Hassan
Khamis, Pemba
KIJANA
Saleh Iddi Ali (32) mkaazi wa Jadida Wete, ametupwa rumande kwa muda wiki mbili
baada ya kupandishwa katika kizimba cha mahakama ya Wilaya hiyo, akikabiliwa na
tuhuma za kupatikana na madawa ya kulevya.
Mwendesha mashtaka kutoka
Jeshi la Polisi Ali Ahmada alidai mahakamani hapo kuwa, Mei 27,mwaka huu majira
ya saa 2:30 asubuhi Mtemani mtuhumiwa alipatikana na kete 37 za unga unaosadikiwa
kuwa ni madawa ya kulevya aina ya “kokeni” zikiwa na uzito wa gramu 0.830 jambo
ambalo ni kosa kisheria.
Kupatikana na unga wa
madawa ya kulevya ni kosa kinyume na kifungu cha 16(1) (a) cha sheria namba 9
ya mwaka 2009 sheria ya kuzuia uingizaji na matumizi ya madawa ya kulevya
sheria ya Zanzibar.
Mara baada ya mtuhumiwa kupandishwa kizimbani hapo na
kusomewa shtaka lake mbele ya hakimi Makame Nyange, alitakiwa kutojibu
kitu chochote na alifahamishwa kuwa dhamana yake haipo wazi kwani shtaka lake lilipaswa kusikilizwa katika mahakama ya
Mkoa.
Alielezwa kuwa, kutokana
na dharura ya hakimu wa mahakama ya Mkoa ndio maana shtaka hilo lilisikilizwa
katika mahakama ya Wilaya.
Kutokana na mahakama
hiyo kutokua na uwezo kisheria kusikiliza shauri hilo, mtuhumiwa amepelekwa
rumande hadi Oktoba 10, mwaka huu ambapo kesi hiyo itatajwa katika mahakama ya
Mkoa wa kaskazini Pemba iliyopo Wete,
No comments:
Post a Comment