Jengo maarufu la Beit Al Jaib ( House of Wonders) ambalo Serikali ya Tanzania inaiomba Serikali ya Oman kuangalia uwezekano wa kulikarabati kama sehemu ya mradi wa kuhifadhi nyaraka, kumbukumbu na majengoa ya kihistoria visiwani Zanzibar
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sultanate of Oman, Dkt Augustine Mahiga ( kushoto) na Yusuf bin Alawi bin Abdullah wakizungumzia kuhusu namna ya kuendelea kuimarisha uhusiano mzuri baina ya nchi hizo mbili. Katika mazungumzo hayo Waziri Mahiga ameiomba serikali ya Oman kupitia Waziri Abdullah kuangalia uwezekano wa kushirikiana katika uhifadhi ya nyaraka na kumbukumbu muhimu pamoja na ukarabati ya jengo la House of Wonders lilojengwa na ufalma wa Oman mwaka 1883
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki, Augustine Mahiga akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayehusika na masuala ya Afrika, Mazungumzo yao yalijielekeza zaidi katika uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizi mbili
Na
Mwandishi Maalum, New York
Ufalme
wa Oman umeonesha nia ya kukarabati majengo
ya makubusho ya kale ya Beit Al Jaib
maarufu kama “ House of Wonders” yaliyopo mjini
Unguja – Zanzibar.
Nia
hiyo imeoneshwa na Waziri wa Mambo
ya Nje wa Oman,
Bw. Yusuf bin Alawi bin Addullah wakati
alipokutana na kufanya mazugumzo
na Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dkt, Augustine Mahiga.
Mazungumzo baina ya
viongozi hao wawili yalifanyika
pembezoni mwa Mkutano wa 71
wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ambapo Mawaziri hao walikuwa wakiongoza ujumbe wa
Nchi zao.
Mazungumzo ya
Mawaziri hao yalijikita
katika uimarishwaji wa uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo baina ya
Oman na Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Katika majadiliano hayo ambapo pamoja
na mambo mengine, Waziri
Mahiga aliomba serikali ya Oman kuangalia uwezekano wa kuanzishwa
kwa miradi wa kutunza mambo ya kale zikiwamo nyaraka muhimu zinazohusu
uhusiano baina ya nchi hizo mbili
Waziri
Mahiga alieelezea pia hali uchakavu wa majengo ya
Beit Al Jaib ( House of wonders)
majengo yaliyokuwa Ikulu ya utawala wa Kifalme, Zanzibar. Makubusho hayo yamesheheni historia ya uhusiano
na ushirikiano kati ya Zanzibar na
Sultanate of Oman na Afrika Mashariki kwa Ujumla.
Na
kutokana na historia hiyo na umuhimu
wa jengo hilo ambalo limejengwa mwaka
1883, Waziri ameiomba Serikali ya Oman kuangalia uwezekano wa kulihifadhi jingo hilo ambalo
pia ni kivutio kikubwa cha utalii.
Akijibu ombi hilo na
mengine yaliyowasilishwa na
Waziri Mahinga, Waziria wa Mambo
ya Nje wa Oman, Bw . Yusuf bin Alawi bin Addullah amemtaka Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki kuandaa andiko na kuliwasilisha
katika Serikali ya Oman ili pendekezo
hilo liweze kufanyiwa kazi pamoja
na mapendekezo mengine.
Katika hatua nyingine, Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Augustine Mahiga amekuwa na kuwa
na mazungumgo na Bi. Linda
Thomas Greenfield, Naibu Waziri wa
Mambo ya Nje wa Marekani anayehusika na
masuala ya Afrika.
Mazungumzo
ya Waziri Mahinga na Bi.
Linda Greenfield yalijikita zaidi
katika uhusiano na ushirikiano baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Marekani.
No comments:
Post a Comment