STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 27.10.2016
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amezihakikishia Wizara za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kuwa juhudi zitaendelea kuchukuliwa katika upatikanaji wa fedha kwenye vifungu
vya matumizi ya Bajeti za Wizara hizo ili zifanye kazi kwa ufanisi zaidi.
Dk. Shein aliyasema ha
yo leo Ikulu mjini Zanzibar katika kikao maalum kati yake na uongozi wa Ofisi
ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, ilipowasilisha
Taarifa yake ya Utekelezaji wa Mpango Kazi
kwa kipindi cha Julai hadi Septemba katika Bajeti ya mwaka 2016-2017.
Katika maelezo yake, Dk.
Shein alisema kuwa hatua kubwa imefikiwa katika upatikanaji wa fedha kwa kila
Wizara katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutokana na mikakati maalum
iliyowekwa ambayo hatimae imeleta mafanikio makubwa.
Dk. Shein alisema kuwa
juhudi zilizochukuliwa na Serikali katika kuondoa matumizi yasio ya lazima
yakiwemo maposho, safari na mambo mengineyo zimesaidia kwa kiasi kikubwa na
ndio maana lengo litafikiwa la kuwaongezea hata mishahara wafanyakazi wa sekta
ya umma.
Aidha, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa uongozi
na watendaji wote wa Wizara hiyo kwa kuwasilisha vyema Mpango Kazi wao.
Mapema Kaimu Waziri wa
Wizara hiyo, Issa Haji Ussi Gavu akisoma
taarifa ya Mapango Kazi huo alisema kuwa
jukumu la msingi la Ofisi hiyo ni kusimamia masuala yanayohusu utawala wa
sheria na utumishi wa umma pamoja na kuimarisha upatikanaji bwa haki.
Aidha, Waziri Gavu
alisema kuwa Ofisi ina jukumu la kusimamia na kuratibu utekelezaji wa misingi
ya utawala bora katika taasisi za umma.
Kaimu Waziri huyo,
alisoma malengo ya Wizara hiyo, pamoja na madhumuni ya taarifa, utekelezaji
kifedha ambapo miongoni mwa malengo ya Wizara hiyo ni kusimamia utoaji na
upatikanaji wa haki, kukagua hesabu za serikali, kuwajengea uwezo watumishi wa
umma, kusimamia mali za Wakfu, kukusanya Zaka, Sadaka na Misaada ya kheri na
kuigawa kwa wanaostahiki pamoja na malengo mengineyo.
Mapema Katibu Mkuu
Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Abdulhamid Yahaya Mzee nae
alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa Wizara hiyo kwa uwasilishaji mzuri wa Mpango
Kazi wake.
Katika maelezo yake
Dk. Mzee alisema kuwa licha ya ukubwa wa Wizara hiyo lakini imeuweka vizuri
mpangilio na uwasilishwaji wa kazi hiyo huku akitoa wito kwa Wizara hiyo
kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi kwa kutambua kuwa Wizara hiyo ni kioo kwa
Wizara nyengine za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Nao uongozi wa Wizara
hiyo, ulitoa pongezi za pekee kwa Dk. Shein kwa kupatiwa fedha za kutosha katika
vifungu vya matumizi kwenye Bajeti yao pamoja na Bajeti za Wizara zote za
Serikali hatua ambayo imezidi kuwapa ari katika kutekeleza majukumu yao ya
kazi.
Uongozi huo
ulimuhakikishia Dk. Shein kuwa haotomuangusha na umeahidi kutekeleza vyema
majukumu yao na kusisitiza kuwa utaendelea kuchapa kazi ili kufikia malengo
yaliokusudiwa.
Nae Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo Asha Ali Abdulla alitumia fursa hiyo kusoma taarifa ya utekelezaji
wa mpango Kazi kwa robo ya kwanza ya Julai hadi Septemba mwaka 2016 pamoja na muhtasari wa upatikanaji wa
fedha kwa kipindi hicho kwa Taasisi zote
za Wizara hiyo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment