Na Haji Nassor, Pemba
VIJANA wa taifa
la Tanzania sasa wameshafikia zaidi ya 16 milioni (sensa 2012).
Ndani yake wamo
wasomi waliobobea, kwenye fani tofauti ambazo naanimi wakiungana pamoja, taifa
hili linaweza kupiga hatua kubwa tena ya kisayansi.
Wangapi
wamekuwa wakitorokea nchi za mashariki ya mbali, eti kusaka maisha bora, na
haya yamekuja baada ya waasisi wa taifa hili rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere na mwenzake wa Zanzibar sheikh Abeid Amani
Karume kutukomboa.
Wastani wa
vijana 50,000 kila mwaka wanaripotiwa kumaliza elimu yao ya juu hapa Tanzania,
iwe ni daktari, mawasiliano ya umma na habari, uhandisi, ualimu, kilimo na hata
kwenye sayansi ya siasa na utawala.
Taifa hili
lazima iwe ni majabu, kwamba eti itokezee skuli iwe na uhaba wa waalimu na kwa
mfano serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ifike pahala hata iwaajiri waalimu
kutoka nje ya Tanzania.
Inawezekana
huku ni kukosa uzalendo, kutopenda taifa, ndugu, jamaa na marafiki kwa hawa
vijana wanaomaliza fani kama ya ualimu na kukimbilia nchi jirani kama za Kenya,
Uganda, Rwanda na au nje ya Afrika.
Hawajiulizi
kwamba kama waasisi wa taifa hili wengekimbilia nje ya nchi, leo na kesho tungekuwa
bado wanyonge wa kielimu, uchumi na hata ubora wa siasa uliopo sasa
usingejitokeza.
Nia thabiti ya
vijana wetu hasa wenye utaalamu na walioupatia ndani ya taifa letu, na kisha
kuwanufaisha wengine inauma sana, uko wapi uzalendo, mapenzi ya utaifa, na
malengo ya kufikia tutakapo.
Kwenye takwimu
ya vijana zaidi ya 16 milioni wa Tanzania, kijana Masoud Ali Mohamed nae
ameongeza idadi hiyo kwenye sensa ya watu na makaazi ilioendeshwa nchi zima
mwaka 2012.
KIELIMU MASOUD
Kijana huyo
aliezaliwa mwishoni mwa miaka ya sabini (1978) katika kijiji cha Ole wilaya ya
wete Pemba, na kuanza kunolewa kwa elimu yake ya msingi katika Skuli ya Ole hadi
darasa la tatu kijijini hapo kuanzia mwaka 1987-1990, na kisha kuhamia kisiwa
cha Unguja.
Masoud akiwa
kwenye heka heka za kujitafutia elimu zaidi miaka kuanzia ya 1990-1998
alizikalia kitako skuli za Kajificheni kisha Hamamni kwa elimu ya msingi na
sekondari, kabla ya kujinga na elimu juu ya kidato cha tano na sita skuli ya
Lumumba mwaka 1999/2001.
Masoud akiwa
kwenye ngarambe za kada ya kielimu, alikuwa tofauti na vijana wengi wa sasa,
ambapo yeye alikuwa akifuatilia sana hotuba za wasisi wa taifa hili, hadi
kufika wakati wenzake wakidhani anaweza kufeli masomo yake.
“Mimi na hotuba
za Nyerere au Karume, ni sawa na mwalimu Nyerere na Azimio la Arusha, huwa
naamini ndani ya moyo wangu kuwa maneno ya
wazee hawa yana falsafa iliyotukuka na chakula cha ubongo wenye kuhitaji maono
ya hali ya juu.’’,alidokeza akizungumza nami.
Mwaka 2001 aliajiriwa na wizara ya elimu, akiwa
mwalimu katika skuli ya sekondari ya Benbela na kubadilishwa jina na hata wazazi
wake, kwa kumuita mwalimu Masoud, mwaka mmoja baadae yaani 2002, kijana
huyo alijiunga na chuo kikuu cha Dar es Salaam ‘Mlimani’ kuchukuwa Shahada ya
kwanza kwenye fani ya sayansi ya siasa na utawala (BA PSPA).
“Niliamua kuchukua
fani ya ‘Political science’ kwani niliamini ni miongoni mwa fani zenye mchango
mkubwa chanya hasa katika siasa hizi za Nchi changa na kuweza kutoa mchango
mkubwa kwa Taifa langu’’,alifafanua.
