-Ngomeni, Mgelema nako dk Shein atoa maagizo
zijengewe
Na Haji Nassor, Pemba
LEO wanzibari wote, tuko
katika shamra shamra za maadhimisho ya miaka 53, ya Mapinduzi Zanzibar, ambayo
yalitukomboa.
Kila
mmoja ni shahidi aidha kwa kuona au kuosma kwenye vitabu, kuwa hatukuwa na
thamani kabla ya mwaka 1964.
Unyonge,
unyonyaji, adhabu ndio iliokuwa imetawala kwa wazalendo kupitia watawala wa
enzi hizo, kabla ya jemedari wetu wa Zanzibar marehemu Abeid Amani Karume
kutukomboa.
“Leo
wana wa nchi tuko katika uhuru, na tumeshajitawala sasa kila mmoja, ataishi kw
afuraha na faraja, maana wale wadhalimu tumeshawaondoa’’,alisema moja kati ya
hutuba zake.
Kabla
ya ujio huu wa uhuru miaka 53 iliopita, hakuna alieamini kwa wananchi wanaoishi
vijijini, kwamba iko siku hata gari ndogo itafika wanakoishi.
Kauli
hii kama ya mzaha hivi, lakini ni ukweli usiofichika baada ya wananchi wa
vijiji hivyo kupokea ahadi ya ujenzi wa barabara zao hawakuamini.
Mimi,
wewe na yule sasa unapotembelea barabara hizi sita za mkoa wa kusini Pemba, mbona
ni bora hata hapo katikati ya mji wa Pemba Chake Chake
Hujafika
wewe….. pamejaa mashimo, misingi inayotishia ajali, lakini tutafanyaje ndio mji
wetu.
Sasa
leo hii tukiwa tunaelekea kushereheke kuadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya
Zanzibar, kwa wananchi wanaoishi vijiji hivyo ikiwa ni pamoja na Kangani,
Kengeja, Pujini na Wambaa, Tundauwa wako burudani.
Huwezi
amini kwamba tokea tulipojinasua na makucha ya wakoloni mwaka 1964, barabara
hizi takriban sita zilikuwa katika mashaka na tabu kubwa ya usafiri, lakini
miaka hii 53 sasa tunasema hongera Mapinduzi.
Ni
ukweli usiofichika kwamba, vijiji kadhaa vya Kisiwani Pemba vilikua
vimeasahauliwa juu ya kufikishiwa huduma ya mawasiliano ya barabara .
Hakuna
asieju kuwa lengo hasa la baba wa taifa hili la Zanzibar jemedari Abeid Aman
Karume, ni kuhakikisha kila mmoja anafaidi matunda ya Mapinduzi.
‘’Leo
wananchi wa Zanzibar, muko huru na sasa ni wakati wetu kujitawala, na udhalimu
na udhalilishaji sasa basi, mmesikiaaa…. ndiooooo……..’’, ni miongoni mwa kauli
zake.
Wakati huu tukiwa kwenye wiki ya miaka 53 ya
Mapinduzi ya Zanzibar, sasa wananchi hawa, wametulia tuli na wanaendelea
kuimarisha uchumi wao kama ilivyokua azma na lengo Mapinduzi.
Miaka
hii 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, iko tofauti na miaka 48 iliopita, maana hatua
hii ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara hizi sita, tena kwa kiwnago cha lami,
kumeondoa utabaka baina ya mjini na vijijini.
‘’Barabara
ndio hazina…….. barabara ndio uti wa mgongo wa taifa lolote lile…………barabara
ndio kiunganishi’’, ni kauli ya rais wa awamu hii ya saba dk Ali Mohamed Shein,
alioitoa wakati wa ufunguzi wa barabara hizo.
Wakati
huu tukiadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanziabr, ni kweli jemedari wetu
mzee Abeid Amani Karume, hatunae tena, lakini fikra, mawazo na busara zake ndio
hayo yanayotumiwa na viongozi waliopo madarakani kipindi hiki.
Ili
kuthibitisha haya….. tembelea vijiji hivyo uone barabara za kiwnago cha lami,
zilivyotandazwa na wananchi kupata faraja ya kuendeleza kazi zao za kujiletea
maendeleo.
Kwa
vile ahadi ni deni, ndio maana Serikali yetu iliopo madarakani kwa kuunganisha
na nguvu za wananchi, ikaanza kuzinduka kwa mwendo wa haraka, ujenzi wa
barabara za vijijini Mkoa wa Kusini Pemba.
