Hotuba ya Shukrani Iliyotolewa na Bwana.Brian Thomson –Mmiliki na Mkurugenzi wa Kampuni ya Pennyroyal (GIBRALTAR) Limited Zanzibar.
Katika Semina na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika Ukumbi wa Hoteli ya Ocean View - Chuini Zanzibar. 24 ktoba 2016
Mheshimiwa Spika wa Baraza la Wawakilishi, na Mwenyekiti wa
Mkutano Huu Muhimu.
Mheshimiwa Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi.
Waheshimiwa Mawaziri na Manaibu Mawaziri;
Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu;
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, Unguja
Mheshimiwa Mwenyekiti wa CCM Kaskazini, Unguja.
Wwaheshimiwa Sana Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ;
Washiriki Kutoka Taasisi za Serikali;
Waandishi wa Habari;
Mabibi na Mabwana;
Itifaki Imezingatiwa,
Mheshimiwa Mwenyekiti,
Mabibi na Mabwana,
Ni heshima
kubwa kwangu kupata fursa hii adhimu ya kutakiwa
kutoa neno la shukrani katika semina hii muhimu na ya kihistoria.
Kwa niaba ya Kampuni ya Pennyroyal (Gibraltar) Limited,
wafanyakazi wote, washiriki waliokusanyika katika ghafla hii na
kwa niaba yangu binafsi, napenda kutoa shukrani za dhati kwako
kwa kutumia muda wako adhimu na kuwa na sisi leo kwa ajili ya
kubadilishana mawazo na kutupa moyo wa kuendelea kutekeleza
azma yetu, tukiamini kuungwa mkono na wewe na Waheshimiwa
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
kutoa neno la shukrani katika semina hii muhimu na ya kihistoria.
Kwa niaba ya Kampuni ya Pennyroyal (Gibraltar) Limited,
wafanyakazi wote, washiriki waliokusanyika katika ghafla hii na
kwa niaba yangu binafsi, napenda kutoa shukrani za dhati kwako
kwa kutumia muda wako adhimu na kuwa na sisi leo kwa ajili ya
kubadilishana mawazo na kutupa moyo wa kuendelea kutekeleza
azma yetu, tukiamini kuungwa mkono na wewe na Waheshimiwa
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
Mabibi na Mabwana,
Sisi,
(Pennyroyal), tunamtambua na tunatoa
shukrani kwake
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein – Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kutuunga mkono,
kutupa ushauri, kutupa moyo na kutuongoza - jambo ambalo linatupa uhakika wa kufanikisha utekelezaji wa Mradi wa Amber Resort. Dira na hamu ya Mheshimiwa Rais ni kuiona Zanzibar kupitia mradi huu inapiga hatua kubwa na ya kipekee itakayoifanya Zanzibar kuwa kivutio kikubwa cha dunia cha utalii, lakini inayotambulika kimataifa na yenye kukabili ushindani.
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein – Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kutuunga mkono,
kutupa ushauri, kutupa moyo na kutuongoza - jambo ambalo linatupa uhakika wa kufanikisha utekelezaji wa Mradi wa Amber Resort. Dira na hamu ya Mheshimiwa Rais ni kuiona Zanzibar kupitia mradi huu inapiga hatua kubwa na ya kipekee itakayoifanya Zanzibar kuwa kivutio kikubwa cha dunia cha utalii, lakini inayotambulika kimataifa na yenye kukabili ushindani.
Mabibi na Mabwana,
Tuko hapa
leo kuonesha azma na malengo yetu kwa Serikali na
kwa Wazanzibari, kupitia nyinyi Waheshimiwa sana Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi, ambao mnawawakilisha jamii yote ya
Zanzibar kutoka kila eneo la visiwa hivi, kwamba Mradi wa
Amber Resort utachangia sana ukuaji wa uchumi wa Zanzibar na mabidiliko yake, lakini pia utachangia kubadilisha na kuleta maisha bora kwa jamii ya wengi. Kwa mnasaba huo na kwa umuhimu mkubwa mulionao, tunawaomba Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kusikiliza kwa makini mawasilisho yetu, baadae mutoe maoni na fikra zenu na muulize maswali, lakini mwisho wa siku, nyinyi kama wadau wetu, tunakuombeni muwe Mabalozi wa Pennyroyal kwa umma wa Zanzibar, kutoa uelewa na kuunga mkono azma hii ili iweze kufanikiwa utekelezaji wake kwa manufaa ya Visiwa hivi.
kwa Wazanzibari, kupitia nyinyi Waheshimiwa sana Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi, ambao mnawawakilisha jamii yote ya
Zanzibar kutoka kila eneo la visiwa hivi, kwamba Mradi wa
Amber Resort utachangia sana ukuaji wa uchumi wa Zanzibar na mabidiliko yake, lakini pia utachangia kubadilisha na kuleta maisha bora kwa jamii ya wengi. Kwa mnasaba huo na kwa umuhimu mkubwa mulionao, tunawaomba Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kusikiliza kwa makini mawasilisho yetu, baadae mutoe maoni na fikra zenu na muulize maswali, lakini mwisho wa siku, nyinyi kama wadau wetu, tunakuombeni muwe Mabalozi wa Pennyroyal kwa umma wa Zanzibar, kutoa uelewa na kuunga mkono azma hii ili iweze kufanikiwa utekelezaji wake kwa manufaa ya Visiwa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti,
Mabibi na Mabwana,
Kabla ya
kumaliza hotuba hii fupi, niruhusu nichukue fursa hii
adhimu kuitambulisha timu ya Pennyroyal niliyokuja nayo leo hii,
ambayo imekuwa ikifanya kazi kubwa sana kwa mradi huu, na
kuhakikisha inatimiza ndoto na hamu yetu hapa Zanzibar. Leo
nimekuja na timu na, naomba niwataje kama ifuatavyo:-
adhimu kuitambulisha timu ya Pennyroyal niliyokuja nayo leo hii,
ambayo imekuwa ikifanya kazi kubwa sana kwa mradi huu, na
kuhakikisha inatimiza ndoto na hamu yetu hapa Zanzibar. Leo
nimekuja na timu na, naomba niwataje kama ifuatavyo:-
1.
TIA EGGLESTONE
2.
MOHAMMED ISSA KHATIB
3.
GASPER NYIKA
4.
BOBBY MCKENNA
5.
SALEH MOHAMED
SAID
Mwisho,
lakini si kwa umuhimu wake, naomba kutambua ushiriki
na kazi kubwa iliyofanywa na Mheshimiwa Spika na Ofisi yake,
kwa maandalizi mazuri yaliyofanikisha shughuli yetu hii. Kwa
niaba ya Pennyroyal na timu nzima na kwa niaba yangu binafsi,
napenda kuchukua fursa hii kuweka katika kumbukumbu shukrani
za dhati kwako Mheshimiwa Spika na Ofisi yako kwa kuunga
mkono juhudi zetu. Tunawashukuru sana.
na kazi kubwa iliyofanywa na Mheshimiwa Spika na Ofisi yake,
kwa maandalizi mazuri yaliyofanikisha shughuli yetu hii. Kwa
niaba ya Pennyroyal na timu nzima na kwa niaba yangu binafsi,
napenda kuchukua fursa hii kuweka katika kumbukumbu shukrani
za dhati kwako Mheshimiwa Spika na Ofisi yako kwa kuunga
mkono juhudi zetu. Tunawashukuru sana.
Ahsanteni
nyote kwa kunisikiliza.
No comments:
Post a Comment