Akiwa
chuoni hapo Massoud kutokana na utundu wake wa kimasomo, aliwahi kukabidhiwa vyeti
mbali mbali kutokana na ushiriki adhimu na wenye mchango mkubwa katika jumuia
kadhaa zilizokuwepo chuoni hapo, aliwahi kutunukiwa vyeti katika masuala ya
haki za binadamu, “Red Cross”na Jumuia ya wanafunzi wa sayansi ya siasa na
utawala.
Aliwahi
kushiriki mijadala na makongamano mbali mbali yaliokuwa yakiandaliwa chuoni
hapo, na hata tasisi nyengine, ambapo alikiri kwamba ndio yaliomutesha mbawa
hadi leo hii kufikia kujiamiani.
Baada
ya kumaliza miaka mitatu chuo kikuu cha Dar es Salaam alitunukiwa Shahada ya
heshima BA (Honours) katika fani ya Sayansi ya Siasa na Utawala/Uongozi wa Umma
(BA (Honours) in Political Science and Public Administration.
Omar
Hassan Ali ambae alisoma na Masoud kwenye elimu ya sekondari, alisema alikuwa
mtulivu na hakuwa na marafiki watundu na hadi kumpachika jina la ‘sheikh Masoud’
wakati huo ila alikua na kipaji cha ajabu katika masomo ya Historia, Civics na
Kiswahili.
“Kwa
kweli Masoud nilikuwa namfahamu sana, na wapo waliosema pamoja na kutokua
mchangamfu anaweza kufika mbali, maana alikuwa anafuatilia masomo yake kwa
karibu”,alifafanua
Mwalimu
aliewahi kufundisha na Masoud Ali Mohamed katika Skuli ya Benbela, mwalimu Ali
Haji Ali alisema miongoni mwa waalimu wanzake waliokuwa makini na kazi hiyo ya
ualimu, ingawa kwa muda mfupi mmoja wao ni mwalimu Masoud (sheikh Masoud).
“Mimi
nilikuwa karibu sana na waalimu wote, lakini mwalimu Masoud, nilikuwa karibu
nae zaidi, maana nilikuwa napata kitu kipya chenye maana kitaaluma na maisha kila
siku kutoka kwake”,alifafanua.
Hassan
Ramadhan rafiki wa Masoud anaeishi Vuga mjini Unguja, alisema kijana huyo
pamoja na umri wake kumruhusu kufanya mambo ambayo yalikuwa yakitendwa na rika
lao, yeye alikuwa zaidi kwenye masomo yake.
Katibu
wa UVCCM wa Wilaya ya Kusini Ramadhani Mcheju anamueleza Masoud kama kijana
aliyeshiba uzalendo kwa Taifa lake na mwenye maadili ya hali ya juu sana na
mapenzi makubwa kwa Chama cha Mapinduzi.
“Unapoona
kijana aina ya Masoud mwenye elimu yake, maisha yake na akaamua kujitoa muhanga
kukipigania Chama cha Mapinduzi hasa maeneo ya Pemba, lazima ujuwe huyu ni
kijana mwenye upeo na uzalendo wa kipekee na kinachomuongoza Masoud ni imani ya
kuwa CCM ndio mkombozi wa mnyonge na chama chenye historia iliyotukuka kwa
Taifa hili”, anaeleza Katibu Ramadhani Mcheju.
Masoud
baada ya kumaliza chuo kikuu cha Dar-es Salaam mwaka 2005, mwaka mmoja baadae
alifanikiwa kujinga na chuo kimoja kilichopo Mkoani Mbeya Tanzania muda wa
miezi tisa kwa ajili ya kupata mafunzo ya ziada mwaka 2007 alimaliza.
KISIASA
MASOUD
Masoud
ambae hakuficha kwamba ni mwanchama hai na madhubuti wa CCM alisema anazo
sababu zaidi ya kumi nzito za kuwa mwanachama wa chama hicho, moja akitaja
kwamba kina dira madhubuti isiyoyumba na ndio chama pekee chenye sura ya
kitaifa, kimuundo na kiitikadi.
“Nangalia
Afrika ni chama gani kinafanana na CCM cha Tanzania, lakini huwa nashindwa
kufafanisha kutokana na CCM kwanza kuwa na histori isiofutika na hasa wakati wa
TANU na ASP kuwang’oa madhalimu wa taifa.
Mbona
Masoud inaaminika kwamba wasomi wengi wenye fani kama yako, twaelezwa kwamba
wanakimbilia vyama vyengine wewe iweje na CCM? nilimuliza na kusema sio sahihi.
