Habari za Punde

UVCCM:Dk Magufuli Anatekeleza Sera za CCM kwa Vitendo

 Na Fahadi Siraji, Same 
Umoja wa Vijana  wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesema mambo yote yanayofanywa  na Rais Dk John Magufuli tokea ashike madaraka anatekeleza misingi ya  sera, shabaha na malengo yatokanayo  na ilani ya uchaguzi ya CCM   ya mwaka 2015/2020.

Imeelezwa kuwa kamwe baba hatelezi mambo yafanywayo aidha hayakutoka  mbinguni au kwenye  mwezi bali yanayofanywa na serikali yake ni maelekezo ya kisera yatokanayo na umakini wa CCM. 
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka ameeleza hayo jana  katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika eneo la Stendi Kubwa Wilayani  Same Mashariki.

Shaka alisema kasi ya utendaji mahiri wa serikali ya Rais Dk Magufuli si nguvu ya soda kwasababu Chama Cha Mapinduzi kipo hai, kinafuatilia ufanisi wa miongozo, sera na program zake hivyo  kitaendelea kuiagiza serikali itekeleze kila hatua kwa lengo la kufufua uchumi, kukomesha wizi, ubadhirifu  na kutumbua majipu. 

Alisema ni jambo la kusikitisha anapowasikia baadhi ya wapinzani wakiwemo Chadema baada ya kukiri kuwa CCM ni kiboko yao kimeamua kudandia hoja na kusema ati Dk Magufuli anatekekeza ilani ya upinzani. 
"Iko wapi hiyo inayoitwa ilani ya uchaguzi ya upinzani, sikumbuki kama wana ilani ya uchaguzi. nijuavyo wana shehena ya magunia ya matusi, jeuri na ubabaishaji si Ilani kama ile ya CCM "alieleza Shaka. 
Aidha alisema UVCCM na chama vimempa ruksa na baraka Dk Magufuli  azidi kutumbua majipu, abinye vipele ikiwabhapana budi ayafanyie uoasuaji maeneo yote yenye uvimbe au uchafu  .
Shaka alisema dhamira alionayo Rais Dk Magufuli ni kuhakikisha anarudisha heshima ya serikali , kuleta mageuzi ya kiutendaji maeneo ya kazi, kupambana na wahujumu uchumi pia kusadusha kila eneo la utoaji  haki na wajibu masuala hayo yakifanyika . 

"Chama chetu hakikufanya kosa kulipitisha jina la Dk Magufuli awe  Mgombea Urais hadi CCM kuifikia uamuzi ule  wakubwa wetu  waliakini akiwa mgombea hana  makandokando na akipewa nchi atamudu  "alieleza Kaimu huyo Katibu Mkuu . 
Msafara wa Mapokezi ya Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka akiwa ziarani Mkoa wa Mara baada ya kuwasili katika Wilaya ya Same
Umati wa wananchi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi ukimpokea kwa Shangwe na Nderemo.

Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka Akihutubia Umati wa wanachama wa CCM mara baada ya kukabidhi kadi kwa wanachama Wapya 

Wanachama wapya  wakila kiapo cha chama  na Jumuiya katika kikao cha ndani kilicho fanyika katika Wilaya ya Same Magharibi
Wanachama wapya  wakila kiapo cha chama  na Jumuiya katika kikao cha ndani kilicho fanyika katika Wilaya ya Same Magharibi
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akikabidhi kadi kwa Wanzchama wapya wa Chipukizi mara baada ya kuwasiri katika viwanja vya Stend Kubwa, akiwa katika ziara yake ya Kikazi Mkoani Mara. 
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Ndg. Shaka Hamdu Shaka akimkabidhi kadi ya Chama cha Mapinduzi aliekuwa Mgombea Udiwani Kata ya Kisima Wilaya ya Same kupitia CHADEMA Ndg:Mgonja, baada ya kukihama chama hicho na kujiunga na CCM.
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndg.Shaka Hamdu Shaka akionyesha Kadi mara baada ya kuzipokea wakati wa mkutano wake wa hadhara akiwa katika ziara yake Mkoani Mara.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.