STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 29.06.2017
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amewatunuku nishani viongozi na
Wananchi mbalimbali ambao waliitumikia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika
Nyanja mbalimbali.
Ghafla hiyo ya utunuku wa nishani hizo ilifanyika ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na Wananchi.
Dk Shein alitoa nishani hizo kwa viongozi na wananchi 52 ikiwemo nishani ya Mapinduzi 12, ambayo hutunukiwa viongozi wenye sifa za kipekee, nishani ya utumishi uliotukuka 20 na nishani ya ushujaa 20.
Waliotunukiwa nishani ya Mapinduzi ambayo hutolewa kwa mtu ambaye alisisi au alishiriki au aliyatukuza na aliyeyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ambapo nishani hii hutunukiwa kwa makundi mawili likiwemo kundi la viongozi wenye sifa za kiepee ambao ni aliyekuwa Makamu wa rais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Omar Ali Juma na Marehemu Ali Muhsin Ali aliekuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi.
Wengine waliotunukiwa nishani ya Mapinduzi viongozi na wananchi wenye sifa maalum ni Pandu Ameri Kificho Spika mstaafu wa Baraza la Wawakilishi , Aboud Talib Aboud Mjumbe mstaafu wa baraza la Mapinduzi,Dk Msimu Abdulrahman Hassan,Mastura Ali Salim na Zainab Omar Mohamed.
Wengine waliotunukiwa nishani hiyo ni Thereza Olban Ali,Marehemu Makame Mzee Suleiman,Marehemu Isaac Abraham Sepetu,Marehemu Asha Bakari Makame na Marehem Hamid Vuai Mkungu.
Aidha, Dk Shei aliwatunuku nishani watumishi wa Serikali, Mahkama na Baraza la Wawakilishi ambao aliwatunuku nishani ya utumishi uliotukuka.
Watunukiwa hao ni Jaji Hamid Mahmoud Hamid, Mohammed Fakih Mohamed, Mohamed Ahmed Mohamed, Ali Rajab Juma, Mwanaidi Saleh Abdallah, Maoud Mohamed Ali Shambi, Mwapili Mohmoud Mzee, Josefrida Gloria Parwira na Marehemu Mohamed Jongo.
Akitoa tamko la kwanza katika shughuli hiyo ya kutunuku nishani katika ghafla hiyo Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum, alisema kuwa waliotunukiwa nishani hizo sifa zao zimekidhi matakwa ya nishani.
Ghafla hiyo ya utunuku wa nishani hizo ilifanyika ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na Wananchi.
Dk Shein alitoa nishani hizo kwa viongozi na wananchi 52 ikiwemo nishani ya Mapinduzi 12, ambayo hutunukiwa viongozi wenye sifa za kipekee, nishani ya utumishi uliotukuka 20 na nishani ya ushujaa 20.
Waliotunukiwa nishani ya Mapinduzi ambayo hutolewa kwa mtu ambaye alisisi au alishiriki au aliyatukuza na aliyeyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ambapo nishani hii hutunukiwa kwa makundi mawili likiwemo kundi la viongozi wenye sifa za kiepee ambao ni aliyekuwa Makamu wa rais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Omar Ali Juma na Marehemu Ali Muhsin Ali aliekuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi.
Wengine waliotunukiwa nishani ya Mapinduzi viongozi na wananchi wenye sifa maalum ni Pandu Ameri Kificho Spika mstaafu wa Baraza la Wawakilishi , Aboud Talib Aboud Mjumbe mstaafu wa baraza la Mapinduzi,Dk Msimu Abdulrahman Hassan,Mastura Ali Salim na Zainab Omar Mohamed.
Wengine waliotunukiwa nishani hiyo ni Thereza Olban Ali,Marehemu Makame Mzee Suleiman,Marehemu Isaac Abraham Sepetu,Marehemu Asha Bakari Makame na Marehem Hamid Vuai Mkungu.
Aidha, Dk Shei aliwatunuku nishani watumishi wa Serikali, Mahkama na Baraza la Wawakilishi ambao aliwatunuku nishani ya utumishi uliotukuka.
Watunukiwa hao ni Jaji Hamid Mahmoud Hamid, Mohammed Fakih Mohamed, Mohamed Ahmed Mohamed, Ali Rajab Juma, Mwanaidi Saleh Abdallah, Maoud Mohamed Ali Shambi, Mwapili Mohmoud Mzee, Josefrida Gloria Parwira na Marehemu Mohamed Jongo.
Akitoa tamko la kwanza katika shughuli hiyo ya kutunuku nishani katika ghafla hiyo Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum, alisema kuwa waliotunukiwa nishani hizo sifa zao zimekidhi matakwa ya nishani.
Alisema
kuwa kwa kutumia uwezo wake Rais Dk. Shein al;iopewa chini ya kifungu cha 4 cha
Sheria ya Mambo ya Rais namba 5 ya mwaka 1993, na ilivyotangazwa katika Tangazo
la Kisheria namba 67 kupitia Gazeti Rasmi la Serikali.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment