Na Ali Othman.
Naibu waziri wa Elimu na mafunzo ya Amali Mh. Mmanga Mjengo
Mjawiri amepokea Cheti cha shukrani kutoka kwa Taasisi ya Rafiki Network
kutokana na juhudi na mchango wake mkubwa aliotoa katika kufanikisha Bonanza la
kihistoria la kimichezo lililoandaliwa na taasisi hiyo kisiwani Pemba.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa cheti na Rais wa Taasisi ya Rafiki Network Bw. Hamad
Hamad ofisini kwake Mazizini nje kidogo ya mji wa Zanzibar, Mh Naibu Waziri
amesema ipo haja ya kufufua michezo iliyosahauliwa ya Kipemba ili kuibua
burudani ambazo amesema kwasasa zimekua adimu.
“Watu wanataka burudani kwasababu zimekua adimu hivyo ni vizuri
kuendelea na kufufua michezo iliyosahauliwa ikiwemo michezo ya kivita ya
kipemba (martial arts) kama vile Ngware na Kirumbizi” Amesema Mh. Mmanga.
Akielezea juu ya kuridhishwa kwake na juhudi za Taasisi ya
Rafiki Network katika kuandaa na kusimamia Tamasha la kimichezo kisiwani Pemba
lijulikanalo kama “Pemba Weekend Bonanza”, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema
Taasisi ya Rafiki Network imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuamsha hisia za watu
kiburudani zinazohusiana na michezo yao ya kiasili.
Aidha Mh. Waziri amesema burudani zimekua adimu kisiwani
Pemba ambapo ametumia kigenzo cha wananchi kujitokeza kwa wingi katika tamasha
la Pemba Weekend Bonanza kuwa ni ishara tosha ya kuadimika kwa michezo na
burudani kisiwani Pemba. Ameongeza kua michezo ni muhimu sana kwa kuwaunganisha
watu.
Taasisi ya Rafiki Network iliandaa tamasha kubwa la
Kimichezo Kisiwani Pemba ambalo lilifanyika kuanzia tare 28 hadi 30 Julai
ambapo michenzo mbalimbali ikiwemo mchezo wa Ng’ombe, Resi za Baiskeli,
Mashindano ya Kuogelea na Resi za Ngalawa yalifanyika ambapo washindi na
washiriki walizawadiwa.
No comments:
Post a Comment