Mchezaji wa zamani wa timu ya Tamasha, Timu ya Taifa ya Zanzibar na Taifa Stars kutoka Pemba , Ali Khamis Mtumweni
WA mwanzo kulia
waliosimama Ali Khamis Mtumweni akiwa na
kikosi chake cha timu ya Tamasha mnamo mwaka 1976 kwenye uwanja wa Mjimbini
Mkoani, kwenuye mchezo wa kirafiki na timu ya Chipukizi ya Chake chake (picha na hisani ya Fuom Haji machezaji wa
Tamasha )
Na
Hamad Hassan, OUT
‘’UTITIRI
wa vilabu haukuzi soka bali washusha soka la Zanzibar’’ ni kauli ya ya aliekuwa
kinara wa soka miaka iliopita.
Kauli hiyo iliotolewa
na mchezaji alievuma miaka ya 80, na jina lake ambalo litachelewa kuvunja
rekodi la ‘Ali Khamis Mtumweni.
Mtumweni
alinishitumia hata mimi mwandishi wa makala haya, juu ya kauli yake kwamba
utitiri wa vilabu unachangia kuangusha soka la Zanzibar.
Hapo sasa
nililazimika kweka sawa kalamu yangu, na niliganda nae kutaka kujua ni kwa nini
uwepo wa vilabu vingi hakuinui soka?
Hakuwa na kigugumizi
kuelezea kwa upana juu ya kuwepo kwa vilabu vingi hasa katika kijiji kimoja na
walioanzisha wakidhani kuwa wanataka kunyanyua soka.
Mtumweni aliezaliwa
mwaka wa Mapinduzi ya Zanzibar, yaani mwaka 1964, hakusita kusema kuwa vilabu
vinapokuwa vingi kinachojitokeza ni ushindani usio na faida kwa taifa.
Kwa mfano katika
ukanda wa Wilaya ya Mkoani ambapo yeye anaishi, kuna vilabu zaidi ya sita
vinavyoshiriki lidi daraja la kwanza taifa Pemba.
Hakusita kutilia
nyama kauli yake kuwa, huku kukiwa hakuna hata klabu moja iliowahii kusonga mbele
na aalu kuwa mshidi wa soka la Zanzibar.
Kauli hiyo ya Ali
Khamis Mtumweni, ilikuwa ikiashiria kwamba hakuna umuhimu wa kuwa na vilabu
vingi hapa Zanzibara, kama kweli kuna nia ya kukuza soka.
‘’Mimi wakati
nakipiga na timu kali ya Tamasha ya Mkoani, ambayo iliwahi kutikisha sana
kulikuwa na timu mbili tu Mkoani mzima, ikiwa ni pamoja na Pindua lakini leo
du…..’’,alisema na kucheka.
Mtumweni ambae soka
lilimuzesha kumpa umaarufa na kisha kujenga nyumba ambayo anaishi huko
Mbuguwani Mkoani, hakusita kunieleza kwa upana historia yake ya soka.
Mtumweni alianza
kulipenda soka akiwa Skuli ya msingi ya Uweleni wakati huo mnamo mwaka 1972,
kabla ya kuingia Sekondari hapo hapo Uwelini miaka 10 baadae.
Alidokiza kuwa,
wakati akiwa Skuli hasa ya Sekondari waliweza kutamba sana akiwa anachezea
namba tisa ‘streak’ na kufanikiwa hata kutwaa uchampioni wa skuli za sekondari.
‘’Nyota yangua hasa
ilianzia nilipoingia Sekondari na ndipo hapo hasa mwalimu wa timu ya Tamasha,
aliponiona na kuanza kunifuatilia na nikafanikiwa kuanza kucheze nayo hata
kabla ya kumaliza skuli’’,alisema huku akiwa juu ya bao analozungumzia.
Mtumweni alianza
kutikisha wavu kwa kujipatia goli lake la kwanza kwenye mashindano maalum ya Skuli
katika miaka ya 80, pale alipoifunga goli pekee kwa timu yake ya Skuli ya
Uweleni.
Mchezo huo ambao
alisema ulianza kumpa umaarufu na kuwa gumzo hata skuli ni pale wakati skuli
yake ilipocheza na skuli jirani ya Ng’ombeni.
Hamu ya kupenda soka
iliendelea kumuingia kichwani na kuwa na hamu ya kuwa mchezaji wa timu ya taifa,
ambapo hilo alifanikiwa kama kula Papai kwa jiko.
Mwaka mmoja tu baada
ya kumaliza masomo yake ya sekondari, Mtumweni ndipo alipoanza rasmi kusakata
kabumbu, akikipiga na Tamasha iliokuwa na mastakimu yake Mkoani Pemba.
Kocha Yussuf Ramadhan,
ndio iliokuwa taa ya mwanadinga huyu, ambae alishalitumikia taifa kwa muda wa
takriba miaka kumi, hadi kufikia kustaafu soka.