“Unajua
unapomaliza sayansi ya siasa na uongozi kuelewa historia ya nchi yetu kupitia
hotuba mbali mbali za waasisi wetu na ukazifahamu malengo na thamani yake,
lazima wewe utaingia CCM au utaipigia kura wakati ukifika, vinginevyo hutakuwa
mzalendo wa Taifa lako’’,alisema.
Masoud
alifafanua zaidi kwamba waasisi wa taifa hili walifanya kazi kubwa hadi leo
ikapatikana idadi kubwa ya vijana ambao ni wasomi, sasa hoja yenye mantiki ya
kuwapinga inatoka wapi, alihoji.
Kijana
Masoud ambae alikata kadi ya chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1998 tawi la
Shangani mjini Unguja, ambapo baadae mwaka 2007 alishajipanga kuingia ndani ya
chama kiuongozi, yeye ni muumini mkubwa sana wa muungano na kusema una faida
lukuki.
“Angalia faida ya Muungano wetu wa mwaka 1964,
mimi nimezaliwa wilaya ya Wete Pemba mwaka 1978, lakini miaka 30 baadae nikiwa Bukoba
Mkoa wa Kagera niligombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM hasa UVCCM
mwaka 2008 na nilichaguliwa kwa nafasi zote nikawa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa
Mkoa wa UVCCM Kagera.
Aidha
Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya UVCCM, Mjumbe wa Baraza la Wilaya UVCCM Bukoba
Mjini, Mjumbe wa Kamati Tekelezaji ya Wilaya ya Bukoba Mjini UVCCM, pia Mjumbe
wa Mkutano Mkuu wa Taifa UVCCM Bukoba mjini, hizi zote ni nafasi za siasa
ambazo aliwahi kuzihudumu kijana huyu.
Kilichompeleka
huko ni kazi yake ambayo hakupenda kuitaja, ingawa baada ya kukaa huko tokea
miaka ya 2007 hadi mwaka 2010 alipojitosa katika kinyang’anyiro kizito cha
kuwania Ubunge kupitia CCM jimbo la Ole Wilaya ya Wete, Mkoa Kaskazini Pemba na
hatimae alishinda kura za maoni na kuteuliwa Halmashauri Kuu ya Taifa kuwa
mgombea Ubunge Jimbo hilo ila kura hazikutosha katika uchaguzi mkuu .
Akiwa
ndani ya siasa, aliona kila kitu ni rahisi kukitekeleza hasa kwa vile tayari
ameshamaliza elimu yake ya masuala ya kisiasa, ingawa ushauri na maelekezo
alisema kwake ndio chakula.
“Unajua
siasa ukishapata waelekezaji wazuri basi hakuna ambalo utashindwa kulifanya,
maana mimi mwenyewe nilikuwa nashauri wadogo zangu, ingawa sisahau pia hotuba
za wasisi wetu’’,alisema.
Hasnuu
Faki Hassan kutoka Jimbo la Ole, Pemba ambaye pia ni Daktari katika hospitali
ya Chake akizungumza kwenye moja ya kongamano ambalo Masoud alitoa mada ya
katiba pendekezwa, alisema atawashawishi wanaccm kumpitisha tena kijana huyo
kugombea Ubunge Jimbo la Ole.
“Mimi
tokea nizaliwe sijakumbana na kijana mwenye upeo na uelewa hasa wa mambo ya
kitaifa na uzalendo kama alivyo kijana Massoud, na nitawashawishi wengine ili
Masoud kama yuko tayari aje agombee jimboni’’,alieleza.
Masoud
alisema hatosahau ndani ya uongozi wake wa UVCCM wakati akiwa mjumbe wa mkutano
mkuu wa Taifa Dodoma alipohudhuria Mkutano mkuu wa saba wa UVCCM na hapo ndipo
alijiridhisha zaidi kuwa CCM ni chama cha Ukombozi na chama cha Kitaifa.
KWENYE
KATIBA.
Yeye
binafsi alisema hakutarajia hata siku moja kwamba ingetokezea wananchi wa
Tanzania kushirikishwa juu ya utungwaji wa katiba maana imekuwa ni jambo adimu
hasa kwa siasa za kiafrika.
Masoud
alisema wakati akiwa chuo kikuu na hata skuli kusoma elimu ya sekondari alikuwa
akisikia kwamba katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, imekua
na mapungufu.
Lakini
hata yeye baada ya kuisoma na kuiangalia, aliona hayo ingawa bado ni Katiba
bora, Uongozi wa rais Dk Jakaya Mrisho Kikwete na Dk Ali Mohammed Shein ndio walioanzisha
mchakato wa kuandikwa kwa katiba hiyo jambo ambalo litawafanya wakumbukwe
milele.
