Na salmin Juma -Pemba
Naibu waziri wa ujenzi mawasiliano na usafirishaji Mhe.Mohamed Ahmada Salum amesema nia ya Serekali ya Mapindunzi ya Zanzibar chini ya uongozi mahiri wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein ni kuwapelekea maendeleo wananchi wake bila ya upendeleo wala kuangalia itikadi za wananchi wake.
Ameyasema hayo wakati wa ziara zake ya kukagua barabara za ndani ikiwemo barabara ya Kichangani jimbo la wawi pamoja na barabara ya Wesha hadi mkumbuu ilioko jimbo la ziwani.
Amesema kuwa serekali inafahamu kiu ya wananchi ya kutaka kuwa nahuduma bora za barabara lakini kutokana na hali ya uchumi barabara hizo zitafanyiwa matengenezo awamu kwa awamu.
Aidha amewataka wananchi kuiunga mkono serekali kwa jitihada kubwa inayofanya kwa wananchi wake ya kutaka kuwaletea maendeleo kwa wananchi wote.
Nae mwakilishi wa jimbo la Ziwani Suleiman Makame amepogeza juhudi zinazochukuliwa na Mh Naibu Waziri kwa kufuatilia kero za wananchi na kutafuta njia mbadala zinazoweza kutatua kero hizo.
Kwa upande wa wananchi wameahidi kutowa ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha lengola serekali lakuwaletea maendeleo.
No comments:
Post a Comment