Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) na Mkurugenzi wa huduma za Hospitali Mohamed Dahoma na Viongozi wengine wakiwa katika chumba cha uchunguzi wa matatizo ya uti wa mgongo baada ya kuizindua rasmi Hospitali ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba leo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt.Juma Malik Akil wakifuatana na Viongozi wengine wakati alipotembelea Hospitali ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kuizindua rasmi leo (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe, Mwanajuma Majid hospitali hii imejengwa na Kampuni ya Kichina Jiang SU Ltd,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kutembelea sehemu mbali mbali za Hospitali ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kuizindua rasmi leo (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe, Mwanajuma Majid hospitali hii imejengwa na Kampuni ya Kichina Jiang SU Ltd.
Katibu Mkuu
Wizara ya Afya Zanzibar dk Juma Malik Akil, akizungumza kwenye ufunguzi wa jengo jipya la hospitali
ya Mkoa ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, ambalo limejengwa upya, na baadhi ya
majengo yake kufanyiwa ukarabati mkubwa, na serikali ya amhuri ya watu wa
China, ambayo imefunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein
Balozi wa China nchini Tanzania, Lv You Qing
akieleza namna ya ushirikiano ulivyo baina ya nchi yake na Tanzania
–kwenye ufunguzi wa jengo jipya la Hospitali ya Mkoa ya Abdall Mzee Mkoani
Pemba, ambayo imefanyiwa ukarabati mkubwa na baadhi ya majengo kujengwa upya na
serikali ya watu wa China
Waziri wa Afya
Zanzibar Mahamuod Thabiti Kombo, akizungumza kwenye ufunguzi wa jengo jipya na
la kisasa la hospitali ya Mkoa ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, ambayo, imejengwa
na kufanyiwa ukarabati mkubwa na serikali ya watu wa China
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi
Afisa Mdhamini wa wizara ya Afya Pemba, Bakar Ali Bakar picha maalumu ya
muasisi wa Hospitali ya Abdalla Mzee,
bwana Abdalla Mzee, kwenye hafla ya kuifungau hospitali hiyo, ambayo imejengwa
na kufanyiwa matengenezo makubwa na na serikali ya watu wa China
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi dk Ali Mohamed Shein, akimkabidhi
zawadi maalum Balozi wa Chini nchini Tanzania Lv You Qing kutambua mchango wao,
katika sekta ya afya, hafla hiyo
ilifanyika kwenye ufunguzi wa hospitali ya Mkoa wa Abdalla Mzee Mkoani Pemba, ambayo
imejengwa na kufanyiwa matengenezo makubwa na na serikali ya watu wa China
Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akizungumza
na mamia ya wananchi wa Pemba, baada ya kulifungua jengo jipya na la kisasa la
hospital ya Mkoa ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, baada ya kujengwa upya na
kufanyiwa matengenezo makubwa na serikali ya watu wa China.
, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
No comments:
Post a Comment