‘’Nilipofika ndani ya
klabu hiyo, nilidhani sitoweza kucheza maana nilikutana na vijeba tena vya
wakati huo vikubwa na vinene’’,alieleza kwa bashasha.
Mtumweni mwenye umbo
la wastan na mrefu aliepanda juu , alisema kutokana na umbo lake sikudhani kuwa
ningeweza kuchuuana na vijeba ambavyo vyengine ni kaka zangu mara mbili i’’,alisema
.
Wakale walisema kuwa
ukubwa sio hoja, wala usione samaki mkubwa ukaogopa kuuliza bei ndivyo
ilivyokuwa kwa Mtumweni wakati alipobisha hodi kwenue klabu ya Tamasha.
Alivitaja vijeba alioanza nao kwenye timu hiyo kuwa ni
pamoja na Salim Kiburungu aliewahi kuwa muwamuzi wa soka, Hamza Ussi aliewahi
kuwa karani wa Mahakama, Foumu Haji nae pia aliwakuwa karani Mahakamani.
Wengine aliocheza nao
Mtumweni akiwa kwenye klabu kongwe ya Tamasha ni Salim Khamis, na Affan Othuman
aliewahi kuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa
ZFA Pemba na wengine aliowasahau.
Mtumweni alijingamba
kwamba wakati huo soka la Zanzibar lilikuwa juu na hata baadhi ya timu za nchi
za Afrika Mashariki na Kati kuiogopa Zanzibar kutokana na mambo kadhaa ikiwa ni
pamoja uchache wa vilabu.
Alivitaja vilabu
ambavyo wakati huo vilikuwepo kuwa ni pamoja na Wete Star, Tamasha ya Mkoani,
Pindua, Chipukizi, na kwa Unguja zikikuwepo kama vile Small Simba, KMKM, Mkoa
wa Mjini Magharibi.
Kimtazamo hapo utaanona
kuwa kauli ya Mtumweni, inaingia akilini kwamba uwepo wa vilabu vingi, kamwe
havisaidii kunyanyua soka hapa Zanzibar.
Mtumweni alidumu na timu ya Tamasha ya kwa muda wa miaka saba,
kuanzia mwaka 1986 ,kabla ya kujiunga na Mkoani Shootin katika miaka ya 1987
mara baada ya kusambaratika kwa timu ya Tamasha.
Timu ya Tamasha
katika uhai wake iliwahi kunyakua nafasi ya tatu kwenye ligi kuu ya Zanzibar, katika
mwaka 1983, huku Small simba ikiibuka na machampion na KMKM kushika anafasi ya
pili.
‘’Mwaka huo
nilijisikia mmbora na safi kwenye soka maana nilicheza mpira bila ya kuchoka na
kama si hujuma zilizofanywa, tulipaswa tuwe washindi wa pili’’,alieleza
Mtumweni.
Hata hivyo Mtumweni
alilalamikia kwa wakati huo kwa kosa udhamini hata kwenye ligi, jambo ambalo
kwa upande mmoja liliamsha ari kwa wachezaji.
‘’Suala la ufadhili
kwa enzi zetu, halikuwa likizungumzwa, na badala yake wachezaji walikuwa
wakijihudumia wenyewe na hata watu wenye uwezo ndio wafadhili’’,alifafanua.
Kwa kanre hii
mwanandinga huyu anashangaa kuona kwamba timu hasa ligi kuu ya Zanzibar, imekuwa
ikipata ufadhili japo mdogo, lakini hakuna kiwango cha soka kinachoonekana.
Hakuacha kurejea
kauli yake kuwa suala la utitiri wa vilabu, sio suluhisho la kukuza soka
Zanzibar, bali uwajibikaji na uzalendo ndio kinachozingatiwa kwa wachezaji.
‘‘Sisi enzi zetu
hatukuwa na njaa ya kuhama hama vilabu, maana tukiona ni usaliti kuacha kbalu
ya nyumbani na kuhamia klabu ya ugenini’’,alisema akiashiria kua suala la
kuhama vilabu sio zuri.
Mtumweni alizidi
kubainisha kuwa kwa sasa wachezaji kadhaa hawana uzalendo, mapenzi, nidhamu,
uwajibikaji kwenye vilabu kutokana na kuweka mbele suala la fedha.
Yeye anadhani suala la kwanza unapoingia kwenye
soka, mchezaji aelewe hakuna malipo yanayofanana na kazi hiyo, ni vyema tu
wachezaji wawajibike ili kuliletea heshima taifa lako.
Pamoja na kwamba
hakupata matatizo mengi alipokuwa kwenye ngarambe za soka, lakini anasema
alipata faida nyingi moja wapo ikiwa ni pamoja na kutembelea nchi kadhaa za
bara la Afrika.