Hili
kwa wale waliofika Pemba kwenye miaka hii miwili ya karibuni wanaweza kuwa
mashahidi, maana kwa sasa ni takriban asilimia 90 ya vijiji vya Pemba, sasa vinabarababara
za uhakika na za kudumu, zinazoteleza kama mgongo wa ngisi.
Hili
kwa haraka sana, si rahisi kuliamini hasa kwa wenzetu walioko nje ya Kisiwa cha
Pemba, hasa kutokana na kutolewa ahadi zisizotekelezwa na za muda mrefu juu ya
ujenzi wa barabara za ndani.
Kama
ukweli ni sumu, basi kila anaesoma makala haya unaweza kumdhuru, maana leo hii
tukiadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, barabara kadhaa za vijijini
kuna mtelezo wa hali juu kutokana na barabara kung’ara.
Serikali
hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, iliovuliwa kutoka makuchani mwa wakoloni, kwa
kushirikiana na washirika wake wa maendeleo, ambao ni Serikali ya Norway,
imejenga barabara sita.
Hizi
zilijengwa kwa pamoja na hata baadhi ya wanasiasa kushindwa kuamini, kama
Serikali hii ingeweza, kama ilivyoahidi kwa wananchi.
Kwa
hakika keki ya taifa hili la Zanzibar, sasa imeanza kuliwa, na kila miaka
ikisonga, ndio kila mmoja anapata kwa mujibu wa tumbo lake, hapa nazungumzia
maendeleo.
“Faida
ya Mapinduzi ya mwaka 1964, sasa hakuna asieiona, maana leo hii tukizifungua
barabara hizi kila mmoja atazitumia bila ya kujali chama, dini, rangi, wala mtu
eneo analotoka’’, alisema dk Shein eneo la Kengeja kwenye ufunguzi wa barabara
hizi.
Ujenzi
wa barabara zote hizo, naamini ni zile ambazo wakaazi wake walikuwa wameshakata
tamaa, kwamba hazitojengwa tena maana walikuwa wameshaahidiwa kwa muda mrefu
bila ya mafanikio.
Miongoni
mwa barabara zilizoingia kwenye mkumbo wa huo wa ujenzi ni pamoja na barabara
ya Mtambile –Kangani yenye urefu wa kilomita 6.2 ambayo kwa sasa haina shaka
tena juu ya usafiri wake.
Said
Omar Juma (50), yeye ni mkaazi wa kijiji hicho, wakati akizungumza na ukurasa
huu, alikua haamini hadi walipoona vitendea kazi vya Wizara ya Miundombinu na
Mawasiliano vikiaza kukata milima na miti.
“Umri
wangu sio mdogo hapa Kangani, na nikikumbuka ahadi zilizokua zikitolewa na
viongozi hata wa majimbo, si kuamini sana wakati nilipoona magari ya
Mawasiliano yakianza pilika pilika za ujenzi nilidhani tu kuondoa
njiani’’,alieleza.
Kama
hayo ni wananchi wa Kangani na barabara yao, ndani ya miaka hii 53 ya mapinduzi, furaha
nyengine iko kwa wananchi wa Mtambile – Kengeja - Mwambe yenye urefu wa
kilomita 9, ambao nao hasa walikua ndio wa mwanzo kukata tamaa.
Maana
wenyewe walitarajia kuwa barabara yao iwe imeshajengwa tokea utawala wa rais wa
mwanzo wa Zanzibar, hayati Abeid Aman Karume, kutokana na mji wao kuwa makao
makuu wa Wilaya ya Mkoani enzi hizo.
Ismaili
Haji Mcha (49), alisema tokea akiwa mdogo, akisikia taarifa za kujengwa
barabara yao kwa kiwango cha lami, lakini lililokuwa likijitokeza ni
kutengenezwa kwa kiwango cha kifusi pekee.
“Naamini
kwa watu wenye umri kama wangu, hakuna hata mmoja aliekua akiamini kwamba
barabara yetu wakati tukiadhimisha miaka 53 hapa Zanzibar itakua imeshajengwa
kwa kiwango cha lami’’,alieleza.
Usafiri
wakati kabla ya kuadhimisha miaka 53, kwa vijiji vyote hivyo, kulikua na gari
moja inayoondoka kijijini huko mjini mapema asubuhi na kurudi mchana.
Leo
hii tukielekea miaka hii 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, wakati suala la
miundombinu ya usafiri ukiwa umeimarika, ndio chachu ya maendeleo, ikiwa ndio
azma ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.
Wananchi wa shehia za Wambaa na Chumbageni
Wilaya ya Mkoani, nao wamepitiwa na mwangaza wa Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka
1964, kwa kujengewa barabara yao tena kwa kiwango cha lami.
‘Sisi
ilikuwa mgonjwa atiwe kwenye gunia hadi barabara kuu kwa kupelekwa hospitali
kutokana na barabara yetu kuwa mbovu na yenye mashimo makubwa’’,alisema Amin
Haji Makame.
Alisema
kua miaka ya 2000 akiwa kwenye kamati ya maendelo ya Shehia ya Wambaa alifika
mahala wakavunja kamati kutokana na kushindwa kuamini waliokua wakiaambiwa juu
ya ujenzi wa babarabara yao.
“Tulifika
mahala siku moja kuivunja kwa muda mrefu kamati yetu, maana walikua wakija
viongozi wanatueleza juu ya ujenzi wa barabara yetu nasi tunawapowaleza
wananchi wanashindwa kutuamini’’,aliongeza Amini Haji.
Akizungumza
bila wasiwasi alisema sasa tukiwa katika maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi
ya Zanzibar hata gari ndogo aina ya ‘MarkII’’inafika Wambaa bila ya tabu.
Haya
yote unapoyaangalia ndio sasa unaona kwamba Kisiwa cha Pemba hasa Mkoa wa
Kusini, kuna utekelezaji mkubwa wa ahadi za ujenzi wabarabara za vijijini na
ile azma ya Mapinduzi ya mwaka 1964 kwa upande wa huduma ya barabara.
Barabara
hii ya Mizingani –Wambaa ambayo ina urefu wa kilomita zaidi ya 9, na kwa sasa
imekamilika kwa kiwango cha lami na kuruhusu kutumika wakati wowote.
Kama
ilivyo barabara nyengine, nayo hii imewapunguzia joto na usumbufu wananchi na
wanfanyabiashara wa vijiji hivyo, kutokana na kupata fursa ya kusafirisha mazo
na wao wenyewe kwa utulivu.
Matunda
ya Mapinduzi ya Zanzibara ya mwaka 1964 pia yakabisha hodi kwenye barabara ya
Kenya- Chambani ikiwa ni miongoni mwa barabara zipazo sita Mkoa wa Kusini Pemba
ambazo imeingia kwenye mkumbo wa ujenzi wa kiwango cha lami.
Eneo
la Chambani hapo awali lilikua likitajwa sana kama ni sehemu mojawapo ambayo
hata barabara yake kwa kipindi cha jua, ilikua na usumbufu mkubwa kupitika.
Idrisa
Juma Khamis (49), alisema kwa mara ya kwanza aliposikia kuhusu ujenzi wa
barabra hiyo alijua hiyo ni sehemu ya kampeni.
‘’Unajua
tokea zamani nilikuwa nasikia kwamba barabara yetu inataka kujengwa lakini
sikuamini, ili sasa mambo ‘bomba’ inapitika vizuri’’,alisema akiwa juu ya
baiskeli yake.
‘’Sisi
ilikua ikifika hekaheka za kampeni basi utasikia tu viongozi hata wa majimbo
‘mkitupa kura tutahakikisha barabara yenu hii inajwengwa kwa kiwango cha lami’,
na baada ya muda inafukiwa mashimo tu’’, alifafanua.
Barabara
ya Chanjamjawiri – Tundaua kwa sasa nako kuna mtelezo wa haja na mg’aro wa
lami, na kuwafanya wananchi wa vijiji vya Misooni, Kungeeni, Tundaua, Kilindi
kufaidika na barabara hiyo.
Juzi
rais wa awamu hii ya saba ndani ya miaka 53 ya Mapinduzi Zanzibar, dk Ali
Mohamed Shein, ameshatoa agizo kwa wizara husika ya ujenzi wa barabara, kwamba
barabara za Ngomeni na Mgelema nazo zijengwe.
“Hadi
ikifika mwakani tukiadhimisha miaka 54 ya Mapinduzi Zanzibar, wananchi
wanaotumia barabara hizi nao wafaidike na matunda kwa kujengewa haraka abarabara
kwa kiwnago cha lami’’,alifafanua.
Dk
Shein ametoa agizo hilo hivi karibuni, wakati alipozitembelea barabara hizo,
kwenye ziara yake ya siku nne kisiwani, Pemba.
Haya
ndio matunda ya Mapinduzi ya Zanzbar na nasema Mapinduziii….diamaaa hasa kwa
vile maana yake ni maendeleo kwa wote.
No comments:
Post a Comment