Habari za Punde

Serikali itaendelea kuviunga mkono vikundi vya ushirika

Na Salmin Juma, Pemba

Mkuu wa Wilaya ya Chake –chake,  Salama Mbarouk Khatib amesema Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi  zinazofanywa na vikundi vya  wajasiriamali kwa lengo la kuwainua kiuchumi wajasiriamali hao .

Amesema serikali imeandaa sera na mikakati ya kuwapatia  mikopo isiyo na riba katika  kuwarahisishia  kuboresha bidhaa zao na kupata nafasi nzuri ya kukopa na kurudisha kwa wakati .

Ameyasema hayo huko Ukumbi wa uwanja wa Gombani alipokuwa akifunga mafunzo ya siku moja ya taaluma ya matumizi bora ya mikopo kwa wajasiriamali waliokwishajaza fomu za mikopo ya bishara zao.

Akitoa maelezo ya kufanyika kwa mafunzo hayo kaimu Mratibu wa Idara ya Mikopo , wizara ya wanawake na watoto Pemba Haji Khamis Haji amesema lengo  ni kuwajengea uwezo katika kuitumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa na kuepuka kupata hasara katika shughuli zao.

Naye afisa mikopo kutoka Idara ya mikopo wizara ya wanawake na watoto Shuwena Hamad Ali amesema ili wajasiriamali waweze kufanikiwa kibiashara lazima wayajuwe malengo makuu ya masoko ilikiwemo kuwatambua wateja wao na mahitaji ya soko katika  kupata faida

Nao baadhi ya wajasiriamali hao wameitaka serikali kutafuta wafadhili wengine watakaosaidia kupatikana kwa fedha zaidi zitakazoweza kupewa wahitaji wengine wa mikopo na kuondoa usumbufu wa kusubiri wengine warudishe na wengine wapewe .

Jumla ya shilingi milioni 76.6 zinatarajiwa kutolewa mkopo kwa vikundi 48 vya wajasiri amali waliojaza fomu na kufanyiwa uhakiki wa kupatiwa mikopo hiyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.