Habari za Punde

ZSTC yaandaa mkutano maalum na wakulima wa zao la Karafuu ksiwani Pemba

 MMOJA ya wakulima wa zao la Karafuu Wilaya ya Chake Chake Kisiwani Pemba, akichangia mada katika mkutano maalumu wa wakulima wa zao hilo ulioandaliwa na Shirika la biashara Taifa Zanzibar ZSTC huko katika ukumbi wa Makonyo Wawi.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MKURUGENZI wa Shirika la Bima la Zanzibar Ofisi ya Pemba, Said Abdalla Suleiman, aklitoa ufafanuzi juu ya fidia wanazowalipa wananchi wanaoanguka mikarafuu katika msimu wa mavuno.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 WAKULIMA mbali mbali wa zao la Karafuu Wilaya ya Chake Chake wakifuatia hutuba ya Mkuu wa Mkoa huo wakati wa kufungua mkutano huo wa wakulima katika ukumbi wa Makonyo Wawi Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla, akizungumza na wakulima wa zao la Karafuu Wilaya ya Chake Chake huko katika Ukumbi wa Makonyo Wawi Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)



MKULIMA bora wa kwanza Wilaya ya Chake Chake Ali Mohamed Nassor, akipokea cheti chake kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla, huko katika ukumbi wa kiwanda wa Makonyo chake chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.