Habari za Punde

Mkutano wa 3 wa Baraza la Wawakilishi kuanza Tarehe 21 Septemba


 Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu Afisi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Ndg Amour Mohammed akizungumza wakati wa mkutano huo. uliofanyika katika Afisi za Baraza kutoa taarifa ya kukamilika kwa Mkutano wa Baraza la Wawakilishi. 
 Mkuu wa Shughuli za Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mussa Kombo akifafanua jambo wakati wa mkutano huo na waandishi wa habari Zanzibar. 
Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar wakimsikiliza Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu wa Afisi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Ndg Amour Mohammed akizungumza kuhusiana na kukamilika kwa matayarisho ya Mkutano wa Baraza unaotarajiwa kuaza 21,Septemba2016.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAARIFA YA SHUGHULI ZA MKUTANO WA TATU  WA BARAZA LA TISA LA WAWAKILISHI UTAKAOANZA TAREHE 21 SEPTEMBA, 2016
Mkutano wa Tatu wa Baraza la Tisa la  Wawakilishi Zanzibar unatarajiwa kuanza siku ya Jumatano tarehe 21 Septemba, 2016, saa 3:00 asubuhi.
SHUGHULI ZITAKAZOFANYIKA.
Shughuli za Mkutano huo zitakuwa kama ifuatavyo:-
1.   Maswali na Majibu.
Maswali 184 yatajibiwa kwenye Mkutano huu.
2.   Miswada ya Sheria
Miswada ya Sheria iliyowasilishwa na kusomwa kwa mara ya Kwanza katika Mkutano wa mwezi Mei, 2016 itasomwa kwa mara ya pili na tatu na kujadiliwa katika Mkutano huu wa Tatu. 

Miswada yenyewe ni:-
i)             Mswada wa Sheria ya Kurekebisha Sheria ya Chuo Kikuu cha Zanzibar, Nam. 8 ya 1999 Kama ilivyorekebishwa na Sheria Nam. 11 ya 2009 na Kuweka Masharti Bora Pamoja na Mambo Mengine Yanayohusiana na Hayo.
ii)           Mswada wa Sheria ya Kuanzisha Taasisi ya Elimu ya Zanzibar na    Mambo mengine Yanayohusiana na Hayo.
iii)          Mswada wa Sheria ya Usimamizi (Utafutaji na Uchimbaji) wa Mafuta na Gesi Asilia, Kuanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia, Kuanzisha Kampuni ya Maendeleo ya Mafuta na Kuhakikisha Uwajibikaji wa Taasisi za Mafuta na Mambo Mengine Yanayohusiana na Hayo.
iv)          Mswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbali Mbali na Kuweka Masharti yaliyo Bora kuhusiana na  Mambo Hayo.
v)            Mswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya Zanzibar ya 1984.
vi)           Miswada minne (4) kusomwa kwa mara ya kwanza

          3. Marekebisho ya Kanuni za Baraza la Wawakilishi Toleo la 2012.
             
(Amour M. Amour)
Kny. Katibu
Baraza la Wawakilishi, Zanzibar   
Tarehe 19 Septemba, 2016

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.