi wakitumiwa ipasavyo wana mchango mkubwa katika kuimarisha
afya ya jamii.
Mheshimiwa mgeni rasmi
Kuongezeka migogoro na wahamiaji duniani, kuongezeka kwa maradhi yasiyo
ya kuambukiza (saratani, kisukari, shindikizo la damu), kuongezeka kwa maradhi
ya mripuko (kipindupindu, ebola), maafa ya kimaumbile (mafuriko, kimbunga na vita),
ongezeko la watu duniani kunaweza kukapelekea kutofikiwa kwa maudhui ya siku ya
wauguzi duniani. Hivyo tunaomba Serekali kuimarisha mifumo thabiti ya afya ili
kukabiliana na changamoto hizi.
Mheshimiwa mgeni rasmi
Ili kupambana na changamoto nilizozitaja hapo juu, mambo yafuatayo
yanahitajika;
·
Kuwepo uwekezaji mkubwa kwenye sekta
ya afya
·
Kuwepo mfumo madhubuti ya taarifa za
maradhi na ufuatiliaji.
·
Kuwepo mfumo bora wa matayarisho na kukabiliana
na majanga mbali mbali
·
Kuwepo kwa miundombinu bora ya afya
·
Upatikanaji endelevu wa dawa na vifaa
tiba
·
Kuajiri watendaji kazi waliopatiwa
mafunzo katika fani uuguzi na ukunga
·
Uwepo vituo na hospitali
zilizowezeshwa kwa vifaa na madawa na kutoa huduma bora
·
Kuwepo bajeti ya kutosha katika
huduma za afya
Kuwatumia wauguzi katika kutoa huduma kutapelekea kufikiwa kwa malengo
ya afya ya ulimwengu (Universal Health Coverage)
Mheshimiwa Mgeni Rasmi
Tunatowa shukrani zetu za dhati kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja
na wadau mbali mbali wa Maendeleo kwa juhudi mbali mbali inazofanya katika
kuhakikisha kada ya Uuguzi inaimarika, hii ni pamoja na kupatiwa ufadhili kwa
Wauguzi kwenda kujiendeleza kielemu. Kuanzia mwaka 2012 hadi 2016, jumla wauguzi
198 wamepatiwa fursa ya kujiendeleza
katika mafunzo ya Uuguzi kwa kiwango cha stashahada, shahada, shahada ya
uzamili na shahada ya uzamivu, haya ni mafanikio makubwa katika fani ya Uuguzi.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi
Pamoja na jitihada zote za Serikali na wadau mbali mbali katika
kudumisha huduma za afya, fani ya Uuguzi inakabiliwa na changamoto zifuatavyo:
·
Uhaba wa Wauguzi bingwa wa maradhi ya
kinamama, maradhi ya watoto wachanga, huduma za dharura na ajali, mifumo ya
fahamu na ubongo hali inayopelekea usumbufu mkubwa katika utoaji huduma za kila
siku
·
Upungufu wa vifaa vya kujifunzia kwa
wanafunzi wauguzi wanapokuwa katika hospitali za kujifunzia
·
Kupunguwa kwa moyo wa kufanya kazi kwa
Wauguzi kulikosababishwa na upungufu wa vitendea kazi za Uuguzi
·
Kazi nyingi wanazofanya Wauguzi kulingana
na idadi ya wagonjwa wanaowahudumia ambapo hakuna wiano sawa na viwango vya
kimataifa vya utowaji wa huduma za kiuguzi, hii inapelekea huduma zinazotolewa zisiwe
na kiwango bora
·
Kukosekana kwa ufadhili kwa Wauguzi wanotaka
kujiendeleza ndani na nje ya nchi
·
Mazingira magumu ya kazi yanayochangiwa
na ukosefu wa posho mbali mbali na vifaa.
Mheshimiwa
Mgeni Rasmi,
Tunaomba utufikishie kilio chetu kwa wahusika ili
utekelezaji wake usiendelee kuchukuwa muda mrefu zaidi. Sisi wauguzi tunaahidi
kwamba tutatekeleza wajibu wetu kwa kufuata miongozo, sheria na kanuni zilizopo
ili kimarisha huduma kwa wagonjwa. Aidha
tunalaani vikali tabia za Wauguzi wachache wasiofuata maadili na miongozo ya
Uuguzi na kuharibu taswira ya Uuguzi kwa jamii.
Mwisho kabisa tunapenda
kukushukuru tena kwa kukubali kwako kuwa Mgeni Rasmi wa siku hii adhimu, kwa
kweli Wauguzi sote tumefarijika sana
kuwa nasi katika siku hii.
Aidha tunashukuru wadau mbali
mbali na wageni waalikwa waliojiunga na sisi na kufanikisha maadhimisho haya.
Ahsanteni.
No comments:
Post a Comment