Mbunifu wa Mavazi nchini Kurwa Mkwendule, akizungumza na waandishi jinsi ya maandalizi ya onesho hilo la aina yake linalotarajiwa kuwashirikisha warembo wanawake wanene Zanzibar na kuwataka wananchi kijitokeza katika shoo hiyo na kuchangia.
Mdhamini wa Maonesho ya Mavazi kuchangia Wagonjwa wa Kensa Zanzibar Bi Wahida Walid, akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na matayarisho ya shoo hiyo inayotarajiwa kufanyika katika ukumbi wa hoteli ya Grand Palace Malindi Zanzibar na kuwahamasisha Wanawake kujitokeza katika onesho hilo litakalowasirikisha Wanawake wanene kuonesha mitindo ya mavazi siku hiyo.
Nadya Jamishad, wakati alipozungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Serena Inn, juu ya matayarisho hayo.
Na Abdi Shamnah
Zaidi ya asilimia 45 ya wanawake waliopo Zanzibar,
ikiwemo wanaojifahamu na wasiojifahamu, wanaishi na aina tofauti za ugonjwa wa
Saratani, ikiwemo ya matiti na aina nyenginezo.
Changamoto
hiyo imetolewa na Mdhamini wa harambee ya kuhamasiha uchangiaji wa fedha, kwa
ajili ya kukabiliana na ugonjwa wa saratani ya matiti ‘Breast Cancer
Awareness’, Nadya Jamishad, wakati alipozungumza na waandishi wa habari katika
Hoteli ya Serena Inn, mjini hapa.
Mbunifu
wa Mavazi nchini Kurwa Mkwendule kwa kushikiana na Titi Ngazi, wameandaa
onyesho maalum la ubunifu wa mavazi na onyesho la wanawake wanene ‘Marashi ya
Pwani Size Fashion show, litakalofanyika Oktoba 8 mwaka huu, katika ukumbi wa Grand Palace Malindi Zanzibar, Kongwe, kwa lengo la kuchangisha fedha kusaidia wagonjwa wanaoishi na
saratani ya matiti Zanzibar.
Alisema
tafiti zilizofanywa zimebaini kuwa
Wazanzibari an Watanzania kwa ujumla wanaguswa kwa namna moja au
nyengine na kuwepo kwa ugonjwa huo, hata hivyo tatizo kubwa liliopo ni ukosefu
wa uwelewa na namna ya kuukabili ugonjwa katika hatua za awali.
Alisema
wengi wa wagonjwa wanaofika hospitali kupatiwa matibabu, hufanya hivyo wakati
ugonjwa ukiwa umewatopea katika viwiliwili vyao.
‘‘Mi
mwenyewe ni muathirika miongoni mwa saratani, wengi wa wagonjwa kutoka Zanzibar
hukimbilia Ocean Road, kati yao wengi wanauguwa saratani ya matiti na kensa ya
kizazi’, alisema.
Aidha
alisema tatizo la uwelewa juu ya ugonjwa huo, hususan kwa wananchi kisiwani
Pemba, ni tatizo linalohitaji kuchukuliwa hatua madhubuti, ili jamii iweze kufahamu
namna ya kuukabili na kuchukua hatua za haraka pale wanapoonesha dalili za kuwa
na ugonjwa huo.
‘‘
Hali hii pia inatokana na Hospitali ya Mnazi Mmoja kutokuwa na kitengo cha
kufuatilia mwenendo wa maradhi hayo pamoja na utaratibu wa kupima wananchi kila
badaa ya kipindi fulani’’, alisema.
Alibainisha
miongoni mwa vyanzo vya maradhi ya saratani ya aina zote, hutokana na jamii
kubadili mfumo wa vyakula kutoka vile vya asili na kujikita katika ulaji wa vyakula
vyenye kemikali.
Mdhamini
huyo alisema kupitia onyesho hilo, wamekusanya nguvu ili kuishajiisha jamii ya
Wazanzibar kutoa michango yao kwa ajili ya kuwasadia watu wanaokabiliwa na
ugonjwa huo.
Nae Wahida Walid aliwataka wafanyabiashara na
watu wote nchini kujitokeza kuchangia kwa hiari, ili kufanikisha juhudi za
kuwasaidia watu wanaoguwa ugonjwa huo.
Alisema
harambee hiyo, ambapo baadhi ya wasanii mashuhri watashiriki kwa lengo la kutia
hamasa, imepata baraka zote za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mapema
Mbunifu wa mavazi Kurwa Mkwendule, alisema katika onyesho hilo wanamitindo
maarufu an wanaochipukia kutoka Tanzania na Bara na Zanzibar, watashiriki,
sambamba na wasanii, akiwemo Khadija Koppa, Jaffar Bhai na Wastara.
No comments:
Post a Comment