STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 09Juni, 2016
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo
amekutana na kuzungumza na watumishi wa vyombo vya habari vya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar na kuhimiza
ushirikiano na mahusiano mazuri kazini ili kufanikisha malengo yaliyowekwa.
Katika
mkutano huo ulioshirikisha pia viongozi na
watendaji wakuu wa Wizara ya Habari,
Utalii, Utamaduni na Michezo, Dk. Shein alisisitiza
umuhimu wa vikao vya mara
kwa mara katika sehemu za kazi ili kujenga mahusiano hayo ambayo ni muhimu
katika kuleta ufanisi mahala pa kazi.
“katika
mahala pa kazi utawala na uongozi unahitaji
vikao kwani ni muhimu katika kujenga mahusiano
kazini na hatimae kuweza kufikia malengo” Dk. Shein
alisema.
Aliwaeleza
watumishi hao kutoka Shirika la Magazeti
la Serikali linalochapisha gazeti la
Zanzibar Leo, Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) Redio na
Televisheni pamoja
na Idara ya Habari MAELEZO kuongeza juhudi na kufanyakazi kwa weledi kwa kuwa wananchi wana imani kubwa na vyombo hivyo vya serikali hivyo ni wajibu wao
kuhakikisha wanakidhi matarajio ya wananchi.
Dk.
Shein alivitaka vyombo hivyo vya habari vya serikali kwenda na kasi ya
mabadiliko kwani wananchi wana hamu kuona vyombo hivyo vinafanya vizuri zaidi.
“Tunataka
mabadiliko ya viongozi, watendaji na watumishi ili kujenga timu moja makini
yenye uwezo wa kusimamia na kutekeleza majukumu ya wizara na idara zake
kikamilifu” Dk. Shein alisema na kudokeza kuwa mabadiliko aliyoyafanya katika
uongozi wa wizara hiyo lengo lake ni kuleta ufanisi na
Kuhusu
maslahi ya watumishi wa vyombo hivyo vya habari Dk. Shein alisisitiza kuwa
serikali inayafanyia kazi kama ilivyo kwa watumishi wengine wa serikali lakini
alikiri kuwa kumekuwepo na ucheleweshaji katika kutekeleza maagizo ya Serikali
katika suala hilo kwa upande wa wizara hiyo.
Kwa
hivyo aliiagiza wizara kutekeleza maagizo hayo mara moja ikiwemo suala la
muundo wa utumishi (sheme of service) kwa ZBC na maslahi mengine ya watumishi
wa taasisi hizo za serikali.
“Lazima
muundo wa utumishi uwepo ili mtumishi ajue maslahi yake, wajibu wake na nafasi
yake katika shirika na hapo ndio tutaweza kuwajibishana” Dk. Shein alieleza.
Alitumia
fursa hiyo kuvipongeza vyombo hivyo vya habari kwa kazi nzuri inayofanya kwa
jamii pamoja na kuwa vinazowakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Dk.
Shein aliwawahakikishia watumishi hao kuwa serikali inatambua umuhimu wa
mafunzo kwa watumishi wake hivyo kila itakapowezekana watumishi watapewa fursa
za mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi na mengine katika sehenu za kazi.
Katika
mkutano huo Mheshimiwa Rais alirejea tena wito wake wa kuwataka viongozi wa
serikali wakiwemo Mawaziri na Makatibu Wakuu kutoa ushirikiano kwa vyombo vya
habari ili kutangaza shughuli za serikali.
Dk.
Shein alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha watumishi wa vyombo hivyo vya habari
vya serikali kuimarisha nidhamu kazini ikiwemo kusoma na kuzifahamu vyema
sheria na kanuni za kazi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma yao.
Akizungumza
katika mkutano huo, Waziri wa Habari,
Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali
Juma lieleza kuwa uongozi mpya wa wizara tayari umeonana na kuzungumza na
watumishi wa Idara na vitendo mbalimbali vya wizara ili kufahamu changamoto
zinazowakabili.
Alibainisha
kuwa mojawapo ya njia ya za kukabiliana
changamoto hizo ni kutumia vizuri
rasilimali zilizopo
na kusimamia mapato. Katika mkutano huo
watumishi walieleza
changamoto mbalimbali
zinazowakabili ikiwemo uchakavu wa vifaa, usafiri na
maslahi duni.
Postal Address: 2422 Tel.+255 776 613 015,
Fax: 024 2231822
No comments:
Post a Comment