Na Salmin Juma kutoka Pemba
MZEE mmoja anayejulikana kwa jina la Saleh Ali Mbwana mwenye umri wa miaka 45 mkaazi wa Maziwang’ombe Wilaya ya Micheweni amefariki dunia baada ya kuzama baharini akiwa katika shughuli zake za uvuvi .
Akithibitisha kutokea kwa tokeo hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Kamishna Msaidizi Haji Khamis Haji amesema tukio hilo limetokea oktoba 20 mwaka huu majira ya saa saba za mchana katika bahari ya Maziwang’ombe .
Amesema kwamba kabla ya kifo chake , marehemu aliondoka nyumbani kwake kwenda baharini kuvua , na alifikutwa na mauti hayo katika bahari wakati akitekeleza shughuli zake za uvuvi.
Kufuatia kutokea kwa tukio hilo Kamanda Haji amewataka wananchi hususani wanaotoka maeneo ya ukanda wa bahari wanapokwenda kuvua au kulima mwani kufuatana na wenzao ili patakapo tokea hitilafu waweze kusaidiana
Akizungumza baada ya uchunguzi daktari dhamana wa hospitali ya Wilaya ya Micheweni Dk Rashid Daudi Mkasha amesema chanzo cha kifo chake kimesababishwa na kukosa hewa baada ya kukaa chini ya maji ya bahari kwa muda mrefu .
Mwili wa marehemu umekabidhiwa kwa ndugu na jamaa baada ya kufanyiwa uchunguzi na dk wa Serikali ambapo mazishi yake yalifanyika katika maburi ya Maziwang’ombe
No comments:
Post a Comment