Habari za Punde

Waziri wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, awatembelea wazee wasiojiweza Pemba

 WAZEE walioathirika wa Ungonjwa wa Ukoma wanaoishi Makundeni Kinyasini Wilaya ya Wete, wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, wakati alipowatembelea wazee hao huko wanakoishi na kuwajuulia hali.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MMOJA wa wazee walioathirika na ugonjwa wa Ukoma Makundeni Kinyasini Hamadi Abdalla, akitoa maelezo juu ya historia ya wazee hao na kuwepo hapo Makundeni kwa waziri wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, wakati alipowatembelea wazee hao.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, akimsikiliza kwa makini mmoja wa wazee wanaoishi katika nyumba ya wazee Gombani Chake Chake Pemba, wakati alipowatembelea wazee hao katika ziara yake ya siku mbili Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, akikabidhi baskeli za walemavu kwa wazee wanaoishi katika nyumba ya wazee Gombani Chake Chake Pemba, ikiwa ni msaada kutoka kwa Makamo wa pili wa rais wa Zanzibar Mhe:Balozi Seif Ali Iddi, kulia ni mtunzaji wa wazee wa Limbani Wete Jadi Mohamed Jadi.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MMOJA wa Wazee wanaoishi katika nyumba ya wazee Gombani akimueleza jambo, Waziri wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, wakati alipowatembelea wazee hao katika nyumba yao.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
WAZIRI wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico,akiwa katika picha ya pamoja na wazee wanaolelewa katika nyumba ya wazee Gombani Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.