Habari za Punde

Profesa Msambichaka Asisitiza Nidhamu Kwa Wanafunzi na Walimu Ili Kuinua Elimu Wakati Akizindua Kampeni ya 3D


 WALIMU, Wanafunzi na Wafanyakazi katika shule mbalimbali wametakiwa kuzingatia nidhamu shuleni ili kuweza kuchochea maendeleo ya ufaulu kwenye shule zao.Wito ulitolewa jana na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya John Baptist iliyopo Boko Basihaya jijini Dar es Salaam, Aspiter Kibona wakati wa mahafali ya 10 ya kidato cha nne ya shule hiyo yaliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya '3D' yenye maana ya !Nidhamu, Nidhamu, Nidhamu!.
Kibona alisema wameamua kuzindua kampeni hiyo ikiwa ni kauli mbio yao kwa wanafunzi wa shule hiyo pamoja na walimu na wafanyakazi wengine kuzingatia nidhamu muda wote ambayo itaendelea kuchochea maendeleo ya ufaulu kwa wanafunzi wa shule hiyo.
"Nidhamu si kwa wanafunzi pekee bali inatakiwa kuanzia hata kwangu mimi mkuu wa shule pamoja na walimu na wafanyakazi wengine katika shule yetu hii, hivyo tumezindua kampeni hii ikiwa ni kauli mbio yetu ya kuendelea kuhamasisha nidhamu katika shule yetu kwa nia kuendelea kuchochea maendeleo ya wanafunzi kufanya vizuri katika masomo yao darasani, " alisema Kibona.
Alisema nidhamu inapoanzia kwa viongozi wa juu, walimu na wafanyakazi wengine inasaidia nidhamu hiyo hiyo kuingia hadi kwa wanafunzi ambayo inawachochea kufanya vizuri katika masomo yao darasani.
Naye Mkurugenzi wa shule hiyo, Jalia Mayanja aliwataka wahimu 53 wa kidato cha nne kuzingatia nidhamu mahali popote watakapokuwa mara baada ya kutoka shuleni hapo kwa faida yao ya huko waendako.
Mayanja alisema nidhamu ndiyo siri ya mafanikio ya shule hiyo katika ufaulu kwa wanafunzi wa shule hiyo.
Alisema ni vema wahitimu hao wa kidato cha nne wakaendeleza nidhamu waliyokuwa wakiionyesha shuleni hapo huko wanapokwenda ili iweze kuwasaidia katika maisha yao ya baadae.
Aliongeza kwa kuwataka wazazi wanaopeleka watoto wao katika shule hiyo kukaa kwa amani kutokana na kwamba wapo katika mikono salama.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.