Habari za Punde

Kongamano la wazee wenye umri wa miaka 70 na kuendelea lafanyika Micheweni Pemba

 
Wazee wa mabaraza ya shehia ya Wilaya ya Micheweni ya mfuko wa  pensheni wakishiriki kongamano la siku moja katika shamra shamra za kuazimisha siku ya wazee duniani zilizofanyika katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari Micheweni Pemba.
 Dkt. Issa Ahmada Mselem akiwashauri wazazi kutumia huduma za afya kwa mujibu wa maelekezo ya madaktari na kwenda hospitali kwa mujibu wa ratiba wazipangiwa kuimarisha afya zao katika kongamano la siku moja la maadhimisho ya siku ya wazee duniani huko Micheweni Pemba.
 Nd Salmin Sheha Haji Mrajisi wa vizazi na vifo akifungua kongamano la siku moja la wazee wenye umri wa miaka zaidi ya 70 na kuendelea katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Micheweni tarehe 30/09/2016  wa mwisho (kulia) ni Afisa wa Pensheni Jamii kutoka Wizara ya kazi Zanzibar.
 Mrajisi wa vizazi na vifo wilaya ya Micheweni akiwasihi wazee wenye umri zaidi ya 70 na kuendelea kwenda hospitali kupima afya zao na kufuata kanuni za afya bora na wafahamu kuwa uzee pekee ni ugonja na kuwataka wafanye mazoezi kila siku katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari Micheweni Pemba.
Afisa kutoka wizara ya kazi akiwatanabahisha viongozi wa mabaraza ya pensheni ya wilaya ya Micheweni kufikiria afya zao, umoja na maelewano na kuanzisha miradi midogo midogo itakayowasaidia kupunguza ukali wa umaskini katika kongamano la siku ya wazee duniani wilayani humo.

Picha zote na Hamad Shapandu Mwinyi, Pemba

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.