Hatua
ya kukusanya maoni, hadi kufikia ngazi ya wilaya na hatima bunge maalumu la
katiba, na vijana kushiriki, kwa Masoud anasema hiyo ni heshima kubwa.
“Ukitaka
kuzihesabu nchi zilizofanya zoezi la kuandika katiba mpya kama ilivyofanya
Tanzania ni chache sana, sasa lazima vijana waheshimi hili na kuona kwamba ni
fursa adhimu’’,alisema.
Hadi
sasa anasema hajafahamu lengo, dhamira na makusudio ya wale wanazunguka nchi
zima kuwataka wananchi waipigie kura ya ‘HAPANA’ katiba hiyo.
Kwake
yeye anaona kama anapata shaka, kwamba inawezekana makundi hayo ya watu iwe ni
wanasiasa, makundi ya dini, asasi za kiraia nia yao hasa sio katiba inawezekana
na kuuchukia Mungano.
Wapo
wanasiasa walikua na madai ya muda mrefu kwamba Katiba iliopo ya mwaka 1977 ya
Jamhuri ya Mungano wa Tanzania inaishusha hadhi Zanzibar na kukosa hata fursa
ya kujiunga na mashirika ya kimataifa.
Alidondoa
baadhi ya vipengele ambavyo yeye vinamshawishi kuipigia kura ya ‘NDIO’ katiba
hiyo, kama kwenye Ibara ya 57, ambayo imetaja haki za wanawake moja kwa moja,
huku kwenye katiba ya sasa hilo likikosekana.
Alitaja
Ibara nyengine ya 78 (i) juu ya wajibu wa viongozi wakuu kulinda Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar ambao uliasisiwa na viongozi wakuu wa nchi mbili hizi.
“Kwangu
mimi anaepinga Muungano, hasa muungano huu tulionao ni sawa na mhaini” ,alisema
Masoud.
Suala
la tume huru ya uchaguzi, alisema nayo imewekwa kwenye Ibara ya 252, ambalo
kubwa na la kujivunia Masoud alisema ni kupewa uwezo kisheria Zanzibar kukopa
ndani na nje.
Kubwa
aliwaasa hasa vijana wenzake kuhakikisha katiba hiyo inayopendekezwa wakati ukifika
wanaipiga kura ya ‘NDIO’kwani watakuwa wamelitendea haki Taifa lao na historia
itakuja kuwatukuza kwa vizazi vijavyo.
RUSHWA
Kijana
huyo amekuwa akiwachukia kwa kinywa kipana walarushwa na watoaji, na katika
hili haangalii chama, bali anavyotaka ni kuhakikisha viongozi wanatekeleza
maagizo ya waasisi wa taifa hili kwa vitendo.
“Vitendo
vya rushwa vimekuwa wazi wazi hasa nyakati kama hizi za kuelekea uchaguzi mkuu
wa vyama vingi, lakini ni vyema wenye mamlaka ya kufanya hivyo wawe
makini’’,alisema kwa uchungu.
Na
ndio maana kijana huyo alilishukuru sana bunge maalumu la katiba kwa kuipitisha
sura ya nne, Ibara 249 ambacho kimeeleza uanzishwa wa chombo cha kuzuia na
kupambana na rushwa.
MUUNGANO
WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
Kwenye
hili anasema halifai kuingizwa kama jambo la kisasa, maana ndio utanzania wa
wananchi hata walioko Zanzibar na wamekuwa wakijivunia pahala popote wendapo.
Haridhishwi
hata kidogo na wale wenye kuomba dua kwamba eti siku moja uwe haupo, huku
akiamini kwamba inawezekana wanafanya hivyo wakikosa kujua athari na madhara
yake hasa kwenye uchumi na usalama wa nchi yetu.
“Hebu
tujifunze kwa wenzetu ni nchi gani iliyowahi kuungana baadae zikatengana na
zikaendelea kubakia salama, jibu ni kuwa hakuna, angalia pale Sudan Kaskazini
na Sudan Kusini, watu wasome historia za nchi nyingi, wasilazimishe
kutufarakanisha kwa faida za kisiasa”, alifafanua Masoud.
“Waliowengi
wanadhani siasa ni kusimama kwenye jukwaa na watu wakacheka na wengine
wakakupigia kofi unapoeleza mambo ambayo taifa linaweza kuanza mwanzo
kujulikana ulimwenguni”,alifafanua.
Alitaja
faida moja kubwa ya Muungano huo kwamba hakuna mtanzania bara wala mzanzibari
anaemkebehi mwenzake, bali kila mmoja anajinasibu kwa utaifa wa Tanzania
uliopatikana kwa Mungano.
Aliwaasa
wanasiasa na hasa vijana wenzake kuacha kuchezea shilingi chooni ikitumbukia
moja kwa moja moja ni sawa na kua na utawala wa kikoloni, maana nchi daima
haitotulia tena.
“Muungano
huu hasa unaimarika vyema na kunawiri unapokua kwenye serikali mbili kama
ilivyo kwenye Ibara ya 1 ya katiba ya sasa ya mwaka 1977 na katiba inayopendekezwa
kwenye Ibara kama hiyo’,alisema kwa kunukuu katiba.
UZALENDO
Bado
kijana Masoud hajapata taswira ya uhakika kuona vijana waliosomeshwa kwenye
wakati mgumu ndani ya taifa hili kisha kwenda mashariki ya mbali kuwanufaisha
wengine.
Yeye
alisema zipo wilaya za Tanzania bara kwenye skuli zake tena za sekondari
zinauhaba mkubwa wa waalimu au kama ni hospitali kuna upungufu wa madaktari
wakati waliokuwepo wanatoa huduma kwa wengine.
Alionesha
uchungu na kusema kuwa ndani ya Ibara ya 52 ya katiba inayopendekezwa, elimu
kwa kila mtanzania ni haki yake, ingawa anawashangaa wengine haki hiyo
kuipeleka nchi jirani.
KIJAMII
Aliesema
amekuwa akipata ushawishi sana kutoka kwa vijana hasa waliosoma pamoja kwamba,
atafute nchi akasake maisha, ingawa dhamira yake ni kuoja jamii ya Tanzania
inaendelea kupata mafanikio kupitia mawazo yake na ni sehemu ya kulipia fadhila
kwa Taifa lake.
“Hebu
fikiria kama akina Mwalimu Nyerere na Mzee Karume wangekimbia nchi kwa
visingizio vya kutafuta maisha binafsi, ile dhamira yao ya dhati ya kuikomboa
nchi yetu je ingefanikiwa? jibu ni hapana!” alisema Masoud.
Hafurahishwi
hata kidogo kuona jamii inakosa wasaidizi wakati wazazi na Serikali
wameshatumia unyonge wa fedha zao kumsomesha kijana kisha kusahau aliokotoka.
“Mimi
ninahamu kama nikifanikiwa kiuwezo, basi nitembelee vijiji vyenye shida sana
niwatatulie ili nijiwekee historia na huku ndio kutekeleza hutuba na maagizo ya
wasisi wa taifa hili’’,alifafanua.
Kijana
Masoud amewataka vijana wenzake kuendelea kufikiria njia sahihi ya kuliinua
taifa hili na badala ya kupanga mipango na mikakati ya kwenda kutafuta maisha
nchi nyingine kwani kufanya hivyo ni kielelezo cha kukosa uzalendo.
Hata
hivyo amewataka vijana wasiogope kuijingiza kwenye masuala ya uongozi, akiamini
kwamba huko ni sehemu mojawapo wanakoweza kutoa wigo mpana juu ya kulitendea
mema taifa lao.
HALI YA NDOA
Katika kuhakikisha
Massoud kwa nia yake ya kuimarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, alisema
alijipoza kwa mpendwa wake anaetokea Mkoa wa Mara na kukubali kufunga ndoa nae,
na tayari ameshapata matunda kwa kuwa na mtoto mmoja.
Massuod yeye ni kijana wa
kwanza kuona mwanga kwenye familia ya watoto kumi na moja ya bawana Ali Mohamed
Ali na bibi Maryam Massoud Nassor ambao wote bado wako hai wakiendelea kufaida
matunda ya mtoto wao.
URAFIKI
Kijana huyo,
amekiri kwamba hakuna hata mtanzania mmoja anaemkaribia kwa kuwa na idadi kubwa
ya marafiki weme, ambapo hata Maulid Shibu Said rafiki yake wa karibu anao
wengi wanaofanana.
UONGOZI.
Rais Wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe: dk Ali Mohamed
Shein, alimteua kuwa Afisa Mdhamini Wizara ya Nchi Afisi ya Rais, Katiba,
Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala bora Pemba, na sasa anaiongoza wizara hiyo.
Kubwa kwenye
mikakati yake, ni kuona kila mmoja anafanya wajibu wake, nay eye kusimamia haki
zake bila ya ubaguzi wala kupendelea akiamini kuwa, kufanya hivyo ni kutekeleza
sheria za kazi kwa vitendo.
No comments:
Post a Comment