Habari za Punde

Dabi Ilikutana Mara Nyingi Duniani Ndani ya Msimu Mmoja ni Dabi ya Jangombe Kati ya Taifa ya Jangombe Wakombozi wa Ngambu na Jangombe Boys.

Na: Abubakar Khatib “Kisandu”, Zanzibar.

Dabi ya Jang’ombe kati ya Taifa ya Jang’ombe na Jang’ombe Boys ndio dabi inayoongoza kukutana mara nyingi msimu mmoja kuliko dabi zote Dunia nzima.

Msimu huu dabi hii mpaka sasa ishakutana mara 5 na kesho kutwa Jumapili ya July 30, 2017 watakutana tena kwa mara ya 6, hii haijawahi kutokea Dabi yoyote Duniani kukutana mara 6 ndani ya msimu mmoja.

Kila mji kuna kuwa na dabi mfano pale Jijini Dar es salam Kariakoo kuna dabi ya Kariakoo kati ya Simba na Yanga, au kule London Uengereza kuna dabi ya London kati ya Arsenal na Totenham Spurs, au kule Jijini Manchester Uengereza kuna dabi ya Manchester kati ya Manchester City na Machester United, au kule Spain kuna dabi ya Madrid kati ya Atletico Madrid na Real Madrid, lakini dabi zote hizo kwa msimu mmoja zinakutana mara 2, 3 au 4, ila kwa dabi ya Jang’ombe itakuwa imevunja rikodi dabi ya kwanza kukutana mara nyingi msimu mmoja.

Ndani ya msimu huu wa mwaka 2016-2017 ambao kwa Zanzibar bado unaendelea dabi hiyo walikutana Novemba 19, 2016 katika Bonanza la Coconut FM ambapo matokeo Taifa 2-0 Boys huku mabao ya Taifa yalifungwa na Mkongo Baraka Ushindi na Mkenya Mohd Said “Mess.

Disemba 10, 2016 walikutana tena kwenye Ligi kuu soka ya Zanzibar Mzunguko wa kwanza na mataokeo Taifa 2-2 Boys ambapo mabao ya Taifa siku hiyo alifunga Omar Yussuf Chande dakika 9 na Abdallah Mudhihir (Mido) dakika 60 wakati mabao ya Boys yote alifunga Khamis Mussa (Rais) dakika ya 45 na 53.
Disemba 30, 2016 pia walikutana tena kwenye Kombe la Mapinduzi 2017 na matokeo Taifa 1-0 Boys kwa bao pekee lililofungwa na Hassan Seif “Banda”.

Aprli 25, 2017 walikutana tena kwenye ligi kuu soka ya Zanzibar Mzunguko wa pili na matokeo Taifa 0-1 Boys kwa bao pekee limefungwa na Khamis Mussa “Rais”.
Mei 14, 2017 walikutana tena kwenye ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora Mzunguko wa kwanza na matokeo Taifa 0-3 Boys ambapo mabao ya Boys yalifungwa na Khamis Mussa “Rais”, Khatib Ng’ombe alijifunga mwenyewe na Juma Mess la tatu.

Jumapili ya July 30, 2017 saa 10:00 za jioni kwenye mzunguko wa pili ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora na huu utakuwa mchezo wao wa sita kukutana katika msimu mmoja.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.