Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Bw. Mogens Lykketoft akiwazungumza washindi 60 wa Insha kuhusu Lugha Nyingi, Dunia Moja, miongoni mwa washindi hao ni mwanafunzi wa Kitanzania Amani Alfred Naburi anayesoma Chuo Kikuu cha African Leadership kilichopo nchini Mauritius wengine katika picha ni Mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya Umma ya Umoja wa Mataifa, Bi. Cristina Gallach.
Amani Alfred Naburi akisoma sehemu ya Insha yake aliyoiandika kwa lugha ya kiingereza ambayo ilizungumzia lengo namba kumi na moja la maendeleo endelevu ambalo linahusu Miji jumuishi, salama na endelevu. Hafla hii ilifanyika siku ya Ijumaa katika Ukumbi Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
Sehemu ya wanafunzi wa Insha kuhusu Lugha Nyingi, Dunia Moja wakiwa katika ukumbi Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa..Hafla hii ilikuwa ni sehemu ya Kongamano la Kimataifa la Vijana
Naburi anaonekana katika mstari wa tatu akishangilia jambo na wanafunzi wenzie kutoka mataifa mbalimbali duniani ambao walikusanyika siku ya Ijumaa baada ya kushinda uandishi wa Insha kwa kutumia lugha sita rasmi zinazotumika katika Mikutano ya Umoja wa Mataifa.
Na
Mwandishi Maalum, New York
Mwanafunzi wa Kitanzania, Amani Alfred Naburi, ni mmoja wa kati ya wanafunzi 60 kutoka Vyuo
Vikuu mbalimbali duniani ambao wameshinda
shindano la Insha ijulikanayo kama “Lugha
nyingi, Dunia Moja” ( Many languages, One World) lililoandaliwa kwa
ushirikiano baina ya United Nations
Academic Impact ( UNAI) na ELS Educational Services, Inc.
Jumla ya wanafunzi
3,600 kutoka mataifa 165 walijitokeza kuwania shindano
hilo ambalo hatimaye majaji waliwaibua wanafunzi 60 kutoka mataifa 36 kama washindi wa shindano hilo.
Amani Alfred Naburi ni mtanzania
anayesoma Chuo Kikuu cha African Leadership University, huko Mauritius. Baadhi ya masharti ya
kuingia shindano hilo lilitaka mshiriki lazima awe ni
mwanafunzi aliye
Washindi hao 60 walipata fursa ya kusoma sehemu ya Insha yao
mbele ya washindi wenzao na
washiriki wengine waliokuwa
wakihudhuria kongamano la vijana, katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
hapa Makao makuu ya Umoja wa Mataifa.
Mbali ya washindi hao 60 kuzungumza, wazungumzaji wakuu
wengine walikuwa ni ambayo
Rais wa Baraza Kuu Bw. Mogens Lykketoft na Bi Cristina Galach Naibu Katibu Mkuu Msaidizi Mwandamizi anayesimamia idara
ya Mawasiliano ya Umma ya Umoja wa
Mataifa na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu
kuhusi Vijana Bw. Ahmad Alhendawi aliwasilisha
Salamu za Katibu Mkuu Ban Ki
Moon.
Washindani wa Insha hiyo walitakiwa kuandisha Insha juu ya namna watakavyochangia katika
utekelezaji wa Malengo
Mapya ya Maendeleo Endelevu ( Agenda (2030). Ambapo kila moja wapo alitakiwa kuiandika insha hiyo yenye
maneno yasiyozidi 2,000 kwa lugha
nje ya lugha yake ya asili ya nchi anayotoka.
Tafsri yake ni kuwa walitakiwa kuandika kwa lugha sita ambazo ni rasmi na
zinazotambuliwa na
kutumika na Umoja wa Mataifa. Lugha hizo ni
Kiingereza, Kifaransa, Kiarabu,
Kichina, Kispanishi na Kirusi
Malengo waliyopewa washindani hao kuyandikia maoni hayo ni lengo namba kumi na mbili linalozungumzia Matumizi na Uzalishaji Bora ( Ensure
Sustainable consumption and production ) lililowasilishwa kwa lugha ya Kifaransa,
lengo namba kumi na sita ambalo linazungumzia kuhusu Amani,
Haki na Taasisi Imara ( Promote
just, peaceful and inclusive societies) lilowasilishwa kwa Kirusi,
lengo namba kumi na tano linaluhusu Uhai juu ya Ardhi( Sustainably manage forests, combat desertification, halt and reverse
land degradation, halt biodiversity loss ) lilowasilishwa kwa Kispanishi
Malengo mengine ni lengo
namba kumi na tatu kuhusu kuchukua
hatua kwa mbadiliko ya Tabia
nchi na
athari zake ( Take urgent action
to combat climate change and its
impacts), lengo namba tisa kuhusu
Viwanda, Ubunifu na Miundo Mbinu ( Build
resilient infrastructure, promote sustainable industrialization and foster
innovation), lengo namba kumi na moja kuhusu kuifanya miji kuwa jumuishi, salama,
na endelevu ( make cities Inclusive, safe, resilient
and sustainable). Lengo hilo ndilo
ambalo
Mwanafunzi Amani Naburi aliliandika insha kwa lugha ya kiingereza kiasi
cha kukoga nyonyo za majaj.
Lengo kuu la uandishi wa insha
kwa lugha sita rasmi zinazotumika
katika umoja wa Mataifa ni pamona na mambo mengine, kuwawezesha wanafunzi
kujifunza lugha na tamaduni za nchi
nyingine , kupanua wigo na fursa ya
kujifunza mambo na changamoto zinazoikabili dunia na kujaribu kutoa mawazo
yao yatakayoweza kusaidia katika
kuzikabili changamoto hizo.
Lengo jingine ni kuwawezesha wanafunzi kutambua uwezo na vipaji vyao kama
njia moja wapo ya kuwaandaa kuwa viongozi wa taifa la kesho.
No comments:
Post a Comment