Habari za Punde

Wakulima 10 hatarini mashama yao kuvamiwa na bahari


Na Haji Nassor, Pemba

FAMILIA 10 zenye wastani wa watu 60, wanaolima bonde la Malindi shehia ya Kilindi wilaya ya Chakechake Pemba, huwenda wakakosa eneo la kilimo cha mpunga, kutokana na mashamba wanayolima, kuanza kuingia maji ya bahari, kwa watu wasiofahamika kuchota mchanga kwa muda miaka mitatu sasa.

Kutokana na kadhia hiyo, tayari wakulima watatu wameshayahama mashamba yao, na wengine saba hulazimika kufikia mashimo yatokanayo na uchotaji wa mchanga kila mwaka kabla ya kuanza kilimo hicho, jambo ambalo walisema halileta mavuno mazuri.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wakulima hao walisema maeneo hayo wanaendesha kilimo cha mpunga kwa zaidi ya miaka 30, ingawa katika miaka mitatu ya hivi karibuni, kumejitokeza watu wanaochota mchanga kwa ajili ya biashara.
Walisema wapo wanachota mchanga kutoka mjini Chakechake na wengine kijijini kwao, hali ambayo inatishia kukosa kilimo cha mpunga ndani ya bonde hilo, pia kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira.

Mkulima Jafar Othman Khamis, alisema wapo wenzao watatu wameshaachana na kilimo hicho, kutokana na mashamba yao kuvamiwa na maji ya bahari, na kuua mbegu yao ya mpunga.

“Kwakweli uchotaji mchanga ndani ya bonde hili la Malindi, umekuwa tatizo, maana maji ya bahari yanapanda juu, na kuhatarisha kilimo chetu cha mpunga’’, alifafanua.

Nae Jokha Seif Baki, alisema wameshafuatilia tatizo hilo kwa kamati ya maendeleo ya kijiji chao bila ya mafanikio, licha kuwepo kwa ushahidi juu ya uchotaji huo mchanga ndani ya bonde hilo.

“Tokea siku ya kwanza tulipogundua tatizo hili na kufanya doria, juu ya wizi wa mchanga ndani ya mashamba yetu, tulisambaaza taarifa kwa wanakijiji wenzetu, lakini walipuuza’’,alifafanua.
Kwa upande wao wakulima Ali Othman Khamis na Asaa Ali Omar, walisema baada ya kuona hali hiyo imekithiri, walitoa taarifa kwa uongozi wa shehia ili kudhibiti hali hiyo.

“Lakini sheha hakuonekana kulichukulia hatua za haraka tatizo letu, sasa sijua kwa sababu za kisiasa au wanaochota mchanga ni watu wake’’,walisema.

Sheha wa shehia ya Kilindi wilaya ya Chakechake Abuu Abrahaman Salim, alikiri kuwepo kwa kadhia hiyo, na amesema amechachukua hatua ya kupinga marufuku.

“Ni kweli wakulima hao walinifika na kunielezea tatizo la uchukuaji mchanga ndani ya mashamba yao, lakini nimeshapiga marufuku na wakimkamata anaechukua mchanga waniletee’’,alifafanua.

Hata hivyo sheha huyo alisema, lazima wananchi wajenge utamaduni wa kuyalinda maeneo yao na uharibifu na uchafuzi wa mazingira, unaofanywa.


Shehia ya Kilindi wilaya ya Chakechake, pamoja na kuwepo kwa tatizo la uchimbaji mchanga kiholela, lakini katika za hivi karibuni, kumeibuka ukataji miti kwa kasi kwa kutumia msumeno wa moto ‘chensoo’.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.