WASIOKUWA NA URAIA WA NCHI YOTE YOTE
NAO WAJADILIWE-TANZANIA
Na Mwandishi Maalum, New York
Tanzania imeitaka jumuiya ya kimataifa kujadili
tatizo la uwepo wa watu
ambao si raia wa nchi yoyote ile.
Pendekezo hilo limetolewa siku
ya Jumanne na Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga ( Mb) katika
mkutano wa Kilele wa
viongozi kuhusu wakimbizi.
Mkutano huo uliandaliwa na Rais wa Marekani Barack Obama kwa
ubia na nchi za Ethiopia, Jordan,
Mexico, Sweden, Canada na Ujerumani ambapo nchi
60 zilialikwa,45 kati ya
zilizoalikwa ikiwamo Tanzania zilitoa ahadi ya namna moja ama nyingine.
Nchi hizo ni zile ambazo kwa namna moja ama
nyingine zimekuwa zikiwapokea na
kuwahifadhi wakimbizi, zimekuwa nchi za
mpito kwa wakimbizi, au zimekuwa zikitoa
misaada ikiwamo ya hali na mali pamoja na kuwapatia uraia, ajira
na misaada ya kibinadamu.
Lengo kuu la mkutano huo wa
viongozi kuhusu wakimbizi lilikuwa ni kwa nchi kutoa ahadi mpya
ambazo kwayo zitasaidia katika kuwapatia fursa za ziada wakimbizi ili
pamoja na mambo mengine kuwapunguzia changamoto zinazowakabili na
kuwafanya wajisikie na kujiona kuwa nao ni binadamua kama
binadamu wengine.
Akizungumza kwa niaba ya Serikali, Waziri Mahiga, amesema, Tanzania kutokana na jiografia ya nchi hiyo ilivyo imejikuta mara kwa mara ikiwa ni kimbilio la wakimbizi kutoka nchi jirani.
Akawaeleza washiriki wa mkutano huo, kwamba, suala
la Tanzania kuwahifadhi
wakimbizi ni la kihistoria na
halikuanza jana au juzi.
“ Tanzania kutokana na jiografia
yake imejikuta ikiwa ni kimbilio wa watu
wanaotafuta salama ya maisha yao. Tumekuwa
tukiwapokea na kuwahifadhi wakimbizi
tangu miaka ya 60. Na tunatekeleza
jukumu hilo kwa kuzingatia
sheria za kimataifa na mikataba ya
kimataifa, na sheria zetu za ndani” akasema Mahiga.
Na kuongeza kwamba, Tanzania itaendelea na
jukumu hilo pale itakapopashwa
kufanya hivyo kwa kufuata na kuzingatia sheria za nchi na
sheria za kimataifa.
“Tumekuwa tukitiliza mkazo na kujadili mara kwa
mara tatizo la wakimbizi na changamoto wanazokabiliana nazo. Na mshukuru
Rais Obama kwa kuitisha mkutano huu. Lakini
kuna jambo jingine muhimu na ambalo
tunatakiwa tulijadili pia . Na hili linahusu uwepo na kuendelea kuongeza wa
idadi ya watu hususani vijana ambao hawana uraia wa nchi yoyote ile ( stateless people).
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akielezea zaidi kuhusu changamoto hiyo ya uwepo wa watu ambao hawana uraia wa nchi yoyote ile.
Amesema tatizo hilo linaonekana zaidi katika eneo la Kusini
na Eneo la Maziwa Makuu.
“ Tunapo jadili namna ya
kuwasaidia wakimbizi, ni vema pia
tukatambua kwamba kuna tatizo kubwa la uwepo wa watu ambao hawajasajiliwa na hawana
uraia wa nchi yoyote. Na tatizo hili ni kubwa na linazindi kuongezeka na lipo zaidi kwa
kizazi cha sasa, hawana uraia.
Tunatakiwa kulijadili tatizo hili”. Akasisitiza Waziri Mahiga.
Na kubainisha kuwa Tanzania, ikiwa ni mwanachana wa
SADC na EAC itaangalia
uwezekano wakuipekea mezani
ajenda hiyo kupita Taasisi hizo
mbili.
Kwa pande wa ahadi za ama nini
zaidi Tanzania itawafanyia wakimbizi , Waziri amesema pamoja na
ahadi ya kuendelea kuwapokea wakimbizi pale inapobidi kufanya hivyo,
Tanzania pia kupitia sheria zake itawasaidia watoto wakimbizi kupata huduma za jamii zikiwamo za elimu na afya, na kwa
wakubwa fursa za kujiajili hususani
katika sekta ya kilimo iliwe waweze kuzalisha
chakula na kujiajili kupitia kilimo.
Ahadi nyingine ni pamoja na kutowarudisha kwa nguvu wakimbizi katika nchi walizotoka.
Katika mkutano huo ambazo uongozi
wa Juu wa Serikali ya Obama
ulikuwapo kuanzia Makamu wake Joe Biden na Waziri wa Mambo ya
Nje John Kerry, Rais Obama kwa upande
wake alitoa ahadi za kuongeza idadi ya
wakimbizi watakaoingia nchini Marekani
pamoja na kuongeza misaada ya kifedha
kwaajili ya misaada na huduma za kijamii pamoja na kuzisaidia nchi zinazobeba
mzigo wa wakimbizi.
Barack Obama ambaye anaelekea ukingoni
mwa uongozi wake, amesema jumuiya ya kimataifa haipashwi kufanya kazi kwa
mazoea na hasa katika eneo hilo la
wakimbizi eneo ambalo anasema
linahitaji ushiriki na ushirikiano wa kila nchi bila ya kujali ukubwa au udogo wake,ajiri au umaskini wake.
Mkutano
huo mbali ya Marais, Wafalme,
Mawaziri Wakuu na Mawaziri kuzungumza
pia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa naye alizungumza pamoja nna Mkuu wa
Banki ya Dunia.
Ni mkutano ambao ulikuwa ni
mwendelezo wa majadiliano ambayo yalifanyika siku ya Jumatatu kuhusu ajenda ya wakimbizi na wahamiaji kama changamoto ya dunia hivi sasa.
Licha ya machafuko na vita, suala
ya umaskini, uongozi mbovu na watu
kutokuwa na matumaini ni maeneo ambayo
yameelezwa kuchangia katika uongezeko la wakimibizi.
Pamoja na kuandaa na kushiriki mkutano wa viongozi
kuhusu wakimbizi, Rais wa Marekani Barack Obama siku hiyo ya jumanne
alilihutubia kwa mara ya mwisho Baraza
Kuu la 71 la Umoja wa Mataifa, ambapo aliainisha masuala mbalimbali
yanayoikabili dunia hivi sasa yakiwamo
ya ugaidi, mabadiliko ya tabia nchi, ukiukwaji
wa haki za binadamu, ukiukwaji wa
utawala wa sheria na demokrasi, milipuko ya magonjwa kama vile Ebola na
Zika, matumizi ya diplomasia katika kutafutia ufumbuzi masuala
magumu likiwamo la mchakato wa kuidhibiti Iran dhidi ya silaha za
nyukilia.
No comments:
Post a Comment