NA HAJI NASSOR, PEMBA
KATIBU Mkuu wizara ya Nchi Afis ya Rais, Katiba, Sheria,
Utumishi wa na Utawala Bora Zanzibar Yakout Hassan Yakout amewaagiza watendaji
wa idara ya utumishi wa umma, kuhakikisha wanakuwa na kumbu kumbu sahihi za
wafanyakazi, ili kuepusha usumbufu pale wanapofikia hatua ya kustaafu.
Alisema
haipendezi na wala haingii akili, kuona mtumishi analitumikia taifa kwa miaka
kadhaa, kishaa anapostaafu iwe ni kazi kupatikana kumbu kumbu zake.
Katibu
huyo alieleza kuwa, lazima kila mmoja ndani ya wizara hiyo, awajibike ipasavyo
na hasa kwa wale wanaohifadhi kumbu kumbu za watumishi wa umma, ili anapomaliza
muda wake wa utumishi, isiwe kuhangaika huku na kule, kutafutiwa vielelezo
vyake.
Katibu
Mkuu huyo alieleza hayo, ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo kisiwani Pemba,
wakati alipokutana na watendaji wa wizara hiyo na wafanyakazi wengine, ili
kusalimiana nao, na kuwataka kuwajibika ipasavyo.
Alisema
jina la wizara hiyo limebeba bango la utumishi wa umma na utawala bora, hivyo
ni vyema wakaendena na kasi ya jina hilo, ili watumishi wanapomaliza
kulitumikia taifa lao, wapate haki yao kwa haraka.
“Mtu
anaefanyakazi kwa muda mrefu, na ikafika siku ya kustaafu anataka kupewa haki
zake, kisha afike wizarani aambiwe ngoja kwanza tutafute vielelezo vyako, kwa
kweli hatutomtendea haki’’,alifafanua.
Katika
kuhakikisha hilo linakuwa imara, Katibu Mkuu huyo Yakout Hassan Yakout alisema
wizara inaendelea na mpango wa kuweka kumbu kumbu za wafanyakazi ‘data base’
ili iwe rahisi kupatikana.
Akizungumzia
suala la nidhamu, aliwataka wafanyakazi hao kuhakikia wanaheshimiana, ili
wafanyekazi zao kwa utulivu, sambamba na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Mpaema
Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba Massoud Ali Mohamed, amemuhakikishia Katibu
Mkuu huyo, kuendelea kufanyakazi kwa moyo mmoja, licha ya changamoto
zinazowakabili.
Hata
hivyo amewataka wafanyakazi hao, kuendelea kusaidiana na kufanya kazi kwa
kushirikiana, ili kufanikisha malengo ya wizara hiyo.
Baadhi
ya wafanyakazi waliochangia kwenye mkutano, huo walisema wanayohamu na shauku
ya kufanyakazi kama wakipatiwa vifaa.
Nassor
Bakar, alisema suala la kuhifadhi kumbu kumbu za watumishi ni jambo jema,
ingawa linahitaji kupwatia vifaa vya kisasa.
Hata
hivyo wafanyakazi hao, wamempongeza Katibu Mkuu huyo kwa kufika kisiwani Pemba
kujitambulisha kwake, na kuahidi kushirikiana naye.
No comments:
Post a Comment