Bw. Huziangyang Jacko, Meneja wa Huawei nchini Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
29 Aprili 2016 Dar es Salaam
Mkakati wa Huawei katika kubadili namna uonavyo dunia
iliyokuzunguka
Kampuni ya Huawei yaungana na Watengenezaji mashuhuri wa kamera
duniani; Leica kutengeneza simu P9
Mwezi Aprili,
Huawei wamezindua simu iliyokua ikisubiriwa kwa muda mrefu katika mlolongo wao
wa simu zao za P Series; Huawei P9. Uzinduzi wa Huawei P9 umezingatia
kipaumbele cha teknolojia ya hali ya juu. Toleo hili la tisa la P Series limewezeshwa
na Kampuni ya Huawei pamoja na kampuni mashuhuri kwa utengenezaji wa camera duniani
Leica. Simu hii ina kamera ya kipekee yenye lenzi mbili, ambayo imeweka rekodi
katika teknolojia ya kamera za simu za kisasa, ikiwa na mwanga Zaidi na ubora
Zaidi, kupata picha zenye rangi nzuri Zaidi katika staili ya Leica ya kipekee.
Watanzania
wanategemea kupata simu hii yenye teknolojia ya hali ya juu na ya kipekee
katika kamera hivi karibuni. Hii inafuatia uzinduzi wa simu hiyo uliofanyika
mji wa Dubai wiki hii. Uzinduzi huo wa kipekee ambao ulihudhuriwa na viongozi
wa Huawei Tanzania na Waandishi wa Habari umeashiria upatikanaji wa simu hii
katika soko la Tanzania hivi karibuni.
Tokea
uzinduzi wake mji wa London, simu hiyo imepata mapokezi makubwa kama simu
“inayobadili namna uonavyo dunia”. Simu mpya ya kipekee Huawei P9 ina malengo
kubadili ubora wa picha unaopatikana katika timu za kisasa maarufu kama “smartphone”.
Teknolojia katika simu hiyo inabadili namna tunavyopiga na kufurahia picha, hii
imetokana na shauku ya Huawei kuendelea kuvuka mipaka ya uvumbuzi, ikilinganishwa
na uzoefu na kipaji katika utengenezaji wa kamera na lenzi wa Leica pamoja na
ushirikiano mzuri katika kutengeneza P9.
Waliokuwepo
katika uzinduzi huo ni pamoja na viongozi wakuu wa Huawei Tanzania akiwemo
Bwana Huziangyang Jacko, Meneja wa Huawei nchini Tanzania, Lydia Wangari Meneja
Masoko kampuni ya Huawei Tanzania, waandishi wa Habari na wadau mbalimbali
kutoka Tanzania.
Akionglea ujio
wa simu hiyo katika soko la Tanzania Bwana Huziangyang Jacko, Meneja wa Huawei
nchini Tanzania alisema ”Tunategemea kuleta simu mpya ya Huawei P9 kwa wateja
wetu wa Tanzania hivi karibuni; Tunaamini teknolojia hii ya hali ya juu na ya
kipekee iliyotokana na utafiti wa hali ya juu na shauku ya kubadili namna watumiaji
wetu waonavyo dunia inayo wazunguka, P9 ikifanya kazi na Leica, tumeweza
kufanya maajabu katika teknolojia ya lenzi ya kamera”.
Akiongea katika
uzinduzi huo, Lydia Wangari Meneja Masoko Huawei Tanzania alisema, ”Tunaendelea
kuzindua simu mpya , tukitilia mkazo katika teknolojia ya kipekee. Kwa
kushirikiana na wadau wengine, tumeweza kujumuisha utamaduni, mtindo ya maisha
ya wateja wetu na teknolojia ili kuwapatia wateja watu simu bora zaidi”.
Kuongezeka
kwa aina mbalimbali za simu za mkononi za smartphone nchini Tanzania inaashiria
ukuaji na umuhimu wa Tanzania katika soko duniani huku wa Tanzania Zaidi
wakigundua umuhimu wa teknolojia maishani mwao. Mahitaji katika maendeleo na
simu za kiteknolojia yanaongezeka kila
kukicha nchini Tanzania na kampuni ya Huawei imeendelea kutatua hitaji hilo nchini
Tanzania.
Kufuatia
mafanikio ya simu aina ya P zijulikanalo kama “P Series”, kwa ujumla mapokezi ya
simu ya Huawei P9 ni mazuri duniani kote. Huawei Tanzania wana matarajio
makubwa juu ya ufanyaji kazi wake katika soko la Tanzania. Wakiahidi watumiaji
simu yenye nguvu na ubora wa kipekee usio linganishwa, simu mpya ya P9
itapatikana katika rangi nne: Dhahabu, kijivu, Dhahabu iliyoiva Zaidi na Siliva
huku P9 Deluxe Version ikipatikana katika rangi ya dhahabu na Nyeupe.
Familia ya
simu za Huawei P9 imetumia njia za
kipekee na ubora wa hali ya juu kubadili namna tunavyoona dunia iliyotuzunguka.
Inaendeleza heshima ya Huawei ya simu zenye ubora wa juu ambazo zimeacha alama
katika soko kwa ubora na ufanisi.
Huawei
itaendelea kukamata fursa mbalimbali ili kubadili soko na kuinuka duniani
katika biashara za watumiaji wa simu za mkononi. Huku simu za kampuni hiyo
zikizidi kua na teknolojia ya hali ya juu, Huawei itaendelea kutengeneza vifaa
vinavyoweza tumika na mteja wakati wowote na mahali popote. Na Wataendelea
kuungana na wadau wengine katika soko la vifaa, programu. Kupitia uvumbuzi wa
teknolojia pamoja na kushirikiana na wadau mbalimbali, kampuni ya Huawei ina
ahidi kuleta vifaa Zaidi kwa wateja wake wote duniani.
Kuhusu Huawei
Huawei ni vinara wa teknolojia na mawasiliano hususani katika kutimiza
matakwa ya wateja wao, katika kuhakikisha wanawapa wateja wao kile kilicho bora
katika viwango vya juu, umuhimu wa mawasiliano na vifaa vya mawasiliano
vinatumika katika nnchi Zaidi ya 170 na mikoa yake, Huawei ilishika nafasi ya
228 ulimwenguni kwa mwaka kutokana na mapato yake mwaka 2014 kati ya makampuni
500. Mapato ya kampuni yamefikia kiasi cha dolla za kimarekani bilioni 46.5.
Huawei imeshika nafasi ya 3 kwenye usambazaji wa simu kwa mwaka 2015 kwa
kusambaza zaidi ya simu milioni 100 duniani kote, Kampuni ya Huawei ipo katika
kuhakikisha inatoa ushirikiano katika kukuza na kuboresha vifaa vya
mawasiliano duniani kote.
Kampuni ya Huawei inajihusisha na utengenezaji wa simu za mkononi,
huduma za intaneti kwa njia ya modemu na vifaa vya matumizi ya nyumbani.
Huawei imeimarisha mahusiania ya biashara na makampuni kama Tigo,
Vodacom, Tigo, Vodacom, Airtel, Zantel, Sasatel, TTCL, SmileCom, Safaricom,
MTN, CellC, Telefónica, China Mobile, Vodafone, T-Mobile, BT, China Telecom,
NTT Docomo, France Telecom, na China Unicom.
Kupata habari Zaidi tembelea www.huaweidevice.com
No comments:
Post a Comment