Habari za Punde

Ibada na Mazishi ya Mwanahabari Marehemu Charles Sokoro wa Barmedas TV Yanafanyika Jijini Mwanza.

Ibada ya Mazishi ya aliekuwa Mkuu wa Vipindi na Afisa Mahusiano katika kituo cha runinga cha Barmedas Tv cha Jijini Mwanza, Mwalimu Charles Sokoro, imefanyika jana katika Kanisa la AICT Makongoro na kufuatiwa na mazishi yaliyofanyika katika Makaburi ya Kitangiri.

Mwalimu Sokoro ambae pia alikuwa mwalimu wa muziki wa Injili na Mwenyekiti wa Kwaya ya AICT Makongoro, alifariki jumamosi Julai 16,2016 majira ya saa mbili usiku katika Hospitali ya Rufaa Bugando baada ya kuugua kwa miezi kadhaa.

Alizaliwa mwaka julai mosi mwaka 1965 katika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza na hadi mauti yanamkuta alikuwa na umri wa 51 ambapo ameacha watoto wanne, alikuwa mgane.
Na BMG
Kwaya ya AICT Makongoro ikiimba katika ibada ya mazishi ya Sokoro
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la AICT Makongoro akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Baba Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la AICT Makongoro, akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Mmoja wawanafamilia wa marehemu Sokoro akisoma wasifu wa marehemu Sokoro.

Mchungaji Mika Ngusa kutoka TCRA akihubiri katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Jackson Manji Songo akiongoza ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro
Mkurugenzi wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania, Abubakar Karsan, akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Wanahabari
Maganga James Gwensaga ambae ni Meneja wa HHC ALive Radio ya Jijini Mwanza, akitoa salamu za rambirambi kutoka kwa wanahabari wa kundi la mtandao wa Whatsupp la BMG Tanzania, ambalo pia marehemu Mwl.Sokoro alikuwa mwanachama.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi akitoa salamu za rambirambi
Mkurugenzi wa Barmedas Tv, alikokuwa akifanya kazi Mwl.Sokoro
Viongozi mbalimbali wa dini mkoani Mwanza, pamoja na waombolezaji wakiwa katika ibada ya marehemu Sokoro.
Viongozi mbalimbali wa dini mkoani Mwanza, pamoja na waombolezaji wakiwa katika ibada ya marehemu Sokoro.
Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Mwanza, na mwanachama wa BMG Tanzania, Edwin Soko, pamoja na waombolezaji wakitoa wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro
Mhariri wa Lake Fm Radio ya Jijini Mwanza, na mwanachama wa BMG Tanzania, Amos Gomba, pamoja na waombolezaji wengine wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro
Haleluya Benjamin kutoka Mtandao wa Wanahabari Watoto mkoani Mwanza pamoja na waombolezaji wengine wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro
Meneja wa Metro Fm ya Jijini Mwanza, na mwanachama wa BMG Tanzania, Alphonce Tonny Kapela, pamoja na waombolezaji wengine wakitoa wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro
Baadhi ya wafanyakazi wa Barmedas Tv pamoja na waombolezaji wengine wakiwa katika mazishi ya mwalimu Sokoro
Mmoja wa watoto wa marehemu Sokoro (mwenye shati jeupe) akiwa na waombolezaji wengine katika mazishi ya Mwalimu Sokoro
Ibada ya Mazishi katika makaburi ya Kitangiri
Shangazi wa marehemu akimwaga udongo ishara ya kuuaga mwili wa marehemu Sokoro
Viongozi wa Barmedas Tv wakimwaga udongo ishara ya kuuaga mwili wa marehemu Sokoro
Mkurugenzi wa Barmedas Tv akimwaga udongo ishara ya kuuaga mwili wa marehemu Sokoro
Baadhi ya Waandishi wa Habari wa kundi la Whatsupp la BMG Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Barmedas Tv
Baadhi ya Waandishi wa Habari wa kundi la Whatsupp la BMG Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Barmedas Tv

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.