Habari za Punde

Nafasi za kazi Mamlaka ya viwanja vya ndege Zanzibar

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar, ni taasisi ya Serikali  iliyoanzishwa kwa sheria namba 8 ya mwaka 2011. 

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege inatangaza nafasi za Kazi katika maeneo yaliyoainishwa hapo chini, kwa wazanzibar wenye sifa zinazohitajika.

1. OFISA USALAMA DARAJA LA I I (AVIATION SECURITY OFFICER GRADE II)  Nafasi 10  Unguja
Sifa ya kuingia kazini
Mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika fani ya Mifumo ya Kompyuta (IT) au Sheria au Sayansi ya Jamii au Utawala au Menejimemti ya Rasilimaliwatu  kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 

1. OFISA USALAMA MSAIDIZI DARAJA LA III (AVIATION SECURITY ASSISTANT OFFICER GRADE III) Nafasi 40 Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye Stashahada ya Mifumo ya Kompyuta (IT) au Sheria au Sayansi ya Jamii au Utawala au Menejimemti ya Rasilimaliwatu  kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 
2. MHANDISI MITAMBO (MECHANICAL ENGINEER) Nafasi 1  Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika fani ya Mitambo au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

3.MHANDISI MAJENGO (CIVIL ENGINEER) Nafasi 1  Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika fani ya Ujenzi au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

2. MHANDISI UMEME (ELECTRICAL ENGINEER) Nafasi 1  Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika fani ya Umeme au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).


3. OFISA MAZINGIRA (ENVIRONMENTAL OFFICER) Nafasi 1  Unguja 
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika fani ya Sayansi/Sanaa ya Mazingira au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

4. FUNDI MCHUNDO UMEME DARAJA LA  III ( Nafasi 1Unguja na 1 Pemba )
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye Stashahada ya kawaida au FTC katika fani ya umeme au cheti chengine kinachofanana na hicho kutoka katika taasisi inayotambulika na serikali.
  




5. FUNDI SANIFU UMEME DARAJA LA  III ( Nafasi 3 Unguja )
Sifa za Kuingilia Kazini
 Mwenye cheti katika fani ya Umeme au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 


6. FUNDI SANIFU KUCHONGA (CARPENTER) Nafasi 1 Unguja

Sifa za Kuingilia Kazini
 Mwenye cheti katika fani ya ufundi  kuchonga au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 


7. FUNDI SANIFU KUCHONGA (ALLUMINIUM) Nafasi 1 Unguja

Sifa za Kuingilia Kazini
 Mwenye cheti katika fani ya ufundi  kuchonga au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 


8. FUNDI MCHUNDO BOMBA (PLUMBER) DARAJA LA  III ( NAFASI 1 UNGUJA)
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye Stashahada ya kawaida au FTC katika fani ya Ufundi Bomba au cheti chengine kinachofanana na hicho kutoka katika taasisi inayotambulika na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 


9. MUEGESHA NDEGE MSAIDIZI DARAJA LA III (nafasi  6 Unguja, 2 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye cheti cha kidatu cha nne pamoja na cheti cha masomo ya Uegeshaji wa Ndege (Appron Management)  au  cheti  kinachofanana na hicho ambacho kimetolewa na Mamlaka inayotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 


10. KATIBU MUKHTASI DARAJA LA III ( Nafasi 3 Unguja)
Sifa za kuingilia kazini 
Mwenye Diploma/Stashahada ya fani ya Uhazili kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



11. OFISA BIASHARA DARAJA LA II ( nafasi 1 Unguja na 1 Pemba)
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika fani ya Masoko, Biashara, Utawala na Uchumi, Sheria za Kibiashara au fani nyengine inayolingana nazo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


12. MHASIBU MSAIDIZI DARAJA LA III (nafasi 1 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye Stashahada ya kawaida ya Uhasibu au Uongozi wa Fedha kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


13. MHUDUMU VIP DARAJA LA II (nafasi 2 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini 
Mwenye cheti cha kidatu cha nne au sita na hicho kutoka katika mamlaka inayotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Mwenye uzoefu wa kuwahudumikia viongozi atapewa kipau mbele.



14. DEREVA DARAJA LA III (nafasi 1 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye cheti cha Kidato cha nne aliyefaulu na kupata leseni ya gari kutoka katika Mamlaka inayotoa leseni na kutambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 



15. a) OFISA WA MIFUMO YA KOMPYUTA DARAJA LA II (System Administrator)  nafasi moja Unguja na moja Pemba

b) OFISA WA MITANDAO YA KOMPYUTA  DARAJA LA II (Net Works Engineer) nafasi moja Unguja.

c) OFISA WA KUKIMU MIFUMO YA KOMPUTA (IT Service/Support Engineer) nafasi moja Unguja

d) OFISA  MUENDELEZAJI MIFUMO YA KOMPUTA (System Developer) nafasi mbili Unguja
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye Shahada ya Kwanza /Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika fani ya Sayansi ya Kompyuta/habari ya Kompyuta au fani nyengine inayolingana nazo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.  

Kufanya kazi nyengine zinazolingana na kazi yake kama atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.









Jinsi ya Kuomba 
Barua za maombi  zielekezwe kwa:-
Mkurugenzi Mkuu 
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
S.L.P 4742
Zanzibar 

Barua hizo ziambatanishwe na taarifa binafsi ya muombaji (CV), Vivuli vya Cheti cha kuzaliwa, Kitambulisho cha Ukaazi cha Zanzibar na vyeti  vya masomo.

Siku ya mwisho ya kupokea maombi hayo ni siku ya Jumatano ya tarehe 04/08/2017.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.