Miongoni mwa nchi
alizozikanyaga mwanandinga huyo wakati akiwa na timu ya taifa ya Zanzibar ni
pamoja na Ethiopia, Oman, Kenya, Malawi ambapo pia aliwahi kucheza michezo
kadhaa ya kimataifa ikiwa ni pamoja na ya kirafiki.
Mchezaji huyo
aliekuwa kama kiraka, pia aliwahi kukipiga na timu ya taifa ya Tanzania mnamo
mwaka 1987, na akiwa na klabu hiyo anasema hatousahu mchezo baina ya Tanzania na
Algeria kwenye uwanja wa Arusha.
Mchezo huo kwa Ali
Khamis Mtumweni ambao walishindwa kutambiana na wageni wao hao, alijiona
kucheza kwa nguvu na maarifa makubwa tena bila ya kuchoka.
‘’Wakati huo nilikuwa
najisikia sana ninapokua na mashujaa wenzangu akina Abubakar Salim, Khalfan
Ngasa, Rajab Risasi, Othuman Jum, na kutoka Zanzibar walikuwepo wengi’’,aliwataja
haraka haraka.
Wakati huo hata
Zahoro Salim, Othuman Abdallah Foreman, Nassor Mwinyi Bwangwa nao walikutana na
Mtumweni kwenye kikosi kizito cha timu ya taifa ya Tanzania.
Ambapo hapo ndio hasa timu hiyo ilipokuwa ikivuma ambapo kwa wakati huo alikuwa mchezaji pekee kutoka Kisiwani Pemba.
Kinara huyo wa soka
alidai kuwa siku hipo waliowaliza wageni wao kutoka Msumbuji kwenye uwanja wa
Dodoma, kwani hadi dakika 88 walikuwa hatujafungana na dakika moja kabla ya
mchezo kumaliza kulipigwa shuti na mchezaji mmoja hadi wavuni.
Miaka michache baadae
Mtumweni alijunga na timu ya Jamhuri akiwa anachezea namba tisa, ingawa
hakuduma kwa muda mrefu na baadae kuamua kustaafu soka.
Kwa muda huu
mwanasoka huyo anasema hana hata klabu moja ya ndani ya nchi anayoishabikia
kutokana na soka bovu linaloonyeshwa na wachazaji ingawa wanaufadhili wa hata
vifaa.
Kuhusu watoto wake,
ikiwa kuna mmoja alau anaefuata nyayo zake alisema kati ya watoto wake 10,
hakuna hata mmoja ambae ameanza kujituma kwenye soka.
‘’Mimi hata mwanangu
mmoja hakuna anaenifuatia na wala sina klabu hata moja ninayoifundisha na nipo tu
na pirikapirika zangu za kuvua tu na kilimo’’,alisema huko nyumbani kwake
Mbuguwani Mkoani Pemba.
Hata hivyo alisema
aliwahi kutimuliwa kazini kutokana na soka, ingawa alipewa mafao yake wakati
alipokuwa akifanya kazi bandari ya Mkoani alipochukuliwa na kocha wake Ramadhan
Yussuf.
Hakuacha kuishauri
Serikali kupitia Wizara yake inayoshughulikia michezo kuwatambua wanamichezo wa
zamani na hasa walioliletea taifa hili heshima kwenye michezo mbali mbali.
‘’Kwa mfano kama mimi
hapa leo hii nikienda kwenye viwanja vya michezo lazima nilipe, lakini mchezaji
wa juzi anapita bure sasa ule mchango wa Serikali kwetu sisi uko
wapi’’,alihoji.
Mtumweni pia
aliwataka vijana wa leo kuacha kuchanganya mpira na uvutaji wa hata sigara,
iwapo wana nia ya kweli katika michezo na kuacha anasa ambazo zitawadhoofisha
afya zao.
Alimtaja mchezaji
Stevin Gerard wa klabu ya Liverpool kwamba ndio klabu na mchezaji pekee
ulimwenguni anaemmaliza moyoni mwake na kukosa usingizi wakati inapocheza.
Ali Khamis Mtumweni (58)
aliezaliwa Mbuguwani Mkoani Pemba, kwa sasa anaishi hapo hapo kwenye nyumba
yake ya kujenga kutokana na soka iliopo mkabala na bekari ya Mbuguani.
Alipata elimu yake ya
Quran katika chuo cha baba yake mzazi mzee Khamis Mtumweni na kuanza masomo yake
ya darasa la kwanza skuli ya Uweleni mwaka 1972 hadi mwaka 1982 na kumalizia
elimu ya sekondari.
Kwa sasa Mtumweni ni
mvuvi mkuu wa bahari ya hindi na anaendesha maisha yake kupitia rasilimali ya bahari, huku alilalamikia kutoenziwa kama mtu alieliletea heshima taifa la
Tanzania na Zanzibar.
No comments:
Post